Simon Mathias Kipala tumaini jipya UVCCM mpya

Simon Mathias Kipala tumaini jipya UVCCM mpya

Ana uwezo wa kununua mapanga mangapi kwa ajili ya uchaguzi wa 2020?
 
Nawaambia wana CCM kwamba uwepo wa upinzani imara ulisaidia sana hata wanaCCM, kwa sababu kujuana kulipungua wakihofia kumchagua mbovu atashindwa kwani kuna mgombea wa upinzani. Nashangaa vijana wa CCM wakifurahia kuuawa kwa upinzani. Mkubali msikubali tutakapo rudi kwenye mfumo wa chama kimoja au kwenye upinzani dhaifu nanyi ndani ya CCM mtakula hasara. Hawatapitishwa watu kwa ubora wao bali watapitishwa watu kwa kujuana na fedha au rushwa. Upinzani imara uliibana CCM ifikirie mara mbilimbili mtu wa kumpitisha kwenye nafasi fulani ya kugombea. Anayebisha haya ataona mbeleni yatakayotokea tukirudi kwenye mfumo wa chama kimoja.
 
Cku hizi humu JF MTU akiwa Msukuma akipata kinafasi kizuri lazima anaonekana kagushi jambo Fulani.Jamani wasukuma popote walipo wanawafikiriaje? Hawa watu hawana shida kabisa wanapenda watu wrote pasipo kubagua makabila ya wengine.Muhimu tudumishe upendo wetu km rais wetu amekuwa akituasa!!!
 
Siyo kila kipala kina busara hata wapumbavu wanazeeka FISIEMU ni ileile
 
Inasikitisha kuona Mh, Magufuli kwenye vikao kaacha ripoti ya usalama wa Taifa kupitisha majina ya wagombea ktk Jumuiya za chama na kutumia ripoti ya; Paul Makonda, Polepole na Simoni Mathias kipala.

Mara baada ya kuchukua na kurejesha fomu tarehe 10/7/2017 Mh, Magufuli aliagiza vyombo vya usalama kufanya vetting ya wagombea wote kuanzia wilaya mpaka taifa kwa chama na jumuiya zake, cha kushangaza katika wilaya na mikoa katumia ripoti ya usalama lkn ilipofika ngazi ya Taifa kaacha ripoti ya usalama wa Taifa na maadili chama baada ya kuona watu wake wa karibu hawajapendekezwa

Mfano, katika Jumuiya ya UVCCM Taifa idara ya usalama ilipendekeza watu sita kutoka 113 ambao ni;
1,Sofia mfaume Kizigo
2.Khadija Shabani (Keisha)
3.Omary Jabiri
4.Josamu Kengia
5.Suleimani Serera na
6.Mwita Nyarukururu

Majina haya baada ya kupendekezwa alipewa Kaimu Katibu mkuu wa uvccm Taifa (shaka), baasha nyingine kapewa Katibu wa organization na kumpelekea Mh, Magufuli ikulu

Lkn cha kushangaza Mh, magufuli kaacha haya mapendekezo ya usalama wa Taifa na kutumia mapendekezo ya Makonda na polepole,

Ushauri wangu kwa Vijana wa ccm tuwe makini tusikubali watu watumie ccm kama chombo cha ukoo flani hawa watu wanaharibu chama chetu
Sizonje na ziro brain wana ajenda binafsi funga mdomo ikibidi shona Kwa uzi
 
Huyu Kipala amegushi umri, ameenda Rita kabadili vyeti vya kuzaliwa bado tunajidanganya kuwa atapambana na Rushwa, CCM leo imebadilika inaongozwa na wasukuma hata kama hawana sifa wakati wameachwa Vijana wenye sifa bila kujadiliwa hii dhambi itawatafuna[/QUO
huyu ni Mpambe wa Paul Makonda,na mkimpa huyu hiyo nafasi mmekwisha
kaghushi vyeti kama kaka yake Ma.Ko.nda.?
 
Huyo nae ni mpwa wake.....amejaza wapwa wake wengi sana...wengine wamemzunguka pale kumlinda wengine wako hazina wengine Mayanga constructions....wengine uvccm....daaaa awamu ya visasi na ukabila....n ufamilia!!! Mud taongeaaa
Time will tell nukuu from lema
 
Chama cha Mapinduzi kama ilivyo desturi yake kinaendelea na chaguzi zake na mara hii ni ndani ya jumuiya zake za wazazi,wanawake na jumuiya muhimu ya vijana UVCCM.

Leo nitajikita ndani ya jumuiya ya vijana UVCCM Taifa na hasa kwa huyu Simon Mathias Kipala. Huyu kwa mnaokumbuka vizuri amewahi kuwa Rais wa serikali ya wanafunzi pale Mlimani (UDSM) maarufu kama DARUSO, pia amewahi kuwa mwenyekiti wa shirikisho la vyuo vikuu yaani TAHLISO.
Mathias Kipala kama anavyojulikana na wengi amekuwa kwa Muda fulani mtumishi wa chama makao makuu na katibu msaidizi Ukerewe.

Kutokana na sifa hizo na nyingine kadhaa anastahili na nadiriki kusema ndiye miongoni mwao mwenye uzoefu, ushawishi, nia,uadilifu na uwezo wa kuirudishia jumuiya hii makali iliyokuwa nayo huko nyuma, akiwa amebobea kwenye sayansi ya siasa na utawala anao uwezo huo wa kuiongoza jumuiya hii kikamilifu na tena kwa kasi ya mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Mh Dkt Magufuli ili kuleta maana na matendo ya mageuzi chanya ndani ya CCM na serikali kwa kuisimamia kikamilifu serikali ambayo imepewa ridhaa ya kuongoza Tanzania kwa kutimiza kikamilifu ahadi ilizoahidi kipindi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

Mara kadhaa Mh Rais amenukuliwa akiishangaa jumuiya hii kujitenga mbali na majukumu na wajibu wake na hasa kuandaa vijana ambao ndio wenye jukumu la uongozi kwa falsafa yake (Mh Magufuli).
UVCCM MPYA inamhitaji sana Kipala ili kuelekea 2019/2020 chama kiwe imara zaidi kushiriki na kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu tukiwa wamoja, wenye ari na mbinu bora zaidi.

Ni matumaini yangu kuwa kwa haya machache niliyoyabainisha hapa wapigakura wote mtakapokutana Dodoma mtamchagua kiongozi huyu shupavu, imara, mcha Mungu, mwadilifu ili aende kuiongoza UVCCM MPYA katika kutekeleza majukumu yake ya msingi kikamilifu.

UVCCM MPYA inamhitaji Simon Mathias Kipala na hakika ndiye chaguo letu na kamwe tusikubali maneno ya hujuma Kwani watani zetu hawapendi safu imara maana wameuona moto wetu kwenye uchaguzi mdogo, hivyo tuendelee kupeleka majonzi Kwao tena kwa mbinu za kisasa zaidi na ari zaidi.

M Jr
Hahaha
 
Chama cha Mapinduzi kama ilivyo desturi yake kinaendelea na chaguzi zake na mara hii ni ndani ya jumuiya zake za wazazi,wanawake na jumuiya muhimu ya vijana UVCCM.

Leo nitajikita ndani ya jumuiya ya vijana UVCCM Taifa na hasa kwa huyu Simon Mathias Kipala. Huyu kwa mnaokumbuka vizuri amewahi kuwa Rais wa serikali ya wanafunzi pale Mlimani (UDSM) maarufu kama DARUSO, pia amewahi kuwa mwenyekiti wa shirikisho la vyuo vikuu yaani TAHLISO.
Mathias Kipala kama anavyojulikana na wengi amekuwa kwa Muda fulani mtumishi wa chama makao makuu na katibu msaidizi Ukerewe.

Kutokana na sifa hizo na nyingine kadhaa anastahili na nadiriki kusema ndiye miongoni mwao mwenye uzoefu, ushawishi, nia,uadilifu na uwezo wa kuirudishia jumuiya hii makali iliyokuwa nayo huko nyuma, akiwa amebobea kwenye sayansi ya siasa na utawala anao uwezo huo wa kuiongoza jumuiya hii kikamilifu na tena kwa kasi ya mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Mh Dkt Magufuli ili kuleta maana na matendo ya mageuzi chanya ndani ya CCM na serikali kwa kuisimamia kikamilifu serikali ambayo imepewa ridhaa ya kuongoza Tanzania kwa kutimiza kikamilifu ahadi ilizoahidi kipindi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

Mara kadhaa Mh Rais amenukuliwa akiishangaa jumuiya hii kujitenga mbali na majukumu na wajibu wake na hasa kuandaa vijana ambao ndio wenye jukumu la uongozi kwa falsafa yake (Mh Magufuli).
UVCCM MPYA inamhitaji sana Kipala ili kuelekea 2019/2020 chama kiwe imara zaidi kushiriki na kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu tukiwa wamoja, wenye ari na mbinu bora zaidi.

Ni matumaini yangu kuwa kwa haya machache niliyoyabainisha hapa wapigakura wote mtakapokutana Dodoma mtamchagua kiongozi huyu shupavu, imara, mcha Mungu, mwadilifu ili aende kuiongoza UVCCM MPYA katika kutekeleza majukumu yake ya msingi kikamilifu.

UVCCM MPYA inamhitaji Simon Mathias Kipala na hakika ndiye chaguo letu na kamwe tusikubali maneno ya hujuma Kwani watani zetu hawapendi safu imara maana wameuona moto wetu kwenye uchaguzi mdogo, hivyo tuendelee kupeleka majonzi Kwao tena kwa mbinu za kisasa zaidi na ari zaidi.

M Jr
Huyu jamaa amefariki Dunia.
May his soul rest in eternal Peace.
Simon Mathias Kipala is no more.
 
Ndo hiyu kafia Mzena hospital na mwili wake umehifadhiwa Lugalo hospital?
 
Back
Top Bottom