Simiyu Usione vyaelea ujue vimeundwa

Simiyu Usione vyaelea ujue vimeundwa

Donald Bakari

Member
Joined
Sep 4, 2020
Posts
32
Reaction score
30
SIMIYU: “USIONE VYAELEA UJUE VIMEUNDWA.”

Na Donald Bakari.

download.jpg


Mnamo tarehe 13 Machi 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli alimteua kijana mwerevu, mnyenyekevu na asiye na mihemko mwenye umri wa miaka 33 Anthony Mtaka kuwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu. Mtaka akaingia katika vitabu vya kihistoria na kuwa mmoja wa wakuu wa mikoa wenye umri mdogo kuwahi kutokea nchini.

Hakutaka kiki, aliitazama ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015 – 2020, kwa upole, busara, hekima na maarifa akaianza kazi na kututimizia maneno ya wahenga yanayosema “Usione vyaelea ujue vimeundwa”.

JPM leo (04/09/2020) atakuwa pale mkoani Simiyu kunadi sera za CCM na kuomba ridhaa ya kuchaguliwa kwa kipindi cha pili katika nafasi ya urais. Kazi yake itakuwa nyepesi sana kwa sababu Mtaka na watendaji kazi wengine walishaviunda na sasa vinaelea.

Yafuatayo ni baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika Mkoa wa Simiyu.
  • Uzinduzi wa muongozo wa uwekezaji umebaini na kunadi fursa za uwekezaji katika mkoa wa Simiyu.
Mtaka ameutendea kazi muongozo huu, mkoa wa Simiyu umefungua fursa za uwekezaji na kunufaika nao. Katika hili JPM ataomba kura bila jasho.
  • Kujengwa kwa hospitali ya rufaa katika mkoa mpya wa Simiyu.
Simiyu ni moja ya mikoa michanga, Serikali ya awamu ya tano ikaamua kujenga hospitali ya rufaa ya Simiyu kwa lengo la kusogeza huduma za rufaa karibu na wananchi kwa sababu Simiyu ni mkoa mchanga kwa namba za kuanzishwa ila sio kwa kuweza kujitegemea. Hapa Chama Cha Mapinduzi na JPM wataomba kura kwa lugha nyepesi sana.
  • Utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji na wa kimkakati wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya mazingira mkoani Simiyu (Simiyu Climate Resilience Water Project).
Mradi huu una thamani ya shilingi bilioni 400, ukigharamiwa na Serikali ya Tanzania, Shirika la GCF na Serikali ya Ujerumani. Mtaka ameusimamia barabara, ameshaunda JPM ataomba kura na kuondoka kwa furaha.
  • Ujenzi wa mahakama ya Hakimu Mkazi wa Simiyu umekamilika.
Chama cha Mapinduzi kinazingatia utoaji wa haki, Ujenzi wa mahakama ya hakimu mkazi umetimiza azma ya wengi ya kuona huduma za kimahakama zinapatikana kwa ubora na wakati. JPM atawapungia mkono wananchi wa Simiyu, nao watampa kura bila kinyongo.
  • Ujenzi wa nyumba ya mkuu wa mkoa wa Simiyu na katibu tawala wa mkoa wa Simiyu umekamilika.
Serikali ilihakikisha watendaji hawa wa mkoa wanakuwa na makazi bora, unajua nini kilifuata? Mtaka na wenzake wakaiongoza Simiyu katika kuhakisha wanafunzi pale Simiyu wanafaulu. Walipigana kufa na kupona kuhakisha Simiyu inapaa katika elimu.

Ukienda pale NECTA watakuambia Simiyu huwa haikosi kumi bora katika matokeo. JPM akifika atawaeleza kuhusu elimu bure, wananachi watasema watoto wetu wanasonga mbele kielimu kura zote Kwako JPM mzalendo wa nchi.
  • Kuongeza uwezo wa kuhifadhi mazao kwa kujenga ghala lenye uwezo wa kuhifadhi tani 34,000.
Usichukulie poa, Serikali iliamua. Pamba ni dhahabu nyeupe inatakiwa kuhifadhiwa vema. Mtaka alisimamia vema, JPM atasisitiza juu ya kujenga viwanda vya kutengeneza nguo zetu wenyewe na kuachana na mitumba, atafunga na kuondoka na kura zake kedekede.

Tuendelee kufurahia mafanikio makubwa na yenye tija yaliyopatikana katika Serikali ya awamu ya tano na tuwasisitize watanzania kuendelea kufanya kazi kwa bidii. “Kwa pamoja tumekeleza kwa kishido, tunasonga mbele pamoja” kura kwa JPM na Chama Cha Mapinduzi.

Wenu Donald Bakari

Email: donaldbakari4@gmail.com
 
Anthony Mtaka ni bonge la RC/kiongozi na siyo mtawala, sema sababu yupo CCM ndiyo hivyo tena.
Ni kweli, Mhe. Mtaka ni moja kati ya viongozi wachache sana ambao ni hazina kwa taifa. Mwenyezi Mungu amjalie afya njema na maisha marefu
 
Nje ya mada, kwahiyo mtaka is now 38 yrs. Duu najuta kumpa shikamoo yangu last year nilipokutana naye ofsini kwake bariadi. Dah Basi ana mwili mbaya Sana afanye fanye mazoezi Basi.
 
Nje ya mada, kwahiyo mtaka is now 38 yrs. Duu najuta kumpa shikamoo yangu last year nilipokutana naye ofsini kwake bariadi. Dah Basi ana mwili mbaya Sana afanye fanye mazoezi Basi.
Daaah, pole kawaida kuna baadhi ya watu kwa umbo unaweza kuwaona wakubwa kumbe ni wadogo. Naamini siku ukikutana naye ukamwambia atakurudishia.
 
Licha ya kuwa na sera zenye misingi ya utekelezaji, lakini pia usimamizi na viongozi bora wa kumsaidia ni msingi mzuri wa mafanikio ya JPM kuanzia mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya.
Magufuli anatosha
 
Nje ya mada, kwahiyo mtaka is now 38 yrs. Duu najuta kumpa shikamoo yangu last year nilipokutana naye ofsini kwake bariadi. Dah Basi ana mwili mbaya Sana afanye fanye mazoezi Basi.
Ndiyo zitakuwepo, zitakuwa vinatumwa hapa ili tuendelee kujenga nchi yetu na kushirikishana maarifa
 
Yaani nikiona watu wanatumia muda na nguvu nyingi kueleza walichokifanya,huwa napata shida kama wamefanya kitu kweli,kwanini mliyoyafanya yasijieleze yenyewe kwa watu,
 
Yaani nikiona watu wanatumia muda na nguvu nyingi kueleza walichokifanya,huwa napata shida kama wamefanya kitu kweli,kwanini mliyoyafanya yasijieleze yenyewe kwa watu,
ndomana mwalimu anatunga mtihani upate asilimia mia, ila wewe unachagua kupata sifuri, wengine mnaelewa taratibu
 
Huo mradi wa maji umekamilika wapi wewe wakati nyuma tu ya hapo mkutano unapofanyikia leo hawana maji, Kuna kimto kidogo hapo nyuma shule ya msingi bariadi hakuna daraja watoto wanachelewa shule wanasubiri maji yapungue ndiyo wavuke.​
Uwekezaji na viwanda upo wapi hapo Simiyu.​
Mtaka yupo overated tu sioni alichofanya kwa Simiyu.​
Viwanda havionekani ni propaganda tu za kisiasa.​
 
Licha ya kuwa na sera zenye misingi ya utekelezaji, lakini pia usimamizi na viongozi bora wa kumsaidia ni msingi mzuri wa mafanikio ya JPM kuanzia mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya.
Magufuli anatosha
Yap, umeongea vema na barabara. Viongozi imara ni chanzo.
 
Back
Top Bottom