Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt. Boniphace Marwa amesema Mkoa huo haufanyi vizuri katika mapokeo ya Chanjo licha ya Maambukizi kuwepo pamoja na Vifo vya Wagonjwa
Dkt. Marwa amesema sababu zinazopelekea mwamko mdogo wa Wananchi ni pamoja na sababu za kijamii na Elimu ya Chanjo kutowafikia Watu wengi
Amewataka Wananchi wanaougua kufika kwa haraka kwenye Vituo vya Afya ili kupata matibabu pamoja na Serikali kupata takwimu za hali ya tatizo jinsi lilivyo.