Hustler_
Member
- Jan 17, 2022
- 42
- 41
Simba yaondoka kwa mafungu mafungu kwenda misri? Nini shida
Kikosi cha Simba kimeondoka nchini leo Julai 14 mchana kwenda nchini Misri huku katika msafara wao walikuwepo wachezaji 19, benchi la ufundi pamoja na kiongozi mmoja ambaye ni Meneja wa habari na mawasiliano Ahmed Ally.Wachezaji walioondoka walikuwepo, Shomari Kapombe, Ally Salim, Benno Kakolanya, Gadiel Michael, Erasto Nyoni, Pape Sakho, Chris Mugalu, Augustine Okrah, Meddie Kagere, Jimson Mwanuke, Victor Akpan na Habibu Kyombo.
Wengine, Clatous Chama, John Bocco, Israel Mwenda, Joash Onyango, Henock Inonga na wengine wawili ambao hawakuonekana.
Kocha msaidizi wa Simba, Selemani Matola alisema katika muda wao wa maandalizi ya msimu ujao watafanya mazoezi aina mbalimbali pamoja na kucheza mechi za kirafiki.
Matola alisema ndani ya wiki ya kwanza tu watacheza mchezo mmoja wa kirafiki kutokana na ratiba ya kocha mkuu, Zoran Maki ilivyo.
“Timu itakuwa Misri kwa makundi matatu la kwanza ndio hili la leo, lingine ni wale ambao viza zao zimechelewa kutoka na kundi la mwisho litakuwa wale waliopo kwenye kambi ya Taifa Stars,” alisema Matola.
Baada ya kambi ya huko Misri kikosi cha Simba kitarejea nchini Agosti 5, kwa ajili ya maandalizi wiki ya Simba pamoja na mchezo wa ufunguzi wa msimu dhidi ya watani zao Yanga utakaopigwa Agosti 13, Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Source: vanforumtz.com