Simba Sports Club. Rasmi sasa Mnapaswa kulipa Deni la Magufuli

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Oct 31, 2014
5,360
11,513
Njia pekee ya kumuenzi kwa mema yake na uchapakaji kazi ni ninyi Kuleta Kombe la CAF hapa Tanzania. Hili ndilo Deni mlilo nalo kwa Marehemu JPM aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tunaomba Mlete Kombe la CAF TANZANIA. HALAFU SISI NA NINYI YANGA MTAVAA JERSEY ZENU ZA NJANO NASI NYEKUNDU TUTABEBA BENDERA YA TAIFA NA KUSIMAMA UWANJA WA TAIFA TUKIIMBA MUNGU IBARIKI TANZANIA.

TUTAWEKA USHABIKI NA UNAZI WETU PEMBENI. TUTASHEREHEKEA PAMOJA NA KUFURAHI PAMOJA KAMA WATANZANIA. TUISHANGAZE DUNIA.

SIMBA hili ndilo mnalopaswa kulibeba kwa sasa kuanzia leo. Msiongeze huzuni tena juu ya huzuni Mioyoni mwetu.
 
Labda hilo kombe tukaliibe! Ila siyo kwa kulichukua kupitia zile dakika 90! Siyo kwa timu ya Wananchi, siyo kwa hao mbumbumbu!

Labda kwa miaka ijayo! Baada ya kufanya uwekezaji ulio tukuka nje na ndani ya uwanja.
 
Back
Top Bottom