Simba SC bora iachane na Chama

Ayenda M

Member
Jan 4, 2018
97
132
Maisha yetu binadamu yamezungukwa na mambo mengi sana. Kuna wakati kwenye maisha ukweli na uongo huamua kujitenga ili maisha halisi yajidhihilishe.

Ni kawaida ya wanadamu wote hasa waafrika kudevelop ego hasa pale wanapoona wao ni wa muhimu sehemu fulani. Sijui nani alituloga sisi ngozi nyeusi.

Huwa tuna imani kuwa kwa kuwa tunafanya kazi fulani, hakuna wa kuifanya kazi ile kuliko sisi au karibu na uwezo wetu. Hapana, tuache kuvimba... kuna mamilioni ya watu wanasubiri uchomolewe waoneshe ubora wao hata kuliko wewe.

Juzi nimeona stori ya Chama na Simba. Nikacheka. Kwa nini nilicheka na naendelea kucheka kila nikisoma makala za baadhi ya wachambuzi wetu wa Bongo.

Miaka ya hivi karibu hasa kipindi cha usajili Chama amekuwa akiichezesha Simba SC kama anavyotaka yeye. Anaisumbua kweli kweli Simba na maneno ya hapa na pale! Kipjndi chote hicho, Simba kama taasisi haijawahi kufanya maamuzi ya tofauti.

Ila Juzi imeamua kutoka na kufanya walichofanya. Simba SC imemchoka Chama, Chama hajaichoka Simba bali alitikisa kiberiti kuona. Show ilianza Chama siku hizi anacheza kifather sana. Anaonesha hana tena ile kiu ya mafanikio na kuipambania Simba SC.

Naamini chini ya Benchikha, Uongozi umuache Chama aondoke. Waishi maisha mengine bila Chama. Na inawezekana.

Walikuwepo akina Kichuya kona, Okwi na Kagere.... tuachane na wazee wetu akina Zamoyoni na wengine waliopita ila Simba bado ipo na itaendelea kupita.

Chama hataki kuiheshimu Simba Sc na ni muda sahihi wamuache aende haijalishi anaenda wapi. Simba iachane na Chama haraka sana kwa mstakabari wa mafanikio yake ya baadae.

Ahsante.
 
Simba kwasasa Haina uwezo wa kucheza mechi tatu bila Chama. Kwa Hali Inavyo elekea kama Simba itakosa matokeo ni lazima kocha au viongozi watakua kwenye presha kubwa.

Hakuna Kiongozi wa kuthubutu kumwazibu Chama adhabu yoyote itakayo mkera Chama zaidi ya onyo na mikwala mingine ya Ki mjini.

Simba haiwezi kusonga mbele kwasasa bila Chama kwakua time ipo upande wa Chama na si kwa mashabiki, kocha Wala Viongozi.

Muda una mmbeba Chama, Wakati uongozi ulipata muda uko nyuma wakafanya maamuzi mabaya, Sasa hawana jinsi kwakua muda umesha shift.
 
Simba kwasasa Haina uwezo wa kucheza mechi tatu bila Chama. Kwa Hali Inavyo elekea kama Simba itakosa matokeo ni lazima kocha au viongozi watakua kwenye presha kubwa...
Kwahiyo unataka kusema siku chama akiacha soka Simba nayo inakufa?
 
Kwahiyo unataka kusema siku chama akiacha soka Simba nayo inakufa ?
Muda wa kuachana na Chama ulikuwepo Waka acha upite, kwasasa Simba kama itaamua iachane na Chama lazima walipie gharama za makosa yaliyopita.

Lazima wavumilie timu ikiwa inakosa matokeo mpaka timu ikae sawa.

Kwakua yeye alitengenezwa kama uti wa mgongo wa timu Sasa wakubali kuishi bila uti wa mgongo walio utengeneza ili wajipange upya.

Kwasasa dirisha dogo unaweza kupata au kukosa mtu kama yeye.

Je, Mashabiki wapo tayari kuvumilia matokeo yoyote ya mpira?
 
Chama atachukuwa namba ya Nani Yanga? Aziz Ki au Pacome?
Anayetoa hela ya kumsajili ndio anayejua atachukua nafasi ya nani.

Raisi wenu mwenyewe anamkubali Chama mara kibao ame declare kumtaka Chama ila fursa hiyo hakuipata.
 
Muda wa kuachana na Chama ulikuwepo Waka acha upite, kwasasa Simba kama itaamua iachane na Chama lazima walipie gharama za makosa yaliyopita.
Lazima wavumilie timu ikiwa inakosa matokeo mpaka timu ikae?
Huo muda ulikuwa ni muda upi?

Kwani matokeo mabaya tunayopata na Chama akiwemo tumewezaje kuvumilia?

Na vipi tukikuambia most ya hayo matokeo mabaya yamechangiwa na Chama mwenyewe?

Chama anaondoka Simba and you will never notice his gap
 
Muda wa kuachana na Chama ulikuwepo Waka acha upite, kwasasa Simba kama itaamua iachane na Chama lazima walipie gharama za makosa yaliyopita.
Lazima wavumilie timu ikiwa inakosa matokeo mpaka timu ikae
Ni bora kutafuta mchezaji mbadala wa chama kwani hata akiachwa kwa sasa,anacheza vibaya maksudi ili atukomoe.

Hatujui Simba tumemkosea nini!
Anatuchomesha mradi yanga wafurahi.

Ni bora aende huko anakopapenda ni muda muafaka
 
Muda wa kuachana na Chama ulikuwepo Waka acha upite, kwasasa Simba kama itaamua iachane na Chama lazima walipie gharama za makosa yaliyopita.
Lazima wavumilie timu ikiwa inakosa matokeo mpaka timu ikae sawa.
Kwakua yeye alitengenezwa kama uti wa mgongo wa timu Sasa wakubali kuishi bila uti wa mgongo walio utengeneza ili wajipange upya.
Kwasasa dirisha dogo unaweza kupata au kukosa mtu kama yeye.
Je! Mashabiki wapo tayari kuvumilia matokeo yoyote ya mpira?
Hapo kwenye kuvumilia matokeo ndo kipengele kilipo ila Chama angeachwa tu.
 
Simba kwasasa Haina uwezo wa kucheza mechi tatu bila Chama. Kwa Hali Inavyo elekea kama Simba itakosa matokeo ni lazima kocha au viongozi watakua kwenye presha kubwa....
Wazee mikono yenu ina Ushirikiano na Ubongo kweli?

Chama awepo asiwepo simba inacheza vibaya.

Huyu ni mwalimu mpya bodo hamtegemei Chama.

Hili ni dirisha la Usajili. Wakikaza vizuri wanapata mchezaji hata wa Mkopo
 
Back
Top Bottom