kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,247
- 16,169
Kama ukiwasikiliza wazee wa Simba unaweza kusema ni wazee wa mtaani tu.
Wazee wa Simba wanaongea, kusema na kutenda kama vijana wengine wa simba.
Wazee wa Simba walipaswa kushauri viongozi wa Simba wakatae udhamini wa Azam kwenye ligi maana Azam anayo timu inayoshiriki ligi kuu ya NBC pia.
Wazee wa Simba walipaswa kujua kuwa Simba (isiyodhaminiwa na GSM) pia imefungwa magoli mengi na Yanga mara 4 mfululizo sasa.
Wazee wa Simba walipaswa kumshauri mo, mdhamini wao azifadhili zile timu 8 ambazo hazina ufadhili wa GSM kama wanadhani kufadhili timu nyingi ni sababu ya kupata ushindi. kwanini wanaiacha hii fursa?
Wazee wa Simba wanasahau kuwa timu zetu zinahitaji wadhamini wengi ili kusaidia kuimarisha timu zao kwenye ligi. Wanataka timu zikose hata nauli ya kusafiri kwenda kwenye mechi ili iwe rahisi kwao kuuza mechi.
Wazee wa Simba hawajui kwamba kosa la kuzuiwa kufanya mazoezi kwenye uwanja hukumu yake sio kuahilisha mechi. Wana madai ambayo yanachosha masikioni kuyasikiliza, kama watoto.
Wanashindwa kutoa maelezo juu kwanini Simba haikuadhibiwa baada ya kuwasajili wachezaji wenye mikataba hai na timu nyingine kinyume cha kanuni.
Hawaelezi ni kwanini TFF imeruhusu ligi kuwa na wachezaji wengi wageni. Idadi hii kubwa ya wachezaji ilikuja wakati Yanga haina mdhamini baada ya Yusuf manji kuondoka na mo kuwa mdhamini wa Simba. TFF ilidhamiria kuinufaisha Simba pekee yenye nguvu ya fedha wakati huo.
Wazee hawa hawashangai kwanini kuondoka kwa Feitoto Yanga ilitumika busara lakini kuondoka kwa Dube Azam ilitumika kanuni.
Wazee hawasemi kwanini Simba wana magoli mengi ya penati na ya hivihivi tu.
Wana wazee wa hivihivi tu.
Wazee wa Simba wanaongea, kusema na kutenda kama vijana wengine wa simba.
Wazee wa Simba walipaswa kushauri viongozi wa Simba wakatae udhamini wa Azam kwenye ligi maana Azam anayo timu inayoshiriki ligi kuu ya NBC pia.
Wazee wa Simba walipaswa kujua kuwa Simba (isiyodhaminiwa na GSM) pia imefungwa magoli mengi na Yanga mara 4 mfululizo sasa.
Wazee wa Simba walipaswa kumshauri mo, mdhamini wao azifadhili zile timu 8 ambazo hazina ufadhili wa GSM kama wanadhani kufadhili timu nyingi ni sababu ya kupata ushindi. kwanini wanaiacha hii fursa?
Wazee wa Simba wanasahau kuwa timu zetu zinahitaji wadhamini wengi ili kusaidia kuimarisha timu zao kwenye ligi. Wanataka timu zikose hata nauli ya kusafiri kwenda kwenye mechi ili iwe rahisi kwao kuuza mechi.
Wazee wa Simba hawajui kwamba kosa la kuzuiwa kufanya mazoezi kwenye uwanja hukumu yake sio kuahilisha mechi. Wana madai ambayo yanachosha masikioni kuyasikiliza, kama watoto.
Wanashindwa kutoa maelezo juu kwanini Simba haikuadhibiwa baada ya kuwasajili wachezaji wenye mikataba hai na timu nyingine kinyume cha kanuni.
Hawaelezi ni kwanini TFF imeruhusu ligi kuwa na wachezaji wengi wageni. Idadi hii kubwa ya wachezaji ilikuja wakati Yanga haina mdhamini baada ya Yusuf manji kuondoka na mo kuwa mdhamini wa Simba. TFF ilidhamiria kuinufaisha Simba pekee yenye nguvu ya fedha wakati huo.
Wazee hawa hawashangai kwanini kuondoka kwa Feitoto Yanga ilitumika busara lakini kuondoka kwa Dube Azam ilitumika kanuni.
Wazee hawasemi kwanini Simba wana magoli mengi ya penati na ya hivihivi tu.
Wana wazee wa hivihivi tu.