DELETED ACCOUNT
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 9,805
- 15,470
Kuna huu upotoshaji unaoendelea mitandaoni kuhusiana na uamuzi wa Serikali ya Rais Samia kuipa tafu klabu ya Simba katika mechi yake ya pili dhidi ya Stellenbosch huko Durban, South Africa.
Yamezuka maneno kutoka pande fulani zikisema Simba imepewa ndege halafu badala ya kubeba mashabiki wake wanaoipambania kila siku wamebeba watu wengine wasio na mchango wa kila siku katika timu.
Kwanza ninavyojua mimi, Simba haijapewa ndege bali imelipiwa nauli katika shirika la Air Tanzania ikiwa katika safari zake za kawaida kwenda South Africa. Siyo kila aliyekuwa kwenye ile ndege iliyoipeleka timu amelipiwa na Simba au serikali.
Kuhusu hao waandishi wa habari walioambatana na timu, wanaweza kuwa wamekwenda kwa pesa za taasisi zao au wanaweza pia kuwa wamelipiwa na Simba au na mfuko huo huo wa Serikali.
Hapo sioni ubaya wowote maana kuambatana na waandishi wa habari ni jambo muhimu sana katika safari hizi. Iwe ni serikali, taasisi zao za habari au Simba yoyote ambaye amechangia kuwapelewa waandishi wa habari nadhani sio jambo la kushangaza.
Nakumbuka vizuri uto wakati wanashiriki mashindano haya hatua hizi za mwisho, walikuwa wanabeba kila mwandishi wa habari. Inashangaza kwamba huku huku South Africa waliwaleta hao hao waandishi halafu leo wao wenyewe wanawaonea gere na kuwasambazia fitna.
Nimalizie kwa kusema Simba ilipewa ofa ya ndege toka hatua ya robo fainali ila mpaka leo haijaitumia. Kuna sababu mbalimbali ambazo zimechangia hilo kutofanyika mpaka sasa.
Nilisema juzi juzi Simba tuachane kubishana na hawa mashabiki wa vitimu vidogo vidogo ambao timu zao zimefeli msimu huu. Roho zinawauma kwa haya ambayo Simba inafanikisha na hawataacha kusambaza fitna na uzushi ili mashabiki wasahau mazuri ambayo timu yao inayapata.
Yamezuka maneno kutoka pande fulani zikisema Simba imepewa ndege halafu badala ya kubeba mashabiki wake wanaoipambania kila siku wamebeba watu wengine wasio na mchango wa kila siku katika timu.
Kwanza ninavyojua mimi, Simba haijapewa ndege bali imelipiwa nauli katika shirika la Air Tanzania ikiwa katika safari zake za kawaida kwenda South Africa. Siyo kila aliyekuwa kwenye ile ndege iliyoipeleka timu amelipiwa na Simba au serikali.
Kuhusu hao waandishi wa habari walioambatana na timu, wanaweza kuwa wamekwenda kwa pesa za taasisi zao au wanaweza pia kuwa wamelipiwa na Simba au na mfuko huo huo wa Serikali.
Hapo sioni ubaya wowote maana kuambatana na waandishi wa habari ni jambo muhimu sana katika safari hizi. Iwe ni serikali, taasisi zao za habari au Simba yoyote ambaye amechangia kuwapelewa waandishi wa habari nadhani sio jambo la kushangaza.
Nakumbuka vizuri uto wakati wanashiriki mashindano haya hatua hizi za mwisho, walikuwa wanabeba kila mwandishi wa habari. Inashangaza kwamba huku huku South Africa waliwaleta hao hao waandishi halafu leo wao wenyewe wanawaonea gere na kuwasambazia fitna.
Nimalizie kwa kusema Simba ilipewa ofa ya ndege toka hatua ya robo fainali ila mpaka leo haijaitumia. Kuna sababu mbalimbali ambazo zimechangia hilo kutofanyika mpaka sasa.
Nilisema juzi juzi Simba tuachane kubishana na hawa mashabiki wa vitimu vidogo vidogo ambao timu zao zimefeli msimu huu. Roho zinawauma kwa haya ambayo Simba inafanikisha na hawataacha kusambaza fitna na uzushi ili mashabiki wasahau mazuri ambayo timu yao inayapata.