Simanzi Mazishi ya Mchezaji wa Liverpool, Diogo Jota

Simanzi Mazishi ya Mchezaji wa Liverpool, Diogo Jota

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Wachezaji wa Liverpool wameungana na familia na marafiki katika mazishi ya mchezaji Diogo Jota na kaka yake André Silva, siku mbili baada ya kaka hao kufariki katika ajali ya barabarani nchini Uhispania

Ibada ya mazishi ilifanyika katika kanisa la Igreja Matriz katika mji wa Gondomar, Ureno, ambako Jota alikuwa na makazi

Kocha wa timu ya taifa ya Ureno, Roberto Martínez, pamoja na wachezaji kadhaa maarufu wa Ureno walihudhuria, wakiwemo Bernardo Silva, Rúben Dias wa Manchester City na Bruno Fernandes wa Manchester United

Wazazi wa marehemu walihudhuria ibada hiyo katika Kanisa la São Cosme, karibu na Porto, pamoja na Rais wa Ureno Marcelo Rebelo de Sousa, Waziri Mkuu Luís Montenegro na wakala wa Jota

Jota, mwenye umri wa miaka 28, na mdogo wake André Silva, 25, walikutwa wamefariki karibu na mji wa Zamora, kaskazini-magharibi mwa Uhispania, mapema Alhamisi baada ya gari lao aina ya Lamborghini kupata ajali na kuwaka moto usiku wa manane

Soma pia: Mshambuliaji wa Liverpool Diogo Jota, afariki dunia katika ajali ya gari

jota.png
 
May God grant peace to the wife and kids. Very sad indeed
 
Dota mwenye umri 28 na kaka yake mwenye umri miaka 25..... au wezetu hawana mdogomtu ila kaka

wapumzike kwa aman
 
Dota mwenye umri 28 na kaka yake mwenye umri miaka 25..... au wezetu hawana mdogomtu ila kaka

wapumzike kwa aman
Wabongo si unajua ni watu wa kucopy na ku paste! Kwenye lugha ya Malkia wamesema ".......his brother......." maana yake ni ndugu yake/mdogo wake! Na siyo kaka yake.
 
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni hazina ya taifa na kielelezo cha uongozi wa kisasa unaojengwa juu ya hekima, uvumilivu na maono ya mbali. Ni kiongozi ambaye anasimamia misingi ya haki, usawa na maendeleo ya watu wote bila ubaguzi. Ujasiri wake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom