Siloam church


Tatizo watu wanaabudu watu ndo shida ya madhehebu mengi ya Ukristo
 
tatizo wewe huelewi toka mwanzo wakati wa mitume imani ilikuwa moja ila kulikuwa na makusanyiko ktk nyumba tofauti na hii ndo inatakiwa siyo watu wako maelfu hawajuani kila mtaa eneo kulikuwa na kusanyiko mfano kanisa la Louse mamaake Timotheo na pia ukisoma vizuri kuikuwa na makusanyiko kikabila mf wayunani, kanis ala efeso, filipi, korintho hii ni kutokana na mila umbali na desturi lakini wakiamini kitu kimoja. Sasa hivi kuna Biblia ndio muongozo yoyote anayefuata Biblia na kuamini Yesu alimuokoa ni sahihi ila kuna izi imani za Yesu ni nabii, mara Yehova pekee, mara hakuna utatu ktk Mungu hapo kuna walakini.
 
Mimi ni mkristo, lakini nadhubutu kusema hawa ndugu zetu wamewekewa vitu kwenye bongo zao, maana si bure.. Ujuha, uozo na ujinga mtupu juu ya mambo wayaaminiayo, eti ELiya alimpiga Shetani na kumuua mwaka 2008, eti nabii wao alipaa, watuonyeshe video zake basi za kupaa si walijiandaa kwa hiyo siku?
 
Kwa nini..kuhani miaka 1000 inatumika hapa? Maana yake ni nini?

Tahadhari: Naomba nisitumwe kanisani nikaulize, anayejua anifafanulie tu ntajitahidi kuelewa.
aliwaambia ameua shetani ataish nao miaka 1000 kwanini wasiamini na kumuabudu chezea muujza wewe
 
Sijasema naendana na sloam,nimesema kwa nini napenda ukristo.

Napenda ukristo kwa kua unasema Yesu alikufa akafuta dhambi zetu zote,hakuna dhambi,chochote ukifanyacho hakuna dhambi tena duniani,tuko huru kufanya chochote maana hatutiwi hatiani.

ni kama sijakuelew au nimesoma vibaya...
chochote tufanyavyo hatuna hatia?! labda ufafanue...vp kuhusu wezi, wabakaji? wazinzi, wauaji, wachawi yaani ni wengu wote hao ruksa kufanya hayo sabb tu msamaha umetangazwa?!! ufafanuzi tafadhari.
 
Alifariki kwa tatizo gani au na yeye alipaa nn
 

Aiseeee!
 

Kama biblia ni moja naamini mafundisho yatakuwa ni yaleyale, taabu inakuja kwanini kuna kuwa na lundo la madhehebu na mafundisho tofauti katika kila dhehebu? Tatizo ni nini? Au mafundisho ya dini hayajitoshelezi?
samahani lakini nahitaji ufafanuzi tu!
 
ni kama sijakuelew au nimesoma vibaya...
chochote tufanyavyo hatuna hatia?! labda ufafanue...vp kuhusu wezi, wabakaji? wazinzi, wauaji, wachawi yaani ni wengu wote hao ruksa kufanya hayo sabb tu msamaha umetangazwa?!! ufafanuzi tafadhari.

chochote tukifanyacho yesu alishalipa garama yake,iwe dhambi au sio dhambi Yesu alishalipa gharama yake,hakuna kitu kinaitwa dhambi. Ukisema dhambi ipo ina maana unakataa kwamba Yesu hakufa msalabani na wala hakuja kwa ajili ya dhambi za wana damu

Yohana 15:3 iansema hakuna upendo mkuu namna hii,mtu kujitoa nafsi yake kwa ajili ya rafiki zake
Yesu alishajitoa kwa ajili yetu ili tuwe huru na dhambi. Mwana akiwaweka huru mnakua huru kweli kweli,tuko huru na kila kitu.

Nampenda Yesu.
 

Kazi kweli kweli, sasa wale wanaojiita kuwa wameokoka huwa wameokoka zambi zipi tena wakati Mungu (yesu) ameshabeba dhambi zao.
 
Hili kanisa linahusanishwa na Freemason na katika maelezo yao ni part of it
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…