Silaha ni kitega uchumi kikubwa cha Marekani

Silaha ni kitega uchumi kikubwa cha Marekani

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
373,309
Reaction score
864,897
Vita inayoendelea mashariki ya kati, Afika na kwingineko duniani ni mpango mahsusi wa marekani na washirika wake.

Kwa macho ya kawaida unaweza kufikiri kuwa Marekani ni mtu mzuri na mpenda amani lakini nyuma ya pazia hali ni tofauti mno, huku anachonganisha watu wapigane ili auze silaha, watu wake wapate ajira, uchumi ukue.

Mbele ya macho ya watu anakuwa mshauri na mpatanishi na mtoa misaada.

Vyovyote iwavyo vita haitakaa ikome duniani, labda wa mabwana wakubwa waache kutengeneza silaha.
 
Sasa wewe ulitaka wamarekani wakupende we na hayo mataifa ya mashariki ili wao kama waamerica wapate faida gani? Kila mtu au taifa hufanya jambo kwa ustawi na maendeleo ya familia au taifa lake.

Kama ndo njia inayowaletea maendeleo hawana budi kufanya hivyo.
Nawe thubutu ukiweza poa, tupo tukaokupigia makofi kama shujaa.
Hivi mtu anayepeleka umbea kwa wanandoa mwisho ndoa ikasambaratika.... tatizo ni mpeleka umbea au wanandoa wenyewe?
Usifikiri kelele zenu wanadamu wa upande wa pili ndo zitawafanya waamerica waache kugombanisha mataifa ili wao wanufaike.

Popote penye udhaifu waweza patumia kama fursa. Wajinga ni hao wanaoshkiana mapanga na bunduki kuuana, na kwa tz na hz siasa zetu za maji taka nahisi tunaelekea huko muda si mrefu...
 
Back
Top Bottom