Sikubaliani na kuvunja baraza la mawaziri!!

tikatika

JF-Expert Member
May 6, 2011
2,330
4,115
Ndugu wana jamvi hebu tutafakari vizuri,
Je kwa ubadhilifu huu kuvunja baraza ni njia sahihi iliyotakiwa kufanywa na mtu aliyechukizwa na wabadhilifu?
. No, binafsi naona kufanya hivi ni kufukia uovu!
kwani haitajulikana nani kaadhibiwa Bali ni kubadilisha watendaji, kama serikali ya ccm ilichukizwa ilitakiwa wafukuzwe watu wote tujue wamefukuzwa kwa makosa haya na kwa kufanya hivyo nikukubaliana na maon ya bunge na wananchi walio weng. Lakn kilicho fanyika ni usanii Kwan hakuna hatua itakayochukliwa dhid Yao na hawatakuwa na aibu Kwan hawajafukuzwa ILA wamebadilishiwa kaz! akina karamag Wako wap?
hapa wamefunika kombe mwanaharam apite!
Sisi wananchi tuwachukulie hatua hata kama wezi wenzao wamewachia aibu!
 

hivi kufukuzwa mpaka kwa mijeledi? halafu wengi wa wanaotakiwa kutolewa si kwamba wamekula au kufanya ubadhirifu wao buinafsi ila wanachukua political responsibility.
 

Hawa magamba wanadhani watatukosha kwa kubadili watu? La hasha! Hoja ya msingi ni sheria kuchukua mkondo wake. Hao mawaziri wafikishwe mahakamani kwa wizi walioufanya, na km ni dhamana wakati kesi ikiendelea basi thamani yake iwe ni zaidi ya wizi walioufanya. LAKINI PIA JAMANI HAWA WATU TUKIWAONA KITAA INABIDI WAPIGWE MAWE NA KUCHOMWA MOTO KM KAWAIDA YA WEZI, TENA HAWA WANAHITAJI KIPIGO MBADALA COZ WAMEKWIBA PESA MINGI AISEE.,

Nadhani ni muda mwafaka wa jeshi la polisi kutangaza kuwatafuta hawa wezi na kutoa zawadi kwa watakaofanikisha kukamatwa kwao!!
 
Lengo hasa ni kuzima discusion & kupoteza ili upepo upite. Kama kawaida yao hawataenda mbali zaidi
 
Atakuwa na sifa ya uongozi mbovu awamu yake kwa kubeba watu wanaompaka uchafu.
 
Mkuu mbona umeingia jamvini bila hodi?
 

Dah! Ndugu, hapo tutapigwa blaa blaa kimeenda kimerudi nyingi, hadi kimya! Tatizo tunaiamin sana siasa, eti utawala wa sheria nani kasema....serikali ikishafuga wezi wa rasilimali basi imekiuka katiba, sasa iweje sisi tuing'ang'ania?
"When forces of oppression come to maintain themselves in power against the established law, peace is considered arleady broken" Che Guevara.
Mungu wetu anaita!
 
Hivi watu nyie, nani aliyesema kuwa Baraza la Mawaziri linavunjwa? Binafsi nilisikia jana ikitangazwa kuwa Baraza la Mawaziri "litasukwa upya". Kulisuka upya haina maana ya kulivunja, wanaweza hamishwa Wizara baadhi ya Mawaziri na mchezo ukaisha. Hii ndio Bongo, mnategwa kidogo mnaingia wazima wazima. Subirini mtaona.
 
hivi kufukuzwa mpaka kwa mijeledi? halafu wengi wa wanaotakiwa kutolewa si kwamba wamekula au kufanya ubadhirifu wao buinafsi ila wanachukua political responsibility.
Kufukuzwa kuna maana sana kwani houni mh.Lowasa anaitwa mstaafu na posho anapewa?. na kwa hawa itakuwa hivyo hivyo kookolikoo. Au na wewe hujuii tena alama za nyakati unawika tu hata saa nane usiku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…