Siku ya ufahamu kuhusu usonji/tawahudi duniani

Siku ya ufahamu kuhusu usonji/tawahudi duniani

Mema Tanzania

Member
Joined
Feb 23, 2020
Posts
66
Reaction score
65
Ikiwa leo ni Siku ya ufahamu kuhusu usonji duniani tutizame kwa uchache kuhusu suala hili

Autism.png


Usonji au tawahudi kwa kiingereza autism ni tatizo la nafsi na hisia linalowatokea watu angali watoto na kuathiri uwezo wa kuwasiliana na wengine. Wenye tatizo hawaonekani watu wa kawaida. Muda mwingine hawapendi kuangalia wengine pale wanapozungumza au kushirikiana na watu wengine katika mambo kadhaa.

Pia hawako vizuri kimawasiliano muda mwingine hawawezi kuongea au kuzungumza na watu wengine. Mtu mwenye tatizo hili mara nyingi hurudia matendo kadhaa na anaweza kuhofia vitu katika mazingira yake yasiyoeleweka, hujijibu wenyewe, wanaweza wakawa na shauku na kitu ambacho mtu mwingine hafikirii kina umuhimu.

Tawahudi ni ugonjwa wa ukuaji wa neva unaojumuisha kudhoofishwa kwa uwezo wa mwingiliano wa kijamii na mawasiliano, na kwa tabia finyu na ya kujirudia. Dalili hizo huanza kabla ya mtoto kutimiza miaka mitatu. Ugonjwa wa akili kwa watoto huathiri uchakataji wa habari katika ubongo kwa kubadili seli za neva na sinepsi zake zinavyounganika na kujipanga.

Usonji ni moja ya matatizo matatu yanayotambulika kama ugonjwa wa akili wa watoto (ASDs), mengine yakiwa maradhi ya Aspaja, ambayo hayacheleweshi ukuaji wa kiutambuzi na lugha na tatizo la ukuaji Ulioenea (PDD-NOS) ambao hutambuliwa kikamilifu wakati vigezo vyote au Aspaja havijatimizwa.

Autism4.png

#WorldAutismAwarenessDay
 
Habari wakuu!
naomba kufahamishwa juu ya ugonjwa huu unaoitwa autisim huu ugonjwa nahisi anao mtoto wa kaka yangu nasema hivo kwa sababu kuu zifuatazo!
1. huyu mtoto amekuwa ni Kama vile anatatizo kwenye ubongo,
2.ni mtu wa kujitenga Sana na Ana hisia Kali Sana
3.pia mpaka Sasa anaongea kwa shida Sana
QNS; je watu wenye autism huwa na tabia tajwa hapo juu wakuu?.

naomba kuwasilisha!
 
Back
Top Bottom