Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Inaweza kutokea kama ajali tu, hujawahi kumwambia kuhusu mwanaume uliyeachana naye miezi kadhaa iliyopita baada ya kudumu naye kwa muda mfupi sana katika mapenzi yenu kutokana na kukumbwa na vurugu za mara kwa mara Kwa kifupi huyo mpenzi alikuwa ni mnyanyasaji sana. Hukuwahi kumzungumzia mpenzi wako wa zamani kwa mpenzi mpya kwa sababu hamkuwahi kuzungumzia jambo hilo.
Lakini kibaya zaidi watu hao wanafahamiana na baada ya kukutana kwao katika mghahawa huo mliokwenda wanasalimiana kwa bashasha na kuzungumza kidogo kuhusu biashara zao wanazofanya pamoja……………. Haiishii hapo huyu mpenzi mpya anatumia nafasi hiyo kukutambulisha kwa huyu mpenzi wako wa zamani kwamba wewe ndiye mtarajiwa wake kama mambo yatakwenda vizuri……………
Hebu niambie mwanamke, unakutana na shiranga hili unafanyaje……………………..?