Siku ya Mazoezi; Arusha Yazizima, RC Gambo anena

kunena

JF-Expert Member
Nov 29, 2016
506
719
Leo ni siku ya mazoezi kitaifa kama ilivyoelekezwa na Mh. Samia Saluhu makamu wa rais....

Mkoani Arusha zoezi hili limezinduliwa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mh Gambo.

Zoezi lilianza saa kumi na mbili asubuhi katika viwanja vya mkuu wa wilaya wa Arusha na kuhitimishwa katika uwanja wa sheikh Amri Abeid Kaluta.

Zoezi hili limefana sana na kupata mwitikio mkubwa wa makundi mbalimbali.Mh Gambo alipata fursa ya kuzungumzia vita ya madawa ya kulevya ambapo alisema kwa mkoa wa Arusha zoezi hili linaendelea kimyakimya ambapo watuhumiwa wanakamatwa na kuhojiwa kabla ya kuja kutangazwa baada ya kujiridhisha na tuhuma zake.

Vile vile mkuu wa mkoa aliwaasa wananchi wasitajane kwa chuki na husuda kwani ni jambo baya na linaleta mvurugano katika jamii...."mutaje watu wanaohusika kweli na sio mtu mmegombana kwenye mambo yenu huko unaamua kumkomoa,RPC anaendelea kupokea majina na task force inaendelea kufanya uchunguzi kabla ya kuja kwenye mediaup
alinukuliwa kiongozi huyo wa juu ngazi ya mkoa.

Mazoezi haya ni kwaajili ya kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi ili kupambana na magonjwa hatari kama kisukari na mengineyo yasiyoambukiza.

7c543122c89b6ab47356698dea3c11f6.jpg

739ed9395b5f59d654a55c27669d8328.jpg

b220c11e92d05d188b2d84b7732b5652.jpg

7c9236ed2b82bfdd167dc770997053f2.jpg

Mh Gambo akimalizia push up ya mia moja...
770eaa25c9869d7625e383bee3c8247b.jpg


3bf42a71fdd44e457df2317fde85578d.jpg

Mkuu wa mkoa wa Arusha akizungumza na walemavu waliokuja mazoezini

e24b29de1ee7c19cd77eaed1fe7cd6f0.jpg

RAS mkoa wa Arusha na RPC Charles Mkumbo wakipiga push up

6a7457c4955d3369a9c00b8e3d3468fc.jpg

Taasisi za umma zilishinda mchezo wa kuvuta kamba.
 
Mbona huyu na RC mwingine wa mkoa maarafu kwa sembe wana wowoo kubwa kubwa?

Hebu muangalieni vizuri. Alafu mazoezi gani hayo ya kubinua makalio juu mbele ya Wanaume?
Hahahaha! Hata Mimi nashangaa sana. Hivi huyu ndio yule alielalamika mama mbunge kumuita shosti ama
 
Hahahaha! Hata Mimi nashangaa sana. Hivi huyu ndio yule alielalamika mama mbunge kumuita shosti ama
Mkuu katika falfasa ya mapambano mtu anapoamua kutumia matusi kwa kweli ni dalili ya woga, kushindwa na kuishiwa hoja.....kama hata suala dogo hivi la mazoezi kwenu ni mtaji wa kufanyia siasa kwakweli nina mashaka sana na aina ya watu mlioko huko.....tuvumiliane tu jamani mpaka 2020.
 
>>> HUYU mkuu Hajaanza VITA kama ya MADEREVA ???? >>
Ukimsoma mleta mada anasema ila wanatumia utaratibu wa kupokea majina toka kwa wananchi ambapo wanayawasilisha kwa RPC ama mkuu wa wilaya then wana task force inayofanya uchunguzi wa kina kisha wanaonekana wana mienendo inayotia mashaka wanaitwa wanahojiwa.....ushahidi ukikamilika watapandishwa mahakamani na orodha ya watuhumiwa wote itawekwa kwenye media.....
 

Hapa akizungumzia ishu ya madawa ya kulevya mkoani Arusha
 
Back
Top Bottom