Siku ya kwanza jijini Dar

katawa

JF-Expert Member
Jan 29, 2010
742
1,656
Ilikuwa ni tar 17-12 1988 nilpopata taarifa kuwa siku tatu baadaye nitasafiri kuelekea 'dizim' Dar es salaam.Maandalizi ya nguvu yakaanza ikiwa ni pamoja na kuazima nguo bila kusahau chupi.Rafiki yangu mpendwa Asuvisye akaniazima chupi aina ya vipi.
Siku ikawadia mimi na kiongozi wangu wa msafara tukapanda basi la Zainabu.Njian nilikuwa kero kwa abiria kwa kuwa nilishangaa mambo mengi na nilikuwa nauliza maswali bila kikomo ukizingatia ni mara ya kwanza kupanda basi ktk umri huo wa miaka kumi na nne.

Siku inayofuata tukafika dar mchana.Tulipofika magomen kiongozi wangu akanitwisha kiroba cha mchele yeye mbele mimi nyuma,akajitokeza muungwana kunisaidia nikampa kiroba mwenyeji wangu akiwa mbele yangu.Alipofika nyumbani kugeuka anaona sina kipeto aliponiuliza kiko wapi nageuka nyuma sikumuona muungwana aliyenipokea.

siku ya pili ilikuwa ijumaa ktk tembea yangu nikapita eneo ambalo watu wengi waliovaa nguo nyeupe na kofia walikuwa wanaingia na kutoka ilikuwa majira ya jioni.nikapata shauku ya kujua kuna nini huko ndani,nikaingia nikiwa nimevaa raba aina ya DH.Kumbe ni msikiti nimeingia na viatu na watu walikuwa kwenye swala kilichotokea unaweza ukakihisi.

Siku nyingine nikapelekwa feri na watoto wenzangu.Nilipoulizwa iwapo najua kuogelea nikakubali ili nisionekane wakuja, nikajitosa kwenye maji kwa nguvu.Washukuriwe wavuvi waliokuwepo eneo lile.

Ndani ya muda mfupi Dar niliyokuwa naiota na kuitamani ikanikifu nikamlazimisha mwenyeji wangu anirudishe kwetu Uyole Mbeya ambako utulivu ni kama Mbinguni.

Je mwanajamii mwenzangu hebu nijulishe wewe ilikuwaje siku ya kwanza jijini DAR?
 
Ilikuwa ni tar 17-12 1988 nilpopata taarifa kuwa siku tatu baadaye nitasafiri kuelekea 'dizim' Dar es salaam.Maandalizi ya nguvu yakaanza ikiwa ni pamoja na kuazima nguo bila kusahau chupi.Rafiki yangu mpendwa Asuvisye akaniazima chupi aina ya vipi.
Siku ikawadia mimi na kiongozi wangu wa msafara tukapanda basi la Zainabu.Njian nilikuwa kero kwa abiria kwa kuwa nilishangaa mambo mengi na nilikuwa nauliza maswali bila kikomo ukizingatia ni mara ya kwanza kupanda basi ktk umri huo wa miaka kumi na nne.

Siku inayofuata tukafika dar mchana.Tulipofika magomen kiongozi wangu akanitwisha kiroba cha mchele yeye mbele mimi nyuma,akajitokeza muungwana kunisaidia nikampa kiroba mwenyeji wangu akiwa mbele yangu.Alipofika nyumbani kugeuka anaona sina kipeto aliponiuliza kiko wapi nageuka nyuma sikumuona muungwana aliyenipokea.

siku ya pili ilikuwa ijumaa ktk tembea yangu nikapita eneo ambalo watu wengi waliovaa nguo nyeupe na kofia walikuwa wanaingia na kutoka ilikuwa majira ya jioni.nikapata shauku ya kujua kuna nini huko ndani,nikaingia nikiwa nimevaa raba aina ya DH.Kumbe ni msikiti nimeingia na viatu na watu walikuwa kwenye swala kilichotokea unaweza ukakihisi.

Siku nyingine nikapelekwa feri na watoto wenzangu.Nilipoulizwa iwapo najua kuogelea nikakubali ili nisionekane wakuja, nikajitosa kwenye maji kwa nguvu.Washukuriwe wavuvi waliokuwepo eneo lile.

Ndani ya muda mfupi Dar niliyokuwa naiota na kuitamani ikanikifu nikamlazimisha mwenyeji wangu anirudishe kwetu Uyole Mbeya ambako utulivu ni kama Mbinguni.

Je mwanajamii mwenzangu hebu nijulishe wewe ilikuwaje siku ya kwanza jijini DAR?
Msikitini uliingia na viatu raba DH
 
Ndo mnaotusumbuaga nyie na maustaarabu yenu ya kujifunzia mjini,,ningekuwa makonda ningeweka utaratibu maalum kuingia mjini
 
Mm mara ya kwanza nilipanda bus la kwenda Dar wakati huo tunaita Kooch, nilianza kuandika majina ya Maeneo yote na vituo vyote tulivyopitia kuanzia mianzini, ilboru, sanawari, mountmeru, philips, kimandolu, ngulelo, kwa mrefu, nduruma, Tengeru, USA, maji ya chai, king'ori , Kia, Boma, sadala, machame, kibosho, changmai, Moshi stand......nimefanya hivyo mpk Dar, huku nikiuliza bila aibu.

Begi langu ilikua ni malboro mbili ya rangi ya blue na nyeusi...jamani tumetoka mbali, ni kwa neema tu tumefika hapa tulipo
 
  • Thanks
Reactions: Ok9
Mm mara ya kwanza nilipanda bus la kwenda Dar wakati huo tunaita Kooch, nilianza kuandika majina ya Maeneo yote na vituo vyote tulivyopitia kuanzia mianzini, ilboru, sanawari, mountmeru, philips, kimandolu, ngulelo, kwa mrefu, nduruma, Tengeru, USA, maji ya chai, king'ori , Kia, Boma, sadala, machame, kibosho, changmai, Moshi stand......nimefanya hivyo mpk Dar, huku nikiuliza bila aibu.

Begi langu ilikua ni malboro mbili ya rangi ya blue na nyeusi...jamani tumetoka mbali, ni kwa neema tu tumefika hapa tulipo
Baada ya Maji ya Chai Kikatiti Mkuu Vepe Naona Vituo Vingi sana Umeviacha...Vikiwemo Kilala, Makumira na Danish Umeruka pia Machame nadhani ndio Machine Tools.

Kiboroloni, and then Njia Panda himo, Mwanga,Same,Hedaru,Mnazi,Mazinde,Mombo,Korogwe,Segera,Handeni,Kwedukwazu,Mkata,Wami,Msata,Chalinze,Ruvu,Kongowe,Maili moja Kibaha,Mbezi,Kimara,Ubungo,Stand ya Mkoa. Zamani ilikuwa Manzese,Argentina,Magomeni Kagera,Magomeni Mwembechai,Magomeni Usalama,Magomeni Mapipa,Fire and then Stand ya Kisutu.
 
Baada ya Maji ya Chai Kikatiti Mkuu Vepe Naona Vituo Vingi sana Umeviacha...Vikiwemo Kilala, Makumira na Danish Umeruka pia Machame nadhani ndio Machine Tools.

Kiboroloni, and then Njia Panda himo, Mwanga,Same,Hedaru,Mnazi,Mazinde,Mombo,Korogwe,Segera,Handeni,Kwedukwazu,Mkata,Wami,Msata,Chalinze,Ruvu,Kongowe,Maili moja Kibaha,Mbezi,Kimara,Ubungo,Stand ya Mkoa. Zamani ilikuwa Manzese,Argentina,Magomeni Kagera,Magomeni Mwembechai,Magomeni Usalama,Magomeni Mapipa,Fire and then Stand ya Kisutu.
Daaah... Vituo vyote unavyo...!? Shikamoo Utingo..!!
 
Daaah... Vituo vyote unavyo...!? Shikamoo Utingo..!!
Ngoja niitikie tu Shikamoo ya kwanza JF Siwezi ilazia damu Marahaba...Abiria ilikuwa Ukitaka Kupanda Bus unasema tu unataka lipi unapata tiketi... Ngorika,Dar Express,Masama Safaris,Fresh Ya Shamba,Njuweni,Sawaya,Mapande,Air Msae ,Yarabi Salama,Imamu Express, Shengena ,Relwe, Kamata,Kindokyakosembe,Kindokyakombe,Zafanana,Kimotco,Islam,Hood, Air Chalinze,Price Osaka,Real No Challenger,Simba Mtoto,Metro,Born City Midfielder ,Bazuu, Moro Kuna Sharuks na Aboud zipo. Hata Treni ukipenda ilikuwepo Dar Moshi.
 
Back
Top Bottom