Mkuu
leroy kuna hoja ya msingi hapa.
Vijana huwa wana mategemeo makubwa. Kumbukumbu zinaonyesha kwamba vijana walikuwa wakishangilia sana wakati Rais JK anaingia madarakani. Walimpigia kura wakidhani sasa ni wakati wa vijana kutesa, waliona vijiwe sasa kwaheri wanaenda kupata wote kazi njema zinazolipa huko maofisini.
JK alianza kwa kutembelea wizara na kuna muda alikuwa anatembea toka wizara moja kwenda nyingine akiwa analakiwa kwa nderemo na vifijo vya vijana waliokuwa wakijipanga kumuona mkombozi wao. Baada ya kuona matokeo si sawa na matarajio yao basi wamejikita CDM wakitegemea hali bora toka huko.
Hakika CDM ina vijana kila kona na wote wanaitimbulia macho CDM iingie ikulu iwaokoe na hali duni. Hivyo CDM kama hawatafikia matarajio ya vijana basi vijana hao hao ndio watawageuka tena na kutafuta mbadala. CDM inabidi ijipange kutekeleza matarajio ya vijana