fakalava
JF-Expert Member
- Jul 16, 2015
- 4,459
- 6,027
Hii kauli imenishutua, ni kauli kutoka kwa rafiki yangu ninayemfahamu kwa muda mrefu. Ndoa yao ina miaka 5 sasa na wamebahatika kupata mtoto mmoja wa kike, kwa haraka haraka unaweza kuiona ndoa yao kama ni ndoa imara na yenye upendo mkubwa na kutamani kujifunza kutoka kwao.
Majuzi nilikutana na huyu rafiki yangu tulikuwa na maongezi ya kikazi, katika maongezi yetu tukawa tumeingiza mambo ya familia, ndipo nilishutushwa na kauli ya rafiki yangu "Siku hizi simwambii mke wangu asante kwa chakula"
Nikamuuliza, kwanini? "Tangu apate hii kazi aliyonayo sasa yapata miaka miwili sili chakula kilichopikwa kwa mikono yake angalau mara moja moja, kwa siku chache za mwanzoni alijitahidi lakini haikudumu kwa muda mrefu akaacha kabisa binti wa nyumbani akawa ndiyo muhusika kwa 100%.
Imenichukua muda mrefu kila nimalizapo kula chakula hasa umwambia mke wangu asante kwa chakula, kilikuwa ni kitamu.
Kwa sasa nimegundua kuwa ninachokifanya ni unafiki tu wa kumfurahisha mke wangu, huku nikiwa na manung'uniko moyoni. Kwa sasa nikimaliza kula nasema asante aliyepika chakula, kilikuwa kitamu sana, naona hii kauli imemshutua na kumchanganya kidogo".
Nikamuuliza kwanini anatumia njia hii badala ya kukaa naye wakaliongelea hili tatizo, akasema "Nimekwisha ongea naye mara nyingi ila amekuwa na sababu nyingi mara kuchoka, mara ubize wa kazi, sababu nyingi tu. Natamani angalau mara moja moja nile chakula chakula kilichopikwa kwa mikono ya mke wangu".
Wanawake jitahidi waume zenu wale chakula kilichopikwa kwa mikono yenu angalau mara moja moja.
Majuzi nilikutana na huyu rafiki yangu tulikuwa na maongezi ya kikazi, katika maongezi yetu tukawa tumeingiza mambo ya familia, ndipo nilishutushwa na kauli ya rafiki yangu "Siku hizi simwambii mke wangu asante kwa chakula"
Nikamuuliza, kwanini? "Tangu apate hii kazi aliyonayo sasa yapata miaka miwili sili chakula kilichopikwa kwa mikono yake angalau mara moja moja, kwa siku chache za mwanzoni alijitahidi lakini haikudumu kwa muda mrefu akaacha kabisa binti wa nyumbani akawa ndiyo muhusika kwa 100%.
Imenichukua muda mrefu kila nimalizapo kula chakula hasa umwambia mke wangu asante kwa chakula, kilikuwa ni kitamu.
Kwa sasa nimegundua kuwa ninachokifanya ni unafiki tu wa kumfurahisha mke wangu, huku nikiwa na manung'uniko moyoni. Kwa sasa nikimaliza kula nasema asante aliyepika chakula, kilikuwa kitamu sana, naona hii kauli imemshutua na kumchanganya kidogo".
Nikamuuliza kwanini anatumia njia hii badala ya kukaa naye wakaliongelea hili tatizo, akasema "Nimekwisha ongea naye mara nyingi ila amekuwa na sababu nyingi mara kuchoka, mara ubize wa kazi, sababu nyingi tu. Natamani angalau mara moja moja nile chakula chakula kilichopikwa kwa mikono ya mke wangu".
Wanawake jitahidi waume zenu wale chakula kilichopikwa kwa mikono yenu angalau mara moja moja.