Wrevta
JF-Expert Member
- Jan 18, 2023
- 1,440
- 1,720
Nawasalimu!
Kwa muda mfupi wa hapa Jamii Forums nimestaajabu sana baada ya kuona wanaume wakiandika maneno yasiyo na utu wala 'sympathy' kwenye nyuzi za wanaume wanaolalamika kunyanyaswa na wake zao. Maneno yafuatayo nimeya note kwa baadhi ya ID's(sitozitaja) ambayo yana walakini usio wa kawaida?
1. "Wanawake nawainulia mikono juu"
Yaani mtu ameleta uzi wa huzuni kuna mwanaume anaandika komenti hiyo hapo juu na kuweka emoj za kucheka na kufurahi na kutoa utukufu kwa mwanamke.
2. "Hawa viumbe ni hatari"
Mtu anahuzunika ila kuna mpuuzi anaandika hayo maneno tena ni mwanaume. Na emoj za kucheka anaziweka.
3. "Wanawake shikamooni"
Hivi mwanaume na akili zako kwenye uzi wa mwenzio unaandika huo upuuzi ukiwa na lengo gani? Mwenzio anaumia wewe unacheka.
Hizo na nyinginezo nyingi zinafanya nijiulize sana, kwa nini wanafurahia wanaume wakiteswa na wanawake na wanawake wakiteswa na wanaume wanatoa komenti za hasira kwa wanaume?
Nimeona post nyingi mwanaume akimkosea mwanamke wengi humu wanamjia juu mwanaume wakimshutumu kuwa ni muovu bila hata kuuliza chanzo.
Wengine huenda mbali kwa kumtusi kabisa matusi ya nguoni.
Na akileta mwanamke uzi wa kunyanyaswa na mwanaume, wanaume wengi pasipo hata kuuliza na kutaka kujua yalianzia wapi, humshambulia mwanaume na kumtukana matusi ya nguoni.
Sasa niwaulize nyie watoto wa kiume mnaofurahia kuona wanaume wenzenu wakinyanyaswa na wanawake, mnapata faida gani, mmetumwa na nani na kwa maslahi ya nani?
Kwa muda mfupi wa hapa Jamii Forums nimestaajabu sana baada ya kuona wanaume wakiandika maneno yasiyo na utu wala 'sympathy' kwenye nyuzi za wanaume wanaolalamika kunyanyaswa na wake zao. Maneno yafuatayo nimeya note kwa baadhi ya ID's(sitozitaja) ambayo yana walakini usio wa kawaida?
1. "Wanawake nawainulia mikono juu"
Yaani mtu ameleta uzi wa huzuni kuna mwanaume anaandika komenti hiyo hapo juu na kuweka emoj za kucheka na kufurahi na kutoa utukufu kwa mwanamke.
2. "Hawa viumbe ni hatari"
Mtu anahuzunika ila kuna mpuuzi anaandika hayo maneno tena ni mwanaume. Na emoj za kucheka anaziweka.
3. "Wanawake shikamooni"
Hivi mwanaume na akili zako kwenye uzi wa mwenzio unaandika huo upuuzi ukiwa na lengo gani? Mwenzio anaumia wewe unacheka.
Hizo na nyinginezo nyingi zinafanya nijiulize sana, kwa nini wanafurahia wanaume wakiteswa na wanawake na wanawake wakiteswa na wanaume wanatoa komenti za hasira kwa wanaume?
Nimeona post nyingi mwanaume akimkosea mwanamke wengi humu wanamjia juu mwanaume wakimshutumu kuwa ni muovu bila hata kuuliza chanzo.
Wengine huenda mbali kwa kumtusi kabisa matusi ya nguoni.
Na akileta mwanamke uzi wa kunyanyaswa na mwanaume, wanaume wengi pasipo hata kuuliza na kutaka kujua yalianzia wapi, humshambulia mwanaume na kumtukana matusi ya nguoni.
Sasa niwaulize nyie watoto wa kiume mnaofurahia kuona wanaume wenzenu wakinyanyaswa na wanawake, mnapata faida gani, mmetumwa na nani na kwa maslahi ya nani?