Siku hizi haya yapo kweli???

Jiwe Linaloishi

JF-Expert Member
May 24, 2008
3,736
2,137
SIJUI KAMA SIKU HIZI ZIPO HIZI
1. Kupakwa GV kwenye kidonda
2. Kung'olewa jino kwa uzi
3. Ubwabwa kupikwa j2 tu
4. Kidonda kuwekwa unga wa 'rangi mbili'
5. Kupamba kadi sebuleni
6. Ukumbi wa sherehe kupambwa kwa toilet paper
7. Kunyolewa na mkasi
8. Kufunga pesa kwenye leso au pindo la kanga
9. Kwenda kuangalia sinema za Ukimwi na Lishe sokoni
10. Ku rewind kanda kwa peni
11. Ndala kuchemshwa ili zisiishe
12. Kucheza umeshikilia kaptula sababu mpira umekatika
13. Kuchonga penseli na meno
14. Kukata ndala, ati ni kifutio
15. Kunyolewa msalaba shuleni kisa nywele ndefu
16.Kwenda shuleni na tofali na kidumu cha maji

17.Kwenda na Kigae cha moto(hii ni kwa Iringa pekee)

18. kununuliwa nguo au viatu vikubwa kwa size ili ukuwe navyo LOL

19.kushika sikio kappa kipio cha ukubwa ready kuanza shule.

Ongezea unayoyakumbuka
 
kukusanyika jioni na kusimuliwa hadithi na wakubwa hasa bibi au babu
 
Back
Top Bottom