Siku ambayo paka walinirukia na kupigana usiku wa manane msibani,

craq

JF-Expert Member
Mar 22, 2017
859
1,864
Kuna tukio ambalo liliwahi kunitokea nimelikumbuka ghafla

Kuna mahala palitokea msiba na nilienda kuhudhuria msiba huo kama mnavyofahamu tulilala pale msibani ili kesho yake tuzike na kufuatilia masuala mengine.Ilipofika usiku watu walilala kwenye majamvi na ukizingatia kulikuwa na turabai 2 zilifungwa..pembeni sehemu ya msiba kuna ofisi za mafundi seremala hivyo kuna kochi la siti ya mtu mmoja lilikuwa wazi nikaliwahi na kujimwaga huku nikijikunyata nikiegemea sponchi zenye kunesanesa huku nikiwaacha wenzangu wakilalia majamvi chini sehemu ngumu hakika nilikuwa na furaha sababu usingizi ambao naupata ulikuwa wa raha mustarehe tofauti ya wale waliokuwa wanalalia majamvi siku zote mtu anayelala masaki na anayelala tandale kwa tumbo au anayelala njiro na anayelala ngarenaro usingizi wao katu haufanani..

Nikiwa nipo kwenye njozi matata nikibembelezwa na kaupepo na nikinesanesa kwenye masponchi mara paap kuna paka walikuwa wanagombana huku wakikimbizana kwa spidi ya ajabu sasa wakatoka spidi huko waliko kituo cha kwanza wakaliparamia ile sofa niliyokuwa nimelala break yao ilikuwa kifuani kwangu huku wakipigana na kutoa milio ya ajabu ajabu ase nilikurupuka na kupiga yowe na kuruka mithili ya spiderman kumbe bwana kuna majamaa watatu walikuwa hawajalala wanapiga stori tukio lile walilishudia wacha wacheke na kuja kuwatimua wale paka..

Usiombe ulale fofofo halafu mapaka wakimbizane na waruke kifuani kwako tena wapigane hapo huku wanalia milio ya ajabu kwa namna nilivyokurupuka daah kila nikikumbuka nacheka sana
 
Kuna tukio ambalo liliwahi kunitokea nimelikumbuka ghafla

Kuna mahala palitokea msiba na nilienda kuhudhuria msiba huo kama mnavyofahamu tulilala pale msibani ili kesho yake tuzike na kufuatilia masuala mengine.Ilipofika usiku watu walilala kwenye majamvi na ukizingatia kulikuwa na turabai 2 zilifungwa..pembeni sehemu ya msiba kuna ofisi za mafundi seremala hivyo kuna kochi la siti ya mtu mmoja lilikuwa wazi nikaliwahi na kujimwaga huku nikijikunyata nikiegemea sponchi zenye kunesanesa huku nikiwaacha wenzangu wakilalia majamvi chini sehemu ngumu hakika nilikuwa na furaha sababu usingizi ambao naupata ulikuwa wa raha mustarehe tofauti ya wale waliokuwa wanalalia majamvi siku zote mtu anayelala masaki na anayelala tandale kwa tumbo au anayelala njiro na anayelala ngarenaro usingizi wao katu haufanani..

Nikiwa nipo kwenye njozi matata nikibembelezwa na kaupepo na nikinesanesa kwenye masponchi mara paap kuna paka walikuwa wanagombana huku wakikimbizana kwa spidi ya ajabu sasa wakatoka spidi huko waliko kituo cha kwanza wakaliparamia ile sofa niliyokuwa nimelala break yao ilikuwa kifuani kwangu huku wakipigana na kutoa milio ya ajabu ajabu ase nilikurupuka na kupiga yowe na kuruka mithili ya spiderman kumbe bwana kuna majamaa watatu walikuwa hawajalala wanapiga stori tukio lile walilishudia wacha wacheke na kuja kuwatimua wale paka..

Usiombe ulale fofofo halafu mapaka wakimbizane na waruke kifuani kwako tena wapigane hapo huku wanalia milio ya ajabu kwa namna nilivyokurupuka daah kila nikikumbuka nacheka sana
₭介흣立
 
IMG_1271.JPG
Paka wana protect! Kulikuwa kuna jambo baya likupate lakini wakaliondoa! Paka wanaondoa mapepo wachafu! That's a good omen!
 
BADO NAJIULIZA HADITHI HII INATUFUNDISHA TUSIWAHI MAKOCHI MSIBANI AU TUSIOGOPE PAKA??
 
Umenichekesha hasa pale uliposema λκιθξηφδψβδδρθοπνα Hatari sana....Pole sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom