Siku 100 za Rais John Pombe Magufuli

Siku 100 za Rais John Pombe Magufuli

Tutajua kama ni nguvu ya soda au la baada ya siku 100 kukaa pale magogoni.
 
Hakuna atakachofanya zaidi ya usanii wa ziara za kushtukiza..cha ajabu anaogopa kwenda bandarini kunakonuka rushwa na ukwepaji kodi anakimbilia muhimbili kufukuza manesi
 
------ wewe...mpeleke baba yako huko bandarini, kwani umekuwa boss wake mpaka umpangie cha kufanya?acha utani na mkuu wa nchi..umejaa kiburi na fedhuri mpumbavu sana wewe
 
Hakuna atakachofanya zaidi ya usanii wa ziara za kushtukiza..cha ajabu anaogopa kwenda bandarini kunakonuka rushwa na ukwepaji kodi anakimbilia muhimbili kufukuza manesi

Usiwe na haraka we tulia tuu mziki wake ni mnene na mtanyooooka tu ninyi mafisadi
 
Hakuna atakachofanya zaidi ya usanii wa ziara za kushtukiza..cha ajabu anaogopa kwenda bandarini kunakonuka rushwa na ukwepaji kodi anakimbilia muhimbili kufukuza manesi

hata mm nasubir kwa hamu sana atakavyo umiliki ule mfupa wa bandarini panaturudisha nyuma sana pale na hapajawa na ufumbuz wa kudumu
 
Siku 26 tangu kutangazwa kuwa rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. JOHN POMBE MAGUFULI, amefanya yafuatayo ikiwa ni mipango yake ya kubana matumizi ya serikali , kusimamia utendajikazi wa idara na taasisi za serikali, kuhakikisha huduma za kijamii zinaboreka n.k:
1. Amefanya ziara ya kushtukiza katika Wizara ya fedha.
2. Amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kumsimamisha kazi aliyekuwa mkugenzi wa Hopitali hiyo kwa kipindi hicho. Aidha kwenye ziara hiyo aliagiza uongozi wa Hospitali hiyo kuhakikisha Machine za MRi na CT-SCAN zinafanyakazi na katika kutekeleza agizo hilo, Wizara ya fedha ilitoa zaidi ya Bil.3 kulipa sehemu ya madeni ya matengenezo ya mashine hizo.
3. kufanya ziara ya kushtukiza katika Mamlaka ya Bandari Tanzania.
4. Amefuta matumizi ya zaidi ya shilingi mil 250. zilizokuwa zitumike kwa ajili sherehe za ufunguzi wa bunge la 11 na zikapelekwa Hospitali ya MUHIMBILI kununua vitanda, magodoro na mashuka kwa ajili ya Wagonjwa.
5. Amefuta safasi kwa watumishi zaidi ya 50 waliokuwa wahudhurie mkutano wa jumuiya ya Madola nje ya nchi, safari ambayo ingegharimu takribani shilingi mil.700
6. Amefuta sherehe za siku ya Uhuru zinazofanyika Desemba 9 ya kila mwaka na kuagiza Watanzania kutumia siku hiyo kufanya usafi katika maeneo yao ili kukabiliana na mpuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambao kwa sasa uko mikoa mingi nchini. Kwa mujibu wa Katibu Mkuu kiongozi, Rais anafikiria pesa zitakazotokana na kufutwa kwa sherehe hizo zifanye kazi gani.
Nimeguswa sana na jitihada hizi binafsi(narudia, jitihada binafsi) za rais. Hivyo nimeamua kuanzisha mada mahsusi ambayo nitakuwa naihuisha kila wakati rais atapokuwa anaibuka na jambo jipya kabisa.
Mods, nawaomba sana mada hii ikae pale juu kabisa ili iwe inaonekana kirahisi kwa kila mmoja wetu ili kujionea mambo gani rais wetu yameapa uzito tangu aingie madarakani.
TUUNGE MKONO JUHUDI HIZI ZA MHE. RAIS KWA MAENDELEO YA TAIFA.

 
Habari wanaJF,

wa-Tanzania wameoadhimia kuacha tofauti zao za kisiasa na kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais wetu Dkt John Pombe Magufuli bado tuna-monitor na ku-evaluata siku 100 za Rais Dkt Magufuli. Feb 14, 2016 tutatoa tathimini ya jumla ya mafanikio na changamoto amezokumbana nazo ndani ya siku mia moja za mwanzo tangu kukaimu madaraka kama Rais wa Jamhuri.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Mi naona atafeli mapema kwa sababu ya kufanya kazi yake hizi kazi zinatakiwa zifanyike as ateam

Mtawala anatawala kwa neno sio kwa team, team zilizokuwapo nyuma mbona zilitudidimiza! Anatoa la moyoni watu wanashughulika. Hawezi fail, watendaji wapo kazini hata sasa, labda kama unazungumzia team mawaziri
 
Kama tunavyojua serikali imeendelea kupiga marufuku matumizi yasiyo ya muhimu ili kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na hizo pesa kupelekwa kwenye matumizi muhimu Zaidi na yenye tija kwa taifa, ili kuweka rekodi vizuri na baada ya miaka mitano tuweze kujua tumeokoa shilingi ngapi na manufa yaliyopatikana.

1.kufutwa kwa safari za nje kwa watumisshi wa serikali
2.kupunguza bajeti ya hafla ya wabunge na kuokoa Zaidi ya mil 200
3.kufutwa sherehe za uhuru
4.kufutwa maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani na hela hiyo kutumika kununulia madawa
5.marufuku ya utengeezaji na uchapishaji wa kadi za xmas na mwaka mpya kwa gharama za serikali

huu uzi utakuwa updated now and then kutokana na marufuku hizo
 
Kati ya mawazi amabao unaona katika siku walizoanza kazi ni akina nani unaona wanaendana na kasi nia, haki, ya kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi.?
 
Hakuna hata mmoja! Wote wanatafuta political Popularity tu kwa style ya kukurupuka.
 
namkubali prof.muhongo...this time amekuja kikazi zaidi...maneno kidogo no majigambo kazi kwenda mbele...
 
Ummy mwalimu waziri wa afya

Huyu mama ameanza vizuri hasa pale alipopangua uongozi wa Ocean Road; sasa anatakiwa asiishie hapo bali arejee hapo wizarani na kupangua uongozi wa kile kitengo kinachoshuhulikia wagonjwa wa kwenda nje, pale kuna watu wanaotakiwa kupumzishwa kwani hawana tija, pia kuna wakurugenzi wa idara ambao hawawezi kuendana na kasi inayotakiwa hususan imama mmoja huwa anakaimu ukatibu mkuu hapo ambae kutopandishwa kwake cheo kunamfanya awaharibie wanaoteuliwa juu yake hivyo kuwepo kwake ni shida hapo!!
 
Wote wanakwenda vizuri, kuna wale mawaziri wa mita 100 wanaonekana kwa sasa lakini wataishiwa pumzi tukifika huko mbele, 2020 tutajua waziri gani alijipanga kwa mbio za marathoni.
 
Back
Top Bottom