Sijui nitumie njia gani anielewe?

Sijui nitumie njia gani anielewe?

Joined
Dec 13, 2015
Posts
21
Reaction score
2
Habari zenu wanajamii forum wenzangu.

Natumaini amjambo na hizi siku kuu zinawaendea vyema. Kwa upande wangu siku kuu zimekaa vibaya mno.

Nilileta mada ya kuachwa na mpenzi ambaye bado anaendelea kuwa pamoja nami kwa kila hali.

Shida yangu ni kwamba, nimemuomba sana msamaha huyu bwana.

Nikiomba msamaha kwa njia ya simu anakua mkali sana tofauti na kuomba msamaha nikiwa ninamtazama.

Hapo kidogo anapunguza ukali na ninaona uelekeo wa kusamehewa.

Shida sasa ni kwamba, anapokuwa busy na kazi zake, sioni dalili hata ya kukumbukwa japo kwa message hata moja.

Nimeona bora nimuache kwanza mpaka siku kuu za mwaka mpya zitakapoanza ndipo niongee nae kiutu uzima kwani atakua ametulia na atakuwa tayari kunisikiliza.

Wanajamii forum, sio kwamba mimi ni king'ang'anizi kama wengine walivyosema, mimi ninampenda kweli huyu mtu kwa hali yoyote ambayo anayo.
Naona si busara kuacha penzi langu la kweli, nimeamua kupigania penzi langu.

Naombeni mnishauri, njia ipi nitaweza kuitumia ili nipate msamaha kutoka kwa mpenzi wangu?

Wanaume uwa mnapenda kufanyiwa nini ili mtoe msamaha?
 
Last edited by a moderator:
Father Superior!!!!??? Hiyo id iko sambamba na malalamiko yako? Au wewe ni shoga???
 
wewe niwa upande gani....? m/f/bwabwa...?
 
Pole,
Kamwe usikubali kulipoteza penzi la mtu ambae unahisi unampenda kirahisi

Pia kwenye msg hapo, usiache paka yeye akutext ndo nawewe ujibu. Uwe wewe unaanzisha chatting.
 
Msamaha unakuja with time, haulazimishwi. Sayari hii ina wanaume zaidi ya bilion 1, kama huyo wako hakusamehe u silazimishe labda alikuwa anatafuta sababu ya kuachana interest zake zimebadilika.
Usijipe moyo ukajiletea maumivu na kupoteza nguvu na muda wako kwa mtu asiyekupenda.
 
sasa utatumiaje id ya kiume dada, hebu kwanza mpe hilo tunda uone kama atakataa au vp
 
Msamaha unakuja with time, haulazimishwi. Sayari hii ina wanaume zaidi ya bilion 1, kama huyo wako hakusamehe u silazimishe labda alikuwa anatafuta sababu ya kuachana interest zake zimebadilika.
Usijipe moyo ukajiletea maumivu na kupoteza nguvu na muda wako kwa mtu asiyekupenda.

sasa hapo ushauri wako nini, asubirie msamaha au aende zake maana sijakusoma
 
Unampa dyudyu kwanza maana anaweza kukusamehe barabara wakati wa kupeana malove.
 
mtu akiwa na hasira inakubidi uwe mvumilivu usichoke kumtafuta msamaha wa gafla hivyo kama chafya haupo moyo utatulia kidogo kidogo hadi atarudi kama zaman ila nawewe ujionyeshe umebadilika sana
 
Back
Top Bottom