Sijui nitumie njia gani anielewe?

Sijui nitumie njia gani anielewe?

Ulimkosea nini? Kuna makosa ambayo wanaume husamehe kirahii lakini kuna mengine huwa ni vigumu kuyasamehe na hata akikubali kukusamehe, uhusiano huwa mgumu kurudi katika hali ya kawaida.
 
mm nikiwa na hasira napenda mtu aniache kdg hasira zangu zipungue, nikiwa nimekasirika na ww unafosi msamaha tena kwa kukera ndio unazidisha ugomvi labda jamaa yupo kama mm naweza kukusamehe bila hata kuniomba msamaha kama utaniacha kichwa kipoe sio umenivuruga alafu unaleta zile umenisamehe? nisamehe basi.. mwengine utamsikia ndio umekasirika? cheka basi..
 
Habari zenu wanajamii forum wenzangu.

Natumaini amjambo na hizi siku kuu zinawaendea vyema. Kwa upande wangu siku kuu zimekaa vibaya mno.

Nilileta mada ya kuachwa na mpenzi ambaye bado anaendelea kuwa pamoja nami kwa kila hali.

Shida yangu ni kwamba, nimemuomba sana msamaha huyu bwana.

Nikiomba msamaha kwa njia ya simu anakua mkali sana tofauti na kuomba msamaha nikiwa ninamtazama.

Hapo kidogo anapunguza ukali na ninaona uelekeo wa kusamehewa.

Shida sasa ni kwamba, anapokuwa busy na kazi zake, sioni dalili hata ya kukumbukwa japo kwa message hata moja.

Nimeona bora nimuache kwanza mpaka siku kuu za mwaka mpya zitakapoanza ndipo niongee nae kiutu uzima kwani atakua ametulia na atakuwa tayari kunisikiliza.

Wanajamii forum, sio kwamba mimi ni king'ang'anizi kama wengine walivyosema, mimi ninampenda kweli huyu mtu kwa hali yoyote ambayo anayo.
Naona si busara kuacha penzi langu la kweli, nimeamua kupigania penzi langu.

Naombeni mnishauri, njia ipi nitaweza kuitumia ili nipate msamaha kutoka kwa mpenzi wangu?

Wanaume uwa mnapenda kufanyiwa nini ili mtoe msamaha?
ogopa sana mwanaume anaetaka mawasiliano kisa yuko bize . Hata sms? Loh mmmmmmmm!
 
Back
Top Bottom