Sijui nichague wapi

Sijui nichague wapi

Huyo new brand anakupa kiasi gani cha pesa ?
 
HODII,mimi ni msichana mwenye umri wa miaka kadhaa,yaani umri wangu unaruhusu kuolewa, niliwahi kuumizwa na mapenzi kiasi kwamba sikuwaza kama nitakuja kutamani kuolewa.

Miaka kadhaa imepita karibu minne sijafanya ngono, sasa nimechoka, natamani mwenza angalau na mimi nipate mfariji, sasa nimepata boyfriend hajajitambulisha home siwezi kumuita mchumba.

Tatizo huyu kaka hanijali hata kidogo niliwahi kupata tatizo nikamuomba elfu 5 tu ya kitanzania yaani alinifokea kama mtoto mdogo eti mimi napenda pesa, sasa nikamchoka.

Nimepata mwingine bado hatujazoeana, sielewi kama na yeye mbahili au vp, je ni sahihi kumuacha yule wa kwanza na kuwa na huyu mpya au nimefuata matatizo zaidi?

Naombeni ushauri

Habari Cornath, kwanza kabisa pole na "experience" uliyokutana nayo katika mahusiano, ni vyema ukatambua ya kwamba si kila baya linatokea kwa ubaya, kuna mabaya yantokea ili kutujenga kifikra na kimtazamo. Ningependa kukushauri ya kwamba usiingie kwenye mahusiano kisa unatafuta mtu wa kukufariji nikiwa na sababu kuu mbili. Kwanza itajidhihirisha kwamba wewe ni mchoyo, nasema mchoyo kwa misingi ya kwamba mtazamo wako kwenye mahusiano utakua tu ya kwamba "MIMI" nifarijike, Je! vipi kuhusu mwenzako? Pili utakuwa "dissappointed" zaidi pale ambapo utakutana na mtu hasiyejali mfano mzuri ni huyo aliyekufokea kwa shilingi 5,000 tu.

Ufanye nini basi?

Kwanza jaribu kusahau YALIYOPITA penda na tamani sana ujipende wewe kama Cornath. Tafuta kuwa karibu sana na Mungu wako, penda kuwa mtu wa kusali maana bila msaada wa Mungu ni vigumu kupata ufumbuzi wa changamto za maisha. Vilevile chukua muda wa kutosha kumdadisi mtu na tabia yake nikimaanisha pelekeni urafiki wenu taratibu.
Nakutakia kila la kheri katika mahusiano yako na Mungu akutangulie.
 
Back
Top Bottom