Sijui mgomo wa madereva wa sasa utakuwaje Makonda akiwa Mkuu wa Mkoa

falcon mombasa

JF-Expert Member
Mar 5, 2015
9,159
9,241
Wakuu habari,

Moja kwa moja niende kwenye hoja. Mimi nikiwa kama mmoja wa wamiliki wa vyombo vinavyobeba abiria hapa nilikuwa na maswali kadhaa najiuliza.

Kwanza ieleweke sipo kwa lengo la kusifia chama fulani bali nitazungumza hali halisi
wakati wa mgomo uliopita nadhani miaka miwili nyuma mimi nilikuwa pale Ubungo, kwakweli makonda wakati ule alikuwa bado Mkuu wa Wilaya lakini kiukweli alishindwa kuuzima ule mgogoro na muda wote alikuja na kundi la askari (nasisitiza sisemi kwa mapenzi ya kisiasa) muda na siku zote za mgomo madereva walioandamana walikuwa na morale ya kujibizana na makonda kwa njia isiyosahihi ya ubabe na ugomvi.

Siku ya mwisho Mbowe alikuja Ubungo kwanza akazuiliwa na askari asiingie eneo la kituo lakini baadae aliruhusiwa akakutana na uongozi wa kituo. Baada ya dakika kadhaa Makonda akaja tena akamkuta Mbowe anaongea na madereva, lakini Makonda alipotokea taharuki ikarudi upya huku madereva wenye jazba wakitaka kumpiga.

Lakini Mbowe kwa ushawishi wake alifanikiwa kuwatuliza na mgomo ukaisha. Sasa ninachojiuliza hapa ni vipi Makonda atamudu kuondoa mgomo huu unaoanza siku ya jumanne akiwa kama Mkuu wa Mkoa ambaye ameandamwa na kashfa nyingi.

 
Hapo Bashite anakazi. Ngoja tuone maana tukiongea wanasema oh upinzani.
Ccm wanatumia nguvu nying na pesa nying za mzee pole pole kushinda humu jf
Lkn muda umefika wa nyeusi kuwa nyeusi na nyeupe kuwa nyeupe. Wapo na dereva ni kibwagizo tu.
Ngoja tuone
 
Kwa wanaoelewa watujuze. Kwani kwa sasa kuna mgomo wa madereva?
 
Hapo Bashite anakazi. Ngoja tuone maana tukiongea wanasema oh upinzani.
Ccm wanatumia nguvu nying na pesa nying za mzee pole pole kushinda humu jf
Lkn muda umefika wa nyeusi kuwa nyeusi na nyeupe kuwa nyeupe. Wapo na dereva ni kibwagizo tu.
Ngoja tuone
CHADEMA mnahangaika sana
 
siku ile alitaka kupigwa akajificha nyuma ya kova kama sikosei alikua kama harmo rappa yeye ni kiki tu

picha zipo zitawekwa humu na ziliwekwa jf haipotezi kitu
 
siku ile alitaka kupigwa akajificha nyuma ya kova kama sikosei alikua kama harmo rappa yeye ni kiki tu

picha zipo zitawekwa humu na ziliwekwa jf haipotezi kitu
unakumbukumbu nzuri nilidhani kuna watu watapinga humu
 
Wakuu habari,

Moja kwa moja niende kwenye hoja. Mimi nikiwa kama mmoja wa wamiliki wa vyombo vinavyobeba abiria hapa nilikuwa na maswali kadhaa najiuliza.

Kwanza ieleweke sipo kwa lengo la kusifia chama fulani bali nitazungumza hali halisi
wakati wa mgomo uliopita nadhani miaka miwili nyuma mimi nilikuwa pale Ubungo, kwakweli makonda wakati ule alikuwa bado Mkuu wa Wilaya lakini kiukweli alishindwa kuuzima ule mgogoro na muda wote alikuja na kundi la askari (nasisitiza sisemi kwa mapenzi ya kisiasa) muda na siku zote za mgomo madereva walioandamana walikuwa na morale ya kujibizana na makonda kwa njia isiyosahihi ya ubabe na ugomvi.

Siku ya mwisho Mbowe alikuja Ubungo kwanza akazuiliwa na askari asiingie eneo la kituo lakini baadae aliruhusiwa akakutana na uongozi wa kituo. Baada ya dakika kadhaa Makonda akaja tena akamkuta Mbowe anaongea na madereva, lakini Makonda alipotokea taharuki ikarudi upya huku madereva wenye jazba wakitaka kumpiga.

Lakini Mbowe kwa ushawishi wake alifanikiwa kuwatuliza na mgomo ukaisha. Sasa ninachojiuliza hapa ni vipi Makonda atamudu kuondoa mgomo huu unaoanza siku ya jumanne akiwa kama Mkuu wa Mkoa ambaye ameandamwa na kashfa nyingi.



Asiende, watamdai vyetii!
 
Back
Top Bottom