Sijamwelewa huyu CEO wa ATCL

Ni kawaida ndege kubeba mizigo wewe..Viti vinaondolewa kwenye reli unapakia mizigo.Wewe mshamba unadhani Viti vya ndege ni sawa na Viti vya mabasi ya daladala vilivyochomelewa welding!!!.Ndege waweza Toa Viti vyote dakika tu ndege ikabeba mizigo ya Aina yeyote.Ushamba mizigo.Wewe mshamba tu

Halafu mizigo utai-secure vipi baada ya kuondoa viti? Muwe mnasoma na kuelewa. Ndege ya abiria inaweza kuwa converted kuwa freighter lakini sio kirahisi kama unavyofikiri. Soma hapa halafu utuambie kama kilichoandikwa kina uhusiano na ulichozusha hapa.

 
Uwe unafatilia bunge ndilo linapanga bajeti hata ijayo ya Dreamliner -900 bunge limepitisha sasa wewe kazana kusema anajipangia ,unajiaibisha ufatilii wala husomi.
Nimemuona huyu CEO kwenye taarifa ya habari akilalamika kwamba eti abiria wanaotaka kutumia usafiri wa ndege wamekuwa wengi hivyo kuathiri na kusababisha kusitishwa na kucheleweshewa ratiba ya Safari za ndege.

Aliyemwelewa naomba anisaidie manake idadi ya siti kwenye ndege inajulikana wakishakata wanaotosheleza si chombo kinaondoka any how ndege Zina ratiba zake hata ikiwa haijaja inatakiwa iondoke kufuatana na ratiba.

Eti analalamika abiria wamekuwa wengi hivyo kusababisha kusitishwa kwa Safari.

Ana mpango wa kuongeza bodi hayo madege au ndio kazi imemshinda anaongea mapumba na mashudu yasiyoeleweka.

Biashara ya ndege ni ngumu tumeingizwa choo Cha kike na jiwe.

Itabidi jiwe azitapike hizo hela zetu alizotumia kienyeji kununulia ndege.
Aiingii akiline eti abiria kuongezeka kusababishe kusitisha Safari.

Kama Kuna anayeelewa vizuri / au alimwelewa yule Komba anieleweshe alikuwa anamaanisha Nini kwenye ongezeko la abiria na kusitishwa kwa Safari za ndege
 
K
Ndio zinabeba na wenye mizigo ukipakia mzigo kwenye ndege uliyolipia kubeba ruksa na wewe kupanda ndani ya hiyo ndege tena unakaa business class.Economy ndio inakuwepo mizigo yako.
kama kwenye kirikuuu mwenye mzigo mbele na dereva, mzigo nyuma,yehodaya shule hiyo.
 
Mpinga kristo
Kama hujawahi kukutana na shida za ATC hutaweza kuelewa kabisa hoja na mleta hoja kwa ujumla. Kifupi ni kwamba hawa waendeshaji wa ATC nafikiri bado hawajitambuhi kabisa. Wanandege mpya na nzuri sana ila wanakosa ufanisi na ubunifu wa kuhudumia wateja wao. Binafsi wamewahi kulikera mara mbili nikwa Mwanza mara moja nikiwa Zanzibar na mara moja nikiwa Dar.
Tunaomba wabadilike
 
Yaani ATCL Sasa hivi wao ndio kama sole service provider wa usafiri wa anga.Yaani Raisi Magufuli wakishindwa kufanya biashara fukuza wote hadi messenger Na mfagiaji.Ajiri watu wapya.Baraza la wafanyakazi na chama cha wafanyakazi ATCL kama menejimenti hawawezi endesha shirika wakomalieni vinginevyo kibarua kitaota majani kwenu wote.Msilete mzaha na ujinga kwenye customer care na good services to customers.Mtaondoka wrote na mafao mtalipwa baada ya miaka 20 Toka Sasa .Mimi Niko tayari kufungua kesi ya uhujumu uchumi dhidi yenu ambayo mkishafukuzwa itachukua miaka mingi kuamuliwa ili mradi nihakikishe hampati hata shilingi Moja ya mafao mkiafukuzwa Kazi
Kwani kiini "root cause" cha tatizo ni nini? Kama hatujaainisha root cause tunaweza kuwa tunafukuza watu bila kupata suluhisho.
 
labda abiria hua wanaachiwa wagombanie ndege kama daladala za gongolamboto/mbagala so ili kuepusha usumbufu wanaamua kuahirisha safari...
 
Tatizo la ATCL siyo abiria kuwa wengi ni mambo yafuatayo.
1. Safari zime pangwa nyingi muda wa karibu hivyo kuleta uhaba wa marubani kurusha ndege katika muda stahiki. Rubani hutakiwa kurusha ndege angalao masaa nane kwa siku na kwenda pumzika Hivyo hawezi pangiwa kurusha ndege tena hadi masaa ya kupumzika yatimie. Kutokana na hali hiyo inabidi kuchelewesha ndege kuondoka ili kusubiri muda ambao marubani watakuwa tayari kuruka.
2. Kitengo cha kupanga ratiba za ndege, marubani na wahudumu (cabin attendants), OPS kichunguzwe kwanini haya yanatokea. Kitengo hiki cha crew scheduling lazima kiwe madhubuti kuondoa kero hii na wawe na mtazamo wa muda wakupata marubani kwa wiki zisizo pungua mbili ili kama kuna wakati kutatokea marubani hawaja kuwa tayati basi safari iahirishwe na abiria wapewe taarifa mapema.
3. Ndani ya shirika kuna kamati ya wawakilishi toka idara mbali mbali hukutana na kupitia mienendo ya safari zilizo pita nakuona changamoto zilizo jitokeza zina chukuliwa hatua na kuzitafutia ufumbuzi. Kamati hii ya OTP, yaani On Time Performance, ni muhimu sana na ikutane si chini ya mara tatu au nne kwa wiki. Ikiwezekana kila siku. Changamoto zinazo jadiliwa ni sababu mbali mbali zilizo chelewesha ndege kuruka katika muda uliyo pangwa. Changamoto hizo ni pamoja na kuchelewa marubani na wahudumu, matatizo ya kiufundi, kuchelewa kupakia chakula, shida za abiria zilizo jitokeza kwenye ndege na kadhalika.
4. CEO awe mkweli kwa yale yanayojiri kwani shirika hili limekuwa na matatizo mengi kutokana na uwongozi kushindwa kuliendesha. Hii ni kujiona kwamba wao ndiyo shirika huku chini ni amri tu. Wataalamu washiriki mikutano ya management ili kusaidia kutatua kero kitaalamu. Muwakilishi mmoja toka fani mbali mbali ndani ya shirika ahudhurie vikao.
5. Upendeleo na makundi vimeshamiri ndani ya ATCL. Ipo haja kukomesha hili kwani utakuta wale wenye uwelewa na ujuzi wakibaguliwa hujirudisha nyuma matokeo ni wanao pendelewa ku fail na kampuni kuyumba mwisho kuanguka. Vyeo kupewa watu wanaojiona na kuwa karibu na viongozi iwe nje au ndani ya shirika. Hili nalo huchangia utendaji mbovu.
6. CEO asitafute mchawi. Yeye na management yake inabidi wabadilike wasizoee vyeo walivyo navyo waone ni dhamana to.
 
Uwe unafatilia bunge ndilo linapanga bajeti hata ijayo ya Dreamliner -900 bunge limepitisha sasa wewe kazana kusema anajipangia ,unajiaibisha ufatilii wala husomi.
Unataka alifuatilie kupitia nini ili hali halipo live!!?
Hutakiwi kumlaumu kwa sababu hana access nalo kwa hiyo yupo sawa kwa taarifa alikozipata hata kama siyo sahihi maana penye ukweli pamezuiwa
 
Nimemuona huyu CEO kwenye taarifa ya habari akilalamika kwamba eti abiria wanaotaka kutumia usafiri wa ndege wamekuwa wengi hivyo kuathiri na kusababisha kusitishwa na kucheleweshewa ratiba ya Safari za ndege.

Aliyemwelewa naomba anisaidie manake idadi ya siti kwenye ndege inajulikana wakishakata wanaotosheleza si chombo kinaondoka any how ndege Zina ratiba zake hata ikiwa haijaja inatakiwa iondoke kufuatana na ratiba.

Eti analalamika abiria wamekuwa wengi hivyo kusababisha kusitishwa kwa Safari.

Ana mpango wa kuongeza bodi hayo madege au ndio kazi imemshinda anaongea mapumba na mashudu yasiyoeleweka.

Biashara ya ndege ni ngumu tumeingizwa choo Cha kike na jiwe.

Itabidi jiwe azitapike hizo hela zetu alizotumia kienyeji kununulia ndege.
Aiingii akiline eti abiria kuongezeka kusababishe kusitisha Safari.

Kama Kuna anayeelewa vizuri / au alimwelewa yule Komba anieleweshe alikuwa anamaanisha Nini kwenye ongezeko la abiria na kusitishwa kwa Safari za ndege

Yaani huyu CEO anaongea as if ndege zimekua mabasi!

Tiketi zinakatiwa mlangoni!

Hili lijamaa ni mwehu kabisa!

Linadhani waTZ ni vilaza sana!

Tiketi zinakatwa online kwa kiwango tena ratiba zishapangwa miezi na miezi iliyopita already!

Huyu mpuuzi anaongea kama ndege ni Ngorika bus la Moshi!

CCM ni kirusi,kimevamia kila mahali watu wamewehuka kabisa!
 
Kuna haja ya kusimamia vyema Shirika ili lizidi kukua zaidi ya ilivyo sasa.
 
Back
Top Bottom