Siielewi hii miche yangu

Siielewi hii miche yangu

Aventus

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2013
Posts
2,011
Reaction score
2,181
IMG-20170608-WA0007.jpg
IMG-20170608-WA0004.jpg
IMG-20170608-WA0005.jpg
IMG-20170608-WA0006.jpg

Naona inarefuka tu ila hakuna maua
 
Maandalizi zaifu hutoa mtoto zaifu inaonyesha hukuanda ipasavyo hapo kuna ziki yamaji mbolea kama samba zima lipo hivyo hiyo nihasara tikiti linaanza kuza Kamba zikiwa dhaifu kabisa mkuu hapo utapata chenga tu nasidhani kama unaweza liokoa
 
1. Pole kongozi naona majani yamekakamaa/hajarelax, nadhani kuna shida ya baridi, au maji (kiasi kidogo) ,au kuna shida ya wadudu (white flies)=Elezea kuna shida yoyote kati ya hizo?

2.Udongo wako unaonekana una mfinyanzi kiasi fulani kwa ndani ndio maana unaona hiyo nyufa, sasa kaka hukuupiga hallo vizuri wakati wa maandalizi maana yake mizizi ya mmea inashindwa kupita kwa urahisi (Hard Pan).

3.Sina hakika sana na dawa za wadudu unazotumia kama ni sahihi, jitahidi kutumia dawa za wadudu ambazo pale chini karibu na kitako cha kopo , ukute kuna ufito wa rangi ya blue au Kijani, ukitumia zenye ufito wa rangi ya njano au red, hizo huua nyuki, na hufanya mmmea kuwa weak kidogo hasa kama unaspray mchana wa jua kali , na hakna maji ya kutosha. Dawa za ufito wa njano au nyekundu huua nyuki wanaosaidia uchavushaji, wakifa nyuki uwezekano wa kupata maua na matunda dhaifu ni mkubwa.

4. Hiyo mbegu uliyopanda ni aina gani (Kito?. Zebra?, Sukari F1?Sugar king?....).

5.Je umetumia booster (Maua/Matunda) yoyote?




 
1. Pole kongozi naona majani yamekakamaa/hajarelax, nadhani kuna shida ya baridi, au maji (kiasi kidogo) ,au kuna shida ya wadudu (white flies)=Elezea kuna shida yoyote kati ya hizo?

2.Udongo wako unaonekana una mfinyanzi kiasi fulani kwa ndani ndio maana unaona hiyo nyufa, sasa kaka hukuupiga hallo vizuri wakati wa maandalizi maana yake mizizi ya mmea inashindwa kupita kwa urahisi (Hard Pan).

3.Sina hakika sana na dawa za wadudu unazotumia kama ni sahihi, jitahidi kutumia dawa za wadudu ambazo pale chini karibu na kitako cha kopo , ukute kuna ufito wa rangi ya blue au Kijani, ukitumia zenye ufito wa rangi ya njano au red, hizo huua nyuki, na hufanya mmmea kuwa weak kidogo hasa kama unaspray mchana wa jua kali , na hakna maji ya kutosha. Dawa za ufito wa njano au nyekundu huua nyuki wanaosaidia uchavushaji, wakifa nyuki uwezekano wa kupata maua na matunda dhaifu ni mkubwa.

4. Hiyo mbegu uliyopanda ni aina gani (Kito?. Zebra?, Sukari F1?Sugar king?....).

5.Je umetumia booster (Maua/Matunda) yoyote?
Mbegu ni ya balton kiongozi.Hakika mimea haukupigwa dawa kwa wakati na pia maji ni machache.mana nilipata dharura ikabidi nimwache kijana sasa amekua si mfatiliaji
 
Kama hutojari toa yote anza upya huku ukizingatia ushauri uliotolewa juu ya ufuatiliaji
 
Mkuu hapo kwanza kuna ukosefu wa mbolea na pia maji inaonesha muda fulani yalikuwa mengi tikiti linahitaji unyevu tu basi.
Naomba msaada wa kupata majina ya mbolea za dukanji kwa ajili ya matikiti
 
Back
Top Bottom