Determinantor
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 61,358
- 100,385
Nasema tena Magazeti yetu ni vichekesho, na habari zetu zinafurahisha kusoma hadi unafurahi, tangu nianze kufuatilia magazeti haya nimejikuta naishiwa nguvu na kuogopa maana kama hawa ndio Waandishi wetu na hizi ndizo taarifa zetu, nasema TUMEKWISHA!!!
Nimependezewa na kuvutiwa na habari hii ya kuletewa simu za ANDROID kwa kila Mtanzania ifikapo 2020. Nikajiuliza faster maswali haya yafuatayo;
Kwa mtazamo wangu mimi, ni vyema Profesa Jk akaomba Makampuni yatupatie Teknolojia ya kutengeneza Simu kuliko kutuletea Simu.
Nimependezewa na kuvutiwa na habari hii ya kuletewa simu za ANDROID kwa kila Mtanzania ifikapo 2020. Nikajiuliza faster maswali haya yafuatayo;
- Yaani safari nzima ni kwenda kutuletea simu za Android?
- Halafu watatuletea na vipuri vyake?
- Hivi teknolojia inavyobadilika hadi 2020 tutakua kwenye hali gani?
- Hivi Profesa alishindwa kuwaomba watuletee teknolojia ya Ujenzi wa Simu kweli?
- Hizi simu zitakua zinajichaji zenyewe? Maana ukweli ni kwamba eneo kubwa halina umeme
Kwa mtazamo wangu mimi, ni vyema Profesa Jk akaomba Makampuni yatupatie Teknolojia ya kutengeneza Simu kuliko kutuletea Simu.