GE2025 Sigrada Mligo: Mimi sijafurahia kuwa Mbunge katika Bunge ambalo taifa linavuja damu

GE2025 Sigrada Mligo: Mimi sijafurahia kuwa Mbunge katika Bunge ambalo taifa linavuja damu

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
505
Reaction score
887
Sasa kama ujafurahishwa mbona umefika huko Bungeni? au unatuletea unafiki wako hapa!

Wewe kama umeona kuna hali mbaya kwa Watanzania wakati huu ungekataa, ila ukakubali kabisa na kufika hadi huko. Pesa tamu wewe tuache sisi kutulamba mikono wakati unataka kuvila vidole vyetu.
===============
Mbunge Mteule wa Viti Maalum kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Sigrada Mligo, amesema hajafurahishwa na uteuzi wake wa nafasi hiyo, akidai kuwa alinyang’anywa ushindi wa Ubunge wa Jimbo na kupewa nafasi ya ubunge wa Viti Maalum.

Mligo ametoa kauli hiyo leo, Novemba 10, 2025, katika viwanja vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mara baada ya kujisajili kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Kwanza wa Bunge la 13, unaotarajiwa kuanza Novemba 11, 2025.

Mligo amesema hajafurahishwa na namna alivyoteuliwa kuwa Mbunge wa Viti Maalum katika Mkoa wa Njombe, hasa katika kipindi ambacho Watanzania wanapitia hali ngumu ya Kisiasa na Kijamii.

Soma Pia: Tume Uhuru ya Taifa ya Uchaguzi INEC yatoa orodha wabunge viti maalum CCM wapo 113, CHAUMMA 2

"Wakati mimi naapishwa, kuna watu Mtaani wamezika ndugu zao, watu wamekufa. Taifa liko kimya. Mimi sijafurahia kuwa Mbunge katika Bunge ambalo taifa linavuja damu,” amesema Bi. Mligo.
 
Duu!
Baadaye ajisilikilize alivyoongea akiwa ametulia.
Lakini aache unafiki. Anajifanya hataki, wakati huo huo anataka! Aache kelele. Yeye aendelee tu kulitumikia tumbo lake
 
Anaogopa kasikia tutaliwasha bunge sasa anatafuta huruma.

Asingeenda kuapishwa tunge muhurumia, but it is too late mow.
 
Unafiki ni siasa na siasa ni unafki
 
"Kura elfu arobaini na mbili laki tisa na tisini na nane" (42,998,000) aliyeelewa hii namba anisaidie huyu ni mbunge anyeenda kukaa bungeni hajui hata hesabu ya chekechea dah maskini Tanzania yangu
 
"Kura elfu arobaini na mbili laki tisa na tisini na nane" (42,998,000) aliyeelewa hii namba anisaidie huyu ni mbunge anyeenda kukaa bungeni hajui hata hesabu ya chekechea dah maskini Tanzania yangu
Nimeshangaa sana. Ikabidi nirudie rudie kusikilliza.

Wabunge vilaza
 
Huo unafiki wa hali ya juu eti hajafurahishwa kwa nini ameenda?
 
Mnafiki.
Kama hajaridhishwa ajiondoe ili chama chake kimteue mwingine.
Asitupigie kelele
 
Atulie tu ajilie posho kuliko kubwabwaja maneno ya kinafiki
 
Back
Top Bottom