Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,027
- 20,413
ZIJUE SIFA ZA MTU AFAAYE KUWA KIONGOZI
Yeyote anaweza kuwa kiongozi lakini si Kila mtu anaweza kuwa kiongozi Bora, Bali washikaji wengi wamekuwa Viongozi kwa kulindwa na mifumo tu hata Kama wamekosa sifa kabisa.
Kalamu ya Mwana wa kasomi, kwa tafakuri ya kina inabainisha hapa sifa za Mtu kuwa kiongozi Bora ambazo akiwanazo anaweza kuwa kiongozi bora sana nazo Ni hizi zifiatazo;
1. AWE NA UWEZO
Sifa kuu ya mtu kuwa kiongozi Bora ni kuwa na uwezo wa kuyatenda kwa weledi yale yanayoihusu nafai anayoiendea, hii tunamaanisha uwezo wa kiakili n akimwili yaani ,awe na afya njema ya mwili na afya ya ubongo. Mtu asiye na uwezo wa kumudu majukumu na mikikimikiki ya nafasi yake hafai hata kidogo kuwa kiongozi wa nafasi hiyo.
2. AWE MKWELI
Ukweli Ni sifa muhimu Sana kwa mtu kuwa kiongozi Bora, awe mtu anayezungumza na kutenda yale ambayo akili yake inayaamini kuwa ndio ukweli na ayatende kadiri ya uwezo wake wote. Mtu yeyote ambaye ukweli umemtoka, mnafiki anayehadaa watu huku ameficha agenda anazojua yeye hafai na ni hatari kumwacha katika ofisi za umma.
3. ASIWE NA NDIMI MBILI
Msimamo na unyoofu wa maamzi na matendo Ni sifa muhimu Sana kwa mtu kuwa kiongozi Bora na akaleta tija, hakuna Jambo linavunja heshima ya mwanasiasa ama kiongozi wa taasisi yoyote kama kusema hiki leo n kesho kusema tofauti na hicho huku mitandao na akili za watu Bado zinakumbuka matamko yake ya awali. Mtu yeyote kigeugeu anayepeperuka Kama bendera kwa kutamka tamka tu na kugekia huku na kule Ni hatari Sana na jamii inao wajibu wa kumkana kwa vitendo kwa kupinga unafiki wake hadharani.
4. ASIZOELEE ULEVI
Kiongozi Bora ni mtu ambaye anapaswa kutokuwa wa kulewa na Mambo yote Kama vile kulewa madaraka, kulewa vilevi Kama pombe na madawa ya kulevya, asilewe umalaya nk. Mambo haya huondoa heshima kwa mtu huyo na huathiri uwezo wake wa kufanya maamzi sahihi na yenye maadili. Msela mlevi wa madaraka, anayetukana na kuumiza watu, anakanyaga katiba na kuongoza taasisi kwa utashi wa matakwa yake binafsi hasi hata kidogo kumiliki ofisi ya umma ama ya taasisi kwani athari zake Ni kubwa.
5. ASIYAENDEE MAPATO YA AIBU
Kiongozi Bora anapaswa kuwa mtu anayeyachukia MAPATO ya aibu anayopewa kwa mgongo wa uovu, rushwa, vyeo vya kupeana kishikaji na kuumiza wengine, ufisadi, kujinufaisha na Mali za umma kwa maslahi binafsi, Kula njama na kujivisha ukuu na heshima isiyoendana na uhalisia, kujiwekea Kinga nyingi dhidi ya taratibu za kuajibishwa ili Mambo yake yawe huru hata Kama atatenda tofauti. Mtu asiyeona haya kusimama mbele ya watu na kujiita mtetea wanyonge huku anawaumiza, asiyeona Soni kupokea rushwa kutoka kwa beberu na kuwafukuza wananchi kwa kubomoa nyumba zao ili beberu aliyemhonga afanya biashara zake, mtu asiyeona haya kutumia ofisi ya umma kwa maslahi yake binafsi Ni kama Simba aliyekabidhiwa kulinda mbuzi huku akiwafanya kuwa chakula chake ili aendelee kuishi awalinde wasidhurike.
Baada ya Tafakuri nzito hii ya Mwana wa Kasomi, unadhani wewe mwenye mamlaka uko sawasawa kuwepo hapo kutokana na matendo yako? Kama jibu Ni siyo badilika na Kama huwezi achia ngazi, je wewe unayetamani kuwa kiongozi umeona mapungufu yako? Jisahihishe ungali katika maandalizi, Bali wale WASIO na hizi sifa na wangali mamlakani wanapaswa kukosolewa na kulazimishwa kujirekebisha kwa maslahi ya jamii zetu, Tafakuri jenzi na ndivyo.
Yeyote anaweza kuwa kiongozi lakini si Kila mtu anaweza kuwa kiongozi Bora, Bali washikaji wengi wamekuwa Viongozi kwa kulindwa na mifumo tu hata Kama wamekosa sifa kabisa.
Kalamu ya Mwana wa kasomi, kwa tafakuri ya kina inabainisha hapa sifa za Mtu kuwa kiongozi Bora ambazo akiwanazo anaweza kuwa kiongozi bora sana nazo Ni hizi zifiatazo;
1. AWE NA UWEZO
Sifa kuu ya mtu kuwa kiongozi Bora ni kuwa na uwezo wa kuyatenda kwa weledi yale yanayoihusu nafai anayoiendea, hii tunamaanisha uwezo wa kiakili n akimwili yaani ,awe na afya njema ya mwili na afya ya ubongo. Mtu asiye na uwezo wa kumudu majukumu na mikikimikiki ya nafasi yake hafai hata kidogo kuwa kiongozi wa nafasi hiyo.
2. AWE MKWELI
Ukweli Ni sifa muhimu Sana kwa mtu kuwa kiongozi Bora, awe mtu anayezungumza na kutenda yale ambayo akili yake inayaamini kuwa ndio ukweli na ayatende kadiri ya uwezo wake wote. Mtu yeyote ambaye ukweli umemtoka, mnafiki anayehadaa watu huku ameficha agenda anazojua yeye hafai na ni hatari kumwacha katika ofisi za umma.
3. ASIWE NA NDIMI MBILI
Msimamo na unyoofu wa maamzi na matendo Ni sifa muhimu Sana kwa mtu kuwa kiongozi Bora na akaleta tija, hakuna Jambo linavunja heshima ya mwanasiasa ama kiongozi wa taasisi yoyote kama kusema hiki leo n kesho kusema tofauti na hicho huku mitandao na akili za watu Bado zinakumbuka matamko yake ya awali. Mtu yeyote kigeugeu anayepeperuka Kama bendera kwa kutamka tamka tu na kugekia huku na kule Ni hatari Sana na jamii inao wajibu wa kumkana kwa vitendo kwa kupinga unafiki wake hadharani.
4. ASIZOELEE ULEVI
Kiongozi Bora ni mtu ambaye anapaswa kutokuwa wa kulewa na Mambo yote Kama vile kulewa madaraka, kulewa vilevi Kama pombe na madawa ya kulevya, asilewe umalaya nk. Mambo haya huondoa heshima kwa mtu huyo na huathiri uwezo wake wa kufanya maamzi sahihi na yenye maadili. Msela mlevi wa madaraka, anayetukana na kuumiza watu, anakanyaga katiba na kuongoza taasisi kwa utashi wa matakwa yake binafsi hasi hata kidogo kumiliki ofisi ya umma ama ya taasisi kwani athari zake Ni kubwa.
5. ASIYAENDEE MAPATO YA AIBU
Kiongozi Bora anapaswa kuwa mtu anayeyachukia MAPATO ya aibu anayopewa kwa mgongo wa uovu, rushwa, vyeo vya kupeana kishikaji na kuumiza wengine, ufisadi, kujinufaisha na Mali za umma kwa maslahi binafsi, Kula njama na kujivisha ukuu na heshima isiyoendana na uhalisia, kujiwekea Kinga nyingi dhidi ya taratibu za kuajibishwa ili Mambo yake yawe huru hata Kama atatenda tofauti. Mtu asiyeona haya kusimama mbele ya watu na kujiita mtetea wanyonge huku anawaumiza, asiyeona Soni kupokea rushwa kutoka kwa beberu na kuwafukuza wananchi kwa kubomoa nyumba zao ili beberu aliyemhonga afanya biashara zake, mtu asiyeona haya kutumia ofisi ya umma kwa maslahi yake binafsi Ni kama Simba aliyekabidhiwa kulinda mbuzi huku akiwafanya kuwa chakula chake ili aendelee kuishi awalinde wasidhurike.
Baada ya Tafakuri nzito hii ya Mwana wa Kasomi, unadhani wewe mwenye mamlaka uko sawasawa kuwepo hapo kutokana na matendo yako? Kama jibu Ni siyo badilika na Kama huwezi achia ngazi, je wewe unayetamani kuwa kiongozi umeona mapungufu yako? Jisahihishe ungali katika maandalizi, Bali wale WASIO na hizi sifa na wangali mamlakani wanapaswa kukosolewa na kulazimishwa kujirekebisha kwa maslahi ya jamii zetu, Tafakuri jenzi na ndivyo.