Mie kukuchezea rafu,ubavu huo ntatoa wapi
hapa nilipo nipo dhohofu,kukuwaza kila wakati
Njoo kwangu asali,useme nikupeleke wapi
najitahidi kila hali,uweze kunikumbuka kila wakati
Hakika nimekusoma, Ufafanuzi murua,
Fikira zilinihama, nikajua watania,
Mawazo yalishazama, lugha sikuitambua,
Utapata wa kuoa, Mola kishakupangia.
Mola kishakupangia, Utapata wa kuoa,
Wala hautojutia, Raha utajipatia,
Naye atawajalia, bora yenu familia
Utapata wa kuoa, Mola kishakupangia.
Amina amina sana, nasema tena amina,
Amina tena na tena, Tena na tena amina,
Tena nasema amina, Amina ilo amina,
Utapata wa kuoa, Mola kishakupangia.
ODM
Niliomba mwaka jana, ila sasa nishaoa.
Ninamiliki kimwana, toto la kitanzanzania.
Anayo shepu mwanana, kitabia katulia.
Sikupata asosoma, msomi nimemkwaa.
Nyumbani nikimuona, nasahau kutembea.
Maisha yawa mwanana, dodo langu najilia.
Twamuomba maulana, watoto kutupatia.
Sikupata asosoma, msomi nimemkwaa.
By Sauti ya nyikani.
Ukitaka kuoa oa tu,acha kuchunguza kuku,
ukimpenda muoe,omba mungu akutunuku,
ndoa zina mengi,usidhani ni kula kuku
wanaofaa wako wengi,acha upukupuku.....
Najikutaga tu napenda kukukoti.
Heeeee!!!!!!!!! safi sana, mke hutafutwa kwa nyimbo, huolewa kwa nyimbo na vigelegele na hubembelezwa kwa nyimbo.
hongera utunzi mzur sanaaa
Hahaha nacheka sana, Nacheka mimi hahaha,
Umenipata kwa kina, wacha nicheke hahaha,
Sikukupata upana, hahahaha hahahaha,
Hongera kwa kuopoa, kimwanacho maridhawa.
Ila chonde angalia, wakware wengi mjini,
Kazi yao kuvizia, vizuri vilivyo ndani,
Usije hapa kulia, Wamekupora mwandani,
Hongera kwa kuopoa, kimwanacho maridhawa.
Hahahahaaa.
Nimekuelewa sana, sitofanya masikhara. Nitamganda kimwana, wasije wakanipora. Nitamtunza kichuna, ili azidi kung'ara. Nashukuru kuopoa, mrembo maridhawa.