Sifa za kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Sifa za kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Robot la Matope

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2015
Posts
8,584
Reaction score
17,528
Kulingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (kama ilivyorekebishwa), sifa za mtu anayestahili kuteuliwa kuwa Attorney General (Mwanasheria Mkuu wa Serikali) zimeelezwa katika Ibara ya 59(3).

Sifa za kuwa Attorney General wa Tanzania

Kwa mujibu wa Katiba hiyo:

1. Lazima awe raia wa Tanzania.

Mtu huyo ni lazima awe raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuzaliwa au kwa kupewa uraia kwa mujibu wa sheria.

2. Lazima awe ni wakili mwenye sifa.

Mtu huyo ni lazima awe amehitimu taaluma ya sheria na ameandikishwa kuwa wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

3. Uzoefu wa kutosha katika taaluma ya sheria.

Katiba inataka awe amefanya kazi kama wakili kwa muda usiopungua miaka 10 tangu aandikishwe kama wakili wa Mahakama Kuu.

4. Kuteuliwa na Rais.

Attorney General huteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mujibu wa mamlaka aliyo nayo chini ya Katiba.

NB: Sometimes N is silent in lines like T in listen
 
Hamza Johari si wakili. Halafu kasomea huko Ukraine. Kwanza inawezekana cheti cha kufoji. Ila si wakili ndo maana alimuuliza DPP kama wana agreement na USA za kuweza kumleta Mange Tanzania. Inshort mwanasheria mkuu hajui sheria na katiba ya Tanzania. Aibu naona mimi ,ndo taabu ya kuwa na Rais la Saba felia.
 
Hamza Johari si wakili. Halafu kasomea huko Ukraine. Kwanza inawezekana cheti cha kufoji. Ila si wakili ndo maana alimuuliza DP kama wana agreement na USA za kuweza kumleta Mange Tanzania. Inshort mwanasheria mkuu hajui sheria na katika ya Tanzania. Aibu naona mimi ,ndo taabu ya kuwa na Rais la Saba felia.
Labda atatumia experience ya DPP?
 
Hamza Johari si wakili. Halafu kasomea huko Ukraine. Kwanza inawezekana cheti cha kufoji. Ila si wakili ndo maana alimuuliza DP kama wana agreement na USA za kuweza kumleta Mange Tanzania. Inshort mwanasheria mkuu hajui sheria na katika ya Tanzania. Aibu naona mimi ,ndo taabu ya kuwa na Rais la Saba felia.
Yule mtu aliposema hivyo ndio nikaona ni mweupe.

Yaani sasa hivi ukitaka kukimbia Tanzania ni simple sana, unachukua hizo picha wanazouia watu wasiwe nazo, habari ya Usalama ya Ubalozi wa Marekani, BBC na Al-Jazeera unaeedna ubalozi wowote wa Ulaya wanakupa Assylum
 
Hajui sheria,itakuwa hata wanasheria hapo kitengoni wanamwingiza chaka kirahisi.Halafu akitoka hapo atakuja teuliwa kuwa jaji.Jaji hajui sheria za Tanzania.
Wakati wa jk alikua ofisi ya mwanasheria mkuu,magu alimpeleka aviation,ni miongoni mwa walioikomboa ndege ilipodakwa south
 
Yule mtu aliposema hivyo ndio nikaona ni mweupe.

Yaani sasa hivi ukitaka kukimbia Tanzania ni simple sana, unachukua hizo picha wanazouia watu wasiwe nazo, habari ya Usalama ya Ubalozi wa Marekani, BBC na Al-Jazeera unaeedna ubalozi wowote wa Ulaya wanakupa Assylum
Bado una mentality ya 80s,90s,00s ya kwenda ulaya!?
 
Back
Top Bottom