Sichangii harusi wala kutoa sadaka kanisani

Sichangii harusi wala kutoa sadaka kanisani

LUBEDE

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2013
Posts
4,322
Reaction score
6,694
Wakuu,katika maisha yangu nilishajiwekea nadhili(kiapo),

kuwa kamwe sitokuja kuchangia harusi wala kutoa sadaka kanisani(mimi ni mkristo).

Mwanzoni nilikutana na vigingi,vikwazo na vitisho kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki,
baada ya kuwapa msimamo wangu,hasa baada ya kuona nina kadi karibia kumi zinataka elfu 50 na 70 na za laki nichangie,
nikapata wazo na akili mpya ya kubadilisha mfumo wa maisha.


Pamoja na kuambiwa kuwa ipo siku na mimi nitapata shida na sitochangiwa,niliamua kuziba pamba masikio na kuisikiliza nafsi yangu,

Nashukuru mungu leo nafunga mwaka wa tatu bila kufanya huo niliouona upuuzi,na hakuna ghasia yeyote iliyonipata,
maana michango yangu niliamua kuielekeza kwa wenye uhitaji wa lazima like magonjwa,elimu,na matatizo ya ghafla(misiba)na mengineyo yasiyo anasa,matokeo yake bado nimeendelea kukubalika zaidi na kuonekana kama Saint kutoka kwa wale walionikatisha tamaa.


Najipongeza kwa kufikisha hii miaka mitatu bila kutoa michango nyonyevu,tukiamua tunaweza,hakuna linaloshindikana!
 
Sawa umemaliza miaka mitatu huchangii, unataka kutuambia nini hasa ? Na sisi tusichangie ? Nini lengo la huu uzi ?

Ama watu wasitoe sadaka kanisani ? Yani hela nitafute kwa jasho langu nipangiwe matumizi ? Ni hivi mkuu, mbuzi hula kulingana na urefu wa kamba yake !
Kama kitu umeona huna uwezo nacho acha, !!!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kutoa michango ya harusi hulazimishwi wengi tunatoa kwa watu wetu wa karibu ili kuweza kufanikisha na kujumuika nao katika siku yao, kuhusu sadaka hiyo unayotoa ni sadaka pia, japo jukumu la kujenga kanisa unajiepusha nalo

Ukiachana na michango ya harusi, watu huwa wanashona na kununua nguo za bei ghali pamoja na zawadi, zaidi hata ya mchango waliotoa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona umeamua kuandika upuuzi, bila shaka hukufikiria vizuri vinginevyo ungo wako utakuwa umecheza... Sadaka kanisani ni sehemu ya ibada labda kama hujui maana ya sadaka. Kifupi ni kwamba una miaka mitatu hujafanya ibada..sasa ni kuuulize huo ni ujanja am a ujinga? Kwakuto kutoa kwako sadaka kanisa limeteteleka? Je wanaotoa wamefilisika? Arusi hazifanyiki kwa sababu we hutoi?

Mungu kwakukuacha kuendelea kuwa hai huku ukiwa na afya tele tayari ameshatoa sadaka.. Au nikuulize unamlipa nini Mungu kwa uhai na uzima anakupa? Au hizo pesa unazosema hutoi nani anakuwezesha kuzipata? Ungekuwa na akili timamu usingeleta huu upuuzi wako mbele za GT.

Narudia kusema huo ulioleta hapa ni upuuzi utawapata wapuuzi wenzio.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu ujumbe umekuja wakati mwafaka.
Kuna mtu Jana niko kazini ananiambia kuna kadi yako ya mchango wa harusi.
Naahidi sitotoa kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,katika maisha yangu nilishajiwekea nadhili(kiapo),
kuwa kamwe sitokuja kuchangia harusi wala kutoa sadaka kanisani(mimi ni mkristo).
Mwanzoni nilikutana na vigingi,vikwazo na vitisho kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki,
baada ya kuwapa msimamo wangu,hasa baada ya kuona nina kadi karibia kumi zinataka elfu 50 na 70 na za laki nichangie,
nikapata wazo na akili mpya ya kubadilisha mfumo wa maisha.
Pamoja na kuambiwa kuwa ipo siku na mimi nitapata shida na sitochangiwa,niliamua kuziba pamba masikio na kuisikiliza nafsi yangu,
nashukuru mungu leo nafunga mwaka wa tatu bila kufanya huo niliouona upuuzi,na hakuna ghasia yeyote iliyonipata,
maana michango yangu niliamua kuielekeza kwa wenye uhitaji wa lazima like magonjwa,elimu,na matatizo ya ghafla(misiba)na mengineyo yasiyo anasa,matokeo yake bado nimeendelea kukubalika zaidi na kuonekana kama Saint kutoka kwa wale walionikatisha tamaa.
Najipongeza kwa kufikisha hii miaka mitatu bila kutoa michango nyonyevu,tukiamua tunaweza,hakuna linaloshindikana
!
Acha ubahili wa kijinga huo
Toa sadaka wewe hilo ndio muhimu sana
Ama michango ya harusi hiyar yako wewe si tayari umeshaoa? Kwani una mpango wa kuongeza mke ili na wewe uchangiwe?
Kama una binti subir akiposwa wambie mahar mil 5 na wakitoa hapohapo muozeshe haraka kablahujazila hizo pesa
Na kama una kijana wa kuoa mwambie asikurupuke mpaka awe ana pesa ya kutosha mahar na sherehe aibebe mwenyewe!! Au wewe uwe na pesa!!!!
Hiyo kwetu inaitwa KUNKA NKUKENKE
Ni ushauri tu ndugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha ubahili wa kijinga huo
Toa sadaka wewe hilo ndio muhimu sana
Ama michango ya harusi hiyar yako wewe si tayari umeshaoa? Kwani una mpango wa kuongeza mke ili na wewe uchangiwe?
Kama una binti subir akiposwa wambie mahar mil 5 na wakitoa hapohapo muozeshe haraka kablahujazila hizo pesa
Na kama una kijana wa kuoa mwambie asikurupuke mpaka awe ana pesa ya kutosha mahar na sherehe aibebe mwenyewe!! Au wewe uwe na pesa!!!!
Hiyo kwetu inaitwa KUNKA NKUKENKE
Ni ushauri tu ndugu

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ni SHEMASI au IMAMU?
 
Naona watu mnatokwa mapovu bure bila kumuelewa mleta mada. Yeye kasema ameamua kuhamishia michango yake kwa wenye uhitaji eg wagonjwa, wafiwa, mayatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu. Hapo ana kosa gani? Mimi namuunga mkono 100%! Na kama watu wote tungefanya kama huyu, basi fedha zetu zingesaidia sana kutatua matatizo ya msingi yanayotukabili badala ya kuziteketeza kwenye sherehe ya siku moja au kununua magari ya kifahari na majumba ya wachungaji!
 
Ongera mkuu na pole maana siku yakikukuta hayo ya kukukuta itabidi uzibe masikio na macho kama unavyofanya sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huu ni uoga wa kijinga. Amin nakuambia, siku yakimkuta atasaidiwa na hao anaowasaidia sasa. Ukimlipia mtu ada, au bili ya hospitali, au ukamsaidia akiwa na shida, atakukumbuka mara 100 zaidi ya yule uliemchangia kwenye harusi.
 
Back
Top Bottom