bhikola
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 1,133
- 1,668
WINO WA DHAHABU..... NILIWAHI KUANDIKA.
SIASA INAVYOVUNA WATAALAMU.
Na Thadei Ole Mushi.
Pale alipo Dr. Mwakyembe, Dr. Tulia,Pro Kabudi, Pro Mbarawa na huko anakokimbilia Prof Kitila Mkumbo na sasa Dr Bashiru Ally ndiko kwenye pesa ya maana.
Kwa Taarifa yako Katika ukanda wa Afrika mashariki Tanzania ndio nchi pekee yenye maprofesa na watu wenye Phd wachache kuliko nchi giants za A. Mashariki na kusini mwa jangwa la sahara. Pamoja na uchache wao Siasa inazidi kuwavuna kila siku... huko ndiko kuliko na Maslah mapana.
Kwa statistics za mwaka 2016 Vyuo vikuu binafsi nchini vilikuwa 35 ila vilikuwa na maprofesa 74 tu hawa ni wale maprofesa kamili. Associate walikuwepo 56 hawa ukijumlisha na hao 74 unapata 130. Associate maana yake ni accademic rank iliyopo kati ya assistant professor na Full professor (operational meaning)
Ambao wana Phd kwenye vyuo vya binafsi ambao wanafundisha ni 138. Ukijumlisha na idadi ya maprofesa unapata 268. Hawa ndio wanaohudumia karibu zaidi ya nusu ya wadahiliwa wote Tanzania wanaosoma vyuo vya binafsi.
Kwa upande wa serikali Full Prof walikuwepo 204 huku associate wakiwa 309 na Phd wakiwa 514 wote hawa wanatengeneza staff ya watu 1,027. Hawa ndio wataalamu wabobezi wanaohudumia vyuo vyote vya Seriali nchini hadi kufikia 2016.
Hadi kufikia 2016 kuliwa kuna vyuo vikuu zaidi ya vinne havina Prof hata mmoja huku kimoja cha serikali kikiwa na Prof mmoja.Nafikiri hivi ni vile vilivyonyimwa udahili wa wanafunzi.
Chuo kilichokuwa kinaongoza kwa kuwa na maprof wengi ni chuo cha SUA kikiwa na maprof 75 huku UDSM ikiwa na maprof 67 hadi kufikia 2016. Kwenge vyuo vya binafsi kuna balaaa kubwa....
Kenya wao miaka 3 iliyopita walikuwa na maprofesa kwenye vyuo vyao vya Serikali 5,189, jumlisha hawa wakwetu kama hata wanafika nusu.
Kenya Kwa mwaka wanazalisha Phd 1,000 huku Tanzania tukizalisha chini ya 500 kwa mwaka.
Tanzania Imefikia mahali umri wa kustaafu wa maprofesa chuoni umeongezwa hadi karibu kufikia miaka 80. Hiki ni kiashiria cha Tatizo kubwa lililopo.
Vyuo vyetu vya binafsi vimeanza kuajiri maprofesa toka nchi jirani kama Kenya huku tukipigana kusema ajira hakuna....
Ni wakati sasa wa Serikali kufikiri namna bora ya kuboresha maslahi ya hawa wataalamu wanaokimbilia kwenye siasa ili wabaki kuzalisha wataalamu wengine.
Wanavyuo wengi wanaomaliza vyuo vikuu kwa sasa hata kuandika barua ya kuomba kazi hawawezi inawezekana ni ukisefu wa wataalamu bora mavyuoni.... .... mimi Sijui.
Ukiangalia bidhaa zinazotengenezwa hapa kwetu ni za kuhesabu ila kila mwaka vyuo vyetu vikuu na vyuo vya kati vinamwaga maelfu ya wahandisi mtaani..... jamani hata Toroli mmeshindwa kulitengeneza....
Hata wataalamu waliobakia wameshaanza kuwa na element za siasa inawezekana nao wapo njiani kutoka. Siku hizi wanajitokeza hadharani kabisa na kusifia chama fulani bila woga... wanakaa karibu na wanasiasa ili kuambulia chochote.......
Haya tunayazungumza huku kada ya Siasa ikiwa inadharau kazi nyingi za wataalamu. Jiulize ni Tafiti ngapi zipo kwenye maktaba zetu za vyuo vikuu na jiulize zinatumika wapi. Katika hali hiyo unafikiri kuna haja ya hawa wataalamu kuumiza kichwa huku kazi zao zikiwa hazitambuliki au wavae Suti wakapige mabenchi makofi pale Dodoma huku wakiingiza mamilioni.??
Ni aibu kwa profesa aliyebaki pale Muhimbili kuzidiwa mshahara na kibajaji na kina mlinga hahahahaha, Natania tu ila unaweza kuona ni kwa namna gani hawa wataalamu wetu wanavyojiongeza. Unamwona Dr. Bana anavyojitutumua? Nani anataka kustaafu na kiinua Mgongo cha ajabu ajabu?
Angalia Umri wanaoondoka nao hawa kina Kitila mkumbo, Dr Tulia na Sasa Bashiru Ally. Ni Umri uliokuwa unahitajika haswa katika kuzalisha wataalamu. Ila tujiulize nini kingeweza kuwashawishi kubaki pale mlimani zaidi ya kukimbilia kwenye Siasa? Jambo pekee ni Maslahi. Kwa maana hiyo tusiwalaumu hata kidogo wamewaza njee ya Box
Kila La kheri Dr Bashiru
Ole Mushi.
0712702602.
SIASA INAVYOVUNA WATAALAMU.
Na Thadei Ole Mushi.
Pale alipo Dr. Mwakyembe, Dr. Tulia,Pro Kabudi, Pro Mbarawa na huko anakokimbilia Prof Kitila Mkumbo na sasa Dr Bashiru Ally ndiko kwenye pesa ya maana.
Kwa Taarifa yako Katika ukanda wa Afrika mashariki Tanzania ndio nchi pekee yenye maprofesa na watu wenye Phd wachache kuliko nchi giants za A. Mashariki na kusini mwa jangwa la sahara. Pamoja na uchache wao Siasa inazidi kuwavuna kila siku... huko ndiko kuliko na Maslah mapana.
Kwa statistics za mwaka 2016 Vyuo vikuu binafsi nchini vilikuwa 35 ila vilikuwa na maprofesa 74 tu hawa ni wale maprofesa kamili. Associate walikuwepo 56 hawa ukijumlisha na hao 74 unapata 130. Associate maana yake ni accademic rank iliyopo kati ya assistant professor na Full professor (operational meaning)
Ambao wana Phd kwenye vyuo vya binafsi ambao wanafundisha ni 138. Ukijumlisha na idadi ya maprofesa unapata 268. Hawa ndio wanaohudumia karibu zaidi ya nusu ya wadahiliwa wote Tanzania wanaosoma vyuo vya binafsi.
Kwa upande wa serikali Full Prof walikuwepo 204 huku associate wakiwa 309 na Phd wakiwa 514 wote hawa wanatengeneza staff ya watu 1,027. Hawa ndio wataalamu wabobezi wanaohudumia vyuo vyote vya Seriali nchini hadi kufikia 2016.
Hadi kufikia 2016 kuliwa kuna vyuo vikuu zaidi ya vinne havina Prof hata mmoja huku kimoja cha serikali kikiwa na Prof mmoja.Nafikiri hivi ni vile vilivyonyimwa udahili wa wanafunzi.
Chuo kilichokuwa kinaongoza kwa kuwa na maprof wengi ni chuo cha SUA kikiwa na maprof 75 huku UDSM ikiwa na maprof 67 hadi kufikia 2016. Kwenge vyuo vya binafsi kuna balaaa kubwa....
Kenya wao miaka 3 iliyopita walikuwa na maprofesa kwenye vyuo vyao vya Serikali 5,189, jumlisha hawa wakwetu kama hata wanafika nusu.
Kenya Kwa mwaka wanazalisha Phd 1,000 huku Tanzania tukizalisha chini ya 500 kwa mwaka.
Tanzania Imefikia mahali umri wa kustaafu wa maprofesa chuoni umeongezwa hadi karibu kufikia miaka 80. Hiki ni kiashiria cha Tatizo kubwa lililopo.
Vyuo vyetu vya binafsi vimeanza kuajiri maprofesa toka nchi jirani kama Kenya huku tukipigana kusema ajira hakuna....
Ni wakati sasa wa Serikali kufikiri namna bora ya kuboresha maslahi ya hawa wataalamu wanaokimbilia kwenye siasa ili wabaki kuzalisha wataalamu wengine.
Wanavyuo wengi wanaomaliza vyuo vikuu kwa sasa hata kuandika barua ya kuomba kazi hawawezi inawezekana ni ukisefu wa wataalamu bora mavyuoni.... .... mimi Sijui.
Ukiangalia bidhaa zinazotengenezwa hapa kwetu ni za kuhesabu ila kila mwaka vyuo vyetu vikuu na vyuo vya kati vinamwaga maelfu ya wahandisi mtaani..... jamani hata Toroli mmeshindwa kulitengeneza....
Hata wataalamu waliobakia wameshaanza kuwa na element za siasa inawezekana nao wapo njiani kutoka. Siku hizi wanajitokeza hadharani kabisa na kusifia chama fulani bila woga... wanakaa karibu na wanasiasa ili kuambulia chochote.......
Haya tunayazungumza huku kada ya Siasa ikiwa inadharau kazi nyingi za wataalamu. Jiulize ni Tafiti ngapi zipo kwenye maktaba zetu za vyuo vikuu na jiulize zinatumika wapi. Katika hali hiyo unafikiri kuna haja ya hawa wataalamu kuumiza kichwa huku kazi zao zikiwa hazitambuliki au wavae Suti wakapige mabenchi makofi pale Dodoma huku wakiingiza mamilioni.??
Ni aibu kwa profesa aliyebaki pale Muhimbili kuzidiwa mshahara na kibajaji na kina mlinga hahahahaha, Natania tu ila unaweza kuona ni kwa namna gani hawa wataalamu wetu wanavyojiongeza. Unamwona Dr. Bana anavyojitutumua? Nani anataka kustaafu na kiinua Mgongo cha ajabu ajabu?
Angalia Umri wanaoondoka nao hawa kina Kitila mkumbo, Dr Tulia na Sasa Bashiru Ally. Ni Umri uliokuwa unahitajika haswa katika kuzalisha wataalamu. Ila tujiulize nini kingeweza kuwashawishi kubaki pale mlimani zaidi ya kukimbilia kwenye Siasa? Jambo pekee ni Maslahi. Kwa maana hiyo tusiwalaumu hata kidogo wamewaza njee ya Box
Kila La kheri Dr Bashiru
Ole Mushi.
0712702602.