Siasa na Dini mapacha wanaofanana ama wasiofanana?

Siasa na Dini mapacha wanaofanana ama wasiofanana?

emmanuel1976

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2011
Posts
301
Reaction score
80
Poleni sana kwa mafuriko hasa wale waliokutwa nayo!

Wana jamvi habarini za asubuhi. Natumaini hamjambo. Kwa miaka mingi hapa kwetu Tanzania kumekuwa na dhana kwamba viongozi wa dini hawapaswi kuingilia masuala ya siasa kwa maana ya ama kukemea viongozi wa kisiasa wanapopotoka ama wakati wa kuwaweka viongozi madarakani (chaguzi mbali mbali). Hali hii imeenda umbali hadi kufikia wana siasa kuwakemea viongozi wa dini kutojihusisha na masuala yanayohusu siasa hasa pale viongozi wa dini wanapokuwa kinyume na watawala wetu.

Mwaka 2005 wakati Mhe. Dr. Jakaya Kikwete alipokuwa anawania uongozi wa juu kabisa wa nchi hii (urais) baadhi ya viongozi wa dini walisikika wakiushawishi umma wa watanzania kuwa Mh. Dr. Kikwete ndiye aliyekuwa chaguo la Mungu. Kampeni hii ilifanikiwa sana na hivyo kumwingiza Rais Kikwete madarakani kwa zaidi ya 80% ya kura zote za watanzania. Hapo hakuna aliyesema siasa na dini havichangamani wala kuhusiana, hakuna aliyekemea wala aliyekemewa.

Katika siku za karibuni viongozi hao hao wa kidini kwa nafasi zao na kwa uzalendo wao kwa mara nyingine wamejitokeza kuikosoa serikali na chama tawala kwa mambo wanayodhani yamekiukwa na moja kati ya mambo hayo ni kutupwa kwa rasimu ya Jaji Joseph Waryoba ambayo kimsingi ndiyo maoni ya wananchi. Hilo limezua balaa hadi kufikia wizara ya mambo ya ndani ya nchi kutishia kuzifuta NGOs, TAASISI ZA DINI ZIKIWA WALENGWA ikiwa zitabainika kujihusisha na mambo ya uchaguzi mkuu 2015 ama kuipinga katiba pendekezwa.

Je ni kweli kwamba siasa na dini haziingiliani? kama jibu ni ndiyo, kivipi?

Asanteni na karibuni kutoa mchango muhimu kwa wakati muhimu..tunapoelekea uchaguzi mkuu 2015.

 
Mkuu Descartes,

Pambanua basi angalau kimstari kimoja ili wengine nao tuone kutokufanana huko. Thank you!

Kwa kutaja machache:

Dini sio siasa.

Siasa sio dini.

Mwanasiasa anaweza kuwa na dini.

Mtu wa dini anaweza kuwa mwanasiasa.

Unaweza kuwa mtu wa dini usiyejihusisha na masuala ya siasa.

Pia unaweza kuwa mwanasiasa usiyejihusisha na masuala ya dini....
 
Kwa kutaja machache:

Dini sio siasa.

Siasa sio dini.

Mwanasiasa anaweza kuwa na dini.

Mtu wa dini anaweza kuwa mwanasiasa.

Unaweza kuwa mtu wa dini usiyejihusisha na masuala ya siasa.

Unaweza kuwa na siasa usiyejihusisha masuala ya pia dini....

Nimekupata mkuu. Kwa hiyo vongozi wa sasa wanawza kuwa viongozi wa dini am a wanadini? na kadhalika viongozi wa dini?
 
Mkuu Emmanuel,respect.siasa ni dini.viongozi wa kiroho/makanisa wana nguvu kubwa sana kwenye jamii yetu kwasababu wana wafuasi wengi nyuma yao.sasa serekali haina uwezo wa kufuta NGO's za kidini kwasababu kwa kifanya Hivyo ndio kujimaliza wenyewe.sana sana ngo's za makanisa ya kikatoliki au za waislamu
 
Mkuu Emmanuel,respect.siasa ni dini.viongozi wa kiroho/makanisa wana nguvu kubwa sana kwenye jamii yetu kwasababu wana wafuasi wengi nyuma yao.sasa serekali haina uwezo wa kufuta NGO's za kidini kwasababu kwa kifanya Hivyo ndio kujimaliza wenyewe.sana sana ngo's za makanisa ya kikatoliki au za waislamu
mkuu Ndusty, nimependa uchambuzi wako hapo mwanzo. Siasa nzuri inaweza kusaidia kutimiza malengo ya dini. so siasa ni dini na dini ni sasa? just curious
 
SIASA=DINI na DINI=SIASA.Bila SIASA dini haiwezi kuwepo na bila DINI siasa haiwezi kuwepo.Hivi vitu viwili vinategemeana,huwezi kuwa na kimoja kingine ukakiacha...

Ona viongozi wa SIASA wanavyohaha pale mambo yanapoharibika,utakuta hawaishi kuomba msaada kwa viongozi wa DINI,na vile vile viongozi wa dini mambo yanapoharibika hawaishi kuwaonya wanasiasa...

Tabu inakuja pale VIONGOZI wa dini wanapoingilia sinia la wanasiasa kwa kuwaonya..........Hapo ndipo mshikemshike unatokea.

Lakini pale wanasiasa wakiharibu ni mbio wanapishana kwenye makanisa na misikiti kuwaomba viongozi wa dini waombee AMANI,waongee na waumini wao nk nka.

Hivyo hawa wawili bwana ni MAPACHA wasiofanana,na pia inapofika mahali wakaomba kusaidiana...........Lakini mara zote huyu wa DINI ndiyo kiboko maana lazima mwanasiasa aende kupiga magoti hiko...............Maana ndiyo PACHA MKUBWA...........
 
Kwa upande wa dini ya kiislamu siasa ni mtoto wa dini km ilivo biashara ndowa n.k. kivipi? nipo safarini nikitulia nitaazisha thread mpya, kuhusu dini nå siasa , kwa saiz niombeni tu nifike salama kwenye safari yangu.
 
SIASA=DINI na DINI=SIASA.Bila SIASA dini haiwezi kuwepo na bila DINI siasa haiwezi kuwepo.Hivi vitu viwili vinategemeana,huwezi kuwa na kimoja kingine ukakiacha...

Ona viongozi wa SIASA wanavyohaha pale mambo yanapoharibika,utakuta hawaishi kuomba msaada kwa viongozi wa DINI,na vile vile viongozi wa dini mambo yanapoharibika hawaishi kuwaonya wanasiasa...

Tabu inakuja pale VIONGOZI wa dini wanapoingilia sinia la wanasiasa kwa kuwaonya..........Hapo ndipo mshikemshike unatokea.

Lakini pale wanasiasa wakiharibu ni mbio wanapishana kwenye makanisa na misikiti kuwaomba viongozi wa dini waombee AMANI,waongee na waumini wao nk nka.

Hivyo hawa wawili bwana ni MAPACHA wasiofanana,na pia inapofika mahali wakaomba kusaidiana...........Lakini mara zote huyu wa DINI ndiyo kiboko maana lazima mwanasiasa aende kupiga magoti hiko...............Maana ndiyo PACHA MKUBWA...........
Mkuu Tetty,

Unasomeka vizuri sana kwa kweli. Ni vigumu kuitenga siasa na dini. Katika Biblia siasa na dini viko pamoja tangu agano la kale na katika Koran bila shaka wanaamini vile vile. Wanasiasa ni waumini wa hizi dini. Mgogoro ni hapo wanapoonywa na viongozi wa dini. Hapo tu
 
Kwa upande wa dini ya kiislamu siasa ni mtoto wa dini km ilivo biashara ndowa n.k. kivipi? nipo safarini nikitulia nitaazisha thread mpya, kuhusu dini nå siasa , kwa saiz niombeni tu nifike salama kwenye safari yangu.

Mkuu Turufudume, huo ndio ukweli hata katika dini ya kikristo ingawa ni kama wakristu hawatii mkazo katika ukweli huo. Nakuombea safari njema!
 
Mkuu Tetty,

Unasomeka vizuri sana kwa kweli. Ni vigumu kuitenga siasa na dini. Katika Biblia siasa na dini viko pamoja tangu agano la kale na katika Koran bila shaka wanaamini vile vile. Wanasiasa ni waumini wa hizi dini. Mgogoro ni hapo wanapoonywa na viongozi wa dini. Hapo tu

Umeona eh!Wanpoonywa ndiyo shida na siyo wanaposifiwa au kuomba ULAJI toka kwa waumini.Na wanajua fika kiongozi wa dini akichomoa tu hakuna KURA....Na wanasiasa wanajua fika makosa yao na kwanini hawapendi kuonywa.Moja kubwa hawapendi kuonekana wabaya kwa wapiga kura wao....
 
Emmanuel

Kwa ufahamu wangu huwezi kutenganisha siasa na dini kwa sababu vyote vinamhusu mtu mmoja (binadamu).

Binadamu ana mwili, roho na nafsi. Binadamu huyu anahitaji chakula, malazi, afya, elimu, uongozi nk. Hayo ni mahitaji ya mwili ambayo ndio siasa yenyewe.

Binadamu huyu anahitaji kumwabudu Mungu msikitini au kanisani au mahali pengine popote anapoona panafaa.

Hayo ni mahitaji ya kiroho. Na mwisho binadamu huyu ana utashi wa kuchagua, kupenda na kutamani. Hayo ni ya nafsi.

Kumtenganisha binadamu huyu na yote hayo maana yake huyo hayuko hai tena, ni mfu.
 
Last edited by a moderator:
Siasa inapaswa kuwa siasa. Dini zitabaki kuwa za wajinga.
Anayechanganya siasa na dini ni mjinga, na wajinga ni loosers.
 
Kwa ufahamu wangu huwezi kutenganisha siasa na dini kwa sababu vyote vinamhusu mtu mmoja (binadamu).

Binadamu ana mwili, roho na nafsi. Binadamu huyu anahitaji chakula, malazi, afya, elimu, uongozi nk. Hayo ni mahitaji ya mwili ambayo ndio siasa yenyewe. Binadamu huyu anahitaji kumwabudu Mungu msikitini au kanisani au mahali pengine popote anapoona panafaa. Hayo ni mahitaji ya kiroho. Na mwisho binadamu huyu ana utashi wa kuchagua, kupenda na kutamani. Hayo ni ya nafsi.

Kumtenganisha binadamu huyu na yote hayo maana yake huyo hayuko hai tena, ni mfu.

Mkuu Danny Jully, nimependa sana maelezo yako. Big up!
 
Kwa upande wa dini ya kiislamu siasa ni mtoto wa dini km ilivo biashara ndowa n.k. kivipi? nipo safarini nikitulia nitaazisha thread mpya, kuhusu dini nå siasa , kwa saiz niombeni tu nifike salama kwenye safari yangu.

Mkuu Turufudume hujarudi safari? Unangojewa hapa kudadavua juu ya siasa kama mtoto wa dini ya kiislamu
 
Ninawaomba wanazuoni na wabobezi wa siasa wanipe tofauti ya msingi kabisa kati ya kanisa na chama cha siasa. Nitashukuru kama mtazungumzia yale makanisa ya mkoloni na haya ya kisasa pia vyama vya ukombozi na hivi vya mageuzi! Mods naomba msiunganishe uzi huu nipate elimishwa, Ahsante!
 
Back
Top Bottom