Siasa kwenye taaluma kama hospitali na vyombo vya habari

Kabachubya

Member
Oct 6, 2009
87
10
Jamani tutafika kweli?

Mimi naweza nikawapongeza ma DR kwa njia moja ya kuamuwa nao kuingia kwenye siasa na propaganda za kukubali wanachokisema wanasiasa ya kua wapo kazini lakini kwa hali halisi si kweli. Sasa hivi muhimbili hata panadol unaambiwa ukanunue.

Nikija kwenye vyombo vya habari ndio nachoka kabisa, hapo ndio nakiri kuwa tanzania hakuna proffesional kabisa, afisa habari ya Muhimbili anawaambia waandishi wa habari kuwa huduma zimerejea kama kawaida na wewe na camera yako unammurika basi unachukuwa bahasha yako unaondoka. Hata kusema upite wodini kuongea na wagonjwa hata wawili kupata ukweli ?
 
Harufu ya rushwa,rushwa imeitafuna sana nchi yetu mpaka inatia kinyaa uongo wa vyombo vya habari mpaka kwenye masuala yanayo husu maisha ya binadamu sasa tilipo tumeshindikana viongozi wetu wa serikali sasa wamrudie Mungu tumesha choka sana jamani hizi pesa wanazotumia kutengeneza propaganda kwenye vyombo vya habari pengine zingetuzogeza mahali kwenye sekta ya afya kwanini hawa watu hawafikiri hata kidogo wamekuwa kama maiti sasa anyway ngoja tuone.
 
Back
Top Bottom