Siamini kama CHADEMA ni chama kikuu cha upinzani naona kama pandikizi la CCM

RWANDES

JF-Expert Member
Jun 12, 2019
1,615
3,909
Chama cha demokrasia na maendeleo viongozi wake wamekuwa wakipambana kwa mambo mbalimbali hasa kuibua madudu ya serikali na wakati mwingine wengine kupewa kesi za uchochezi pamoja na yote hayo sakata kubwa ambalo liliibua hisia za wengi ni swala la Dp world ambao hadi viongozi wa kabisa katoliki waliamua kulivalia njuga na kupelekea kuandika waraka mzito uliosomwa kwenye vigango vyote vya kanisa Hilo nachojiuliza nini mbowe kimemkuta au ni kweli minongo'no inayosemwa tayari yeye na Tundu lisu A/c zao zimenona au nini hasa!

Naona hata swala la katiba mpya wanalisema kwa kulegeza misuli ya shingo si kama mwanzo nilivyokuwa namuona Tundu lisu akizunguka na kukaa kwenye vijiwe vya kahawa akiwaelimisha watu kuhusu katiba mpya.

Pamoja na yote yupo aliyewahi kuwa ndani ya mfumo wa serikali aliniambia kwamba CHADEMA huwa wanataka nusu mkate na serikali maswala ya kuhitaji kuongoza nchi CCm ndoo Baba lao na ndio wenye mifumo iliyoimara ya kupata viongozi na kukemea viongozi waliomo ndani ya chama hao wengine wameshashindwa kuweka mifumo Kila wote ni kambale na aliendelea kusema kwamba hawa ili upate uongozi ni kuwa jasiri na kutukana serikali na pia akitokea mwenye mtazamo tofauti na wao hufanyia Zengwe asipopotezwa bas mnakutana mahakamani jiulizeni haya-

Hivi ni kweli wale wabunge wanaowakejeli kwa Kuwaita COVID 19 mnaamini Ile kesi itatolewa maamuzi Leo Mwaka wa ngapi na uchaguzi ni lini ! Hao Jamaa waliamua swala Hilo liwe kwenye vyombo vya Sheria lakin ni kiini macho ili waendelee kuaminika kwa watu lakini Ile kesi ipo kimaagizo Kati ya viongozi wa CHADEMA na serikali.

Vijana endeleeni kumwita mbowe mwamba huku yeye na wenzake wanajutengenezea pesa.

Nawatakia alhamis njema bila kusahau kuwaombea vijana wetu wanaoendelea na mtihani wa kidato cha nne.
 
Tuletee chama chako ambacho sio pandikizi unadhani kuanzisha chama sawa na kula mihogo
 
We ndio unajua leo
F_CM5RmXYAAzxD7.jpeg
 
Back
Top Bottom