Si kila umuonae mshamba ni mshamba

Si kila umuonae mshamba ni mshamba

Unajua hapa bongo,kuna maviazi huwa yanahisi mtu ambae haishi dar basi ni mshamba.kumbe mtu unaweza ukawa unaishi zako arusha,moshi au musoma afu mishe zako unapigia hapo Nairobi..sasa wa Nairobi na wa dar nani mshamba?
 
Ushamba siyo kabisa haitakiwi iwe lifestyle hata kidogo, lakini pia usijidai mjanja sana balance nusu kwa nusu
 
Ushamba siyo kabisa haitakiwi iwe lifestyle hata kidogo, lakini pia usijidai mjanja sana balance nusu kwa nusu
Kuna watu hawapendi tu kujulikana wao ni smart hivo hupendelea kuishi kishamba(kama hawajui mambo vile)
 
Sahihi kabisa. Hapa ni nilipo kuna mlinzi mwenzangu nafanya naye kazi! Aisee ukimkuta yupo yupo tu. Comedian sana! Rafu rafu tu! Mwonekano wake ni kama ule wa Bongo muvi wanaoigiza maisha ya kijijini!

Ila ukija sasa kwenye masuala ya IT; jamaa yuko vizuri sana. Yaani mpaka wale jamaa wanaokaa maofisini na matumbo yao makubwa huwa wanakuja kumuomba msaada wa kubadilishiwa window kwenye PC zao na huyu mwamba! Hatari sana.
Mshauri jamaa ajikite kuendeleza ujuzi wake wa IT, Kuna siku utamlipa vizuri sana..
 
Tujuze kwanza maana halisi ya Ushamba na Mshamba, then turudi kwenye bandiko lako tumuangalie mfadhili wako.
Hilo ndilo Jambo la msingi kuna baadhi ya watu wa kanda Fulani hujiona wanajua Sana ili Hali ni weupe kabisa
hawana uwezo wa kujenga hoja chanya na umaskini kwako umetamalaki
 
Vijana wa 2000+ wanaamini ujanja ni kuchana suruali kwenye magoti, kunyoa kiduku na kutembea kama mtu aliyechomwa na mwiba na ndo hao hao ambao ukiwauliza mji mkuu wa kenye ni wapi wanakauka lips. Kulikuwa na kijana mmoja alikuwa anevaa jeans iliyochanika magotini, ananyoa kiduku halafu anajiona mjanja sana, Sasa Kuna siku tulikuwa tunaangalia laliga akawa anashindwa kutamka vizuri real Madrid akawa anasema "real magrid" mara siku nyingine akasema sei toto badala ya fei toto. Haya niambieni ujanja wa huyu dogo uko wapi, utopolo matupu.
 
Vijana wa 2000+ wanaamini ujanja ni kuchana suruali kwenye magoti, kunyoa kiduku na kutembea kama mtu aliyechomwa na mwiba na ndo hao hao ambao ukiwauliza mji mkuu wa kenye ni wapi wanakauka lips. Kulikuwa na kijana mmoja alikuwa anevaa jeans iliyochanika magotini, ananyoa kiduku halafu anajiona mjanja sana, Sasa Kuna siku tulikuwa tunaangalia laliga akawa anashindwa kutamka vizuri real Madrid akawa anasema "real magrid" mara siku nyingine akasema sei toto badala ya fei toto. Haya niambieni ujanja wa huyu dogo uko wapi, utopolo matupu.
Hao ni washamba wa kidijitali
 
nakubalina na wewe hata kwenye biashara jamaa wa vijijini na wazee wastahafu wana pesa sana unakuta unafanya biashara na mzee anakwambia subiri nikupatie pesa yani katezingatenga pesa zake kwenye vikopo vya mafuta ya kujipaka akija kukuhesabia huwezi amini wallah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom