Shule za Tusiime na athari za Corona

Shule za Tusiime na athari za Corona

Msulibasi

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2014
Posts
5,957
Reaction score
8,005
Ndugu wanabodi,

Baada ya serekali kutangaza kufunga shule zote za msingi na sekondari , Uongozi wa shule za Tusiime ulitangaza kuathirika kiuchumi hivyo kushindwa kulipa mishahara ya watumishi kwa shule zake za msingi na sekondari zilizopo Tabata Saanene..

Watumishi wakiwemo wapishi , madereva ,waalimu na matrons walipewa likizo bila malipo iliyoanza tarehe moja April hadi 29 June shule zilipofunguliwa.

Chakusikitisha baada ya watumishi kuripoti kazini walikumbana na barua za kusitishiwa mikataba yao ya ajira na hawakupewa stahiki zao ikiwemo mishahara ya Aprili , May na June.

Zoezi la kuondoa wafanyakazi limeendelea kushamiri toka hiyo June hadi sasa. Watumishi wengi wamepeleka madai mahakama ya kazi na wengine wameamua kunyamaza baada ya kupatiwa kiasi kidogo cha fedha.

Swali langu ni je ?Iweje Tusiime pekee ndio iathiriwe na Korona kwa haraka kiasi hicho hata kushindwa kulipa japo robo mshahara kwa miezi mitatu.

Iweje hata baada ya kufungua shule watumishi wasipewe japo nauli ya kuendea kazini mpaka waombe advance ya mshahara wa mwezi wa saba.

Hivi Tusiime inawezaje kufanya vurugu za kiwango hichi katikati ya jiji la Dar es Salaam na kuachwa kama kisiki?

Je, Serikali imepata kodi yake ya Aprili , May na June?
NSSF wamekusanya mafao ya Aprili May na June kutoka Tusiime?
Bodi ya mikopo je ?/mmepata 15% yenu?

Haki ya wanafunzi kupata huduma bora kutoka kwa watumishi kwenye uwiano sawa na wanafunzi inazingatiwa? Ni wajibu wa serekali yetu tukufu kumulika na kuondosha ubabe huu wa Tusiime . Patrobas Katambi anzia Tusiime.
 
Hii thread ilishaletwa humu kitambo sana. Nadhani hata mmiliki wa shule alikanusha hii kitu na akadai kuwa ni propaganda chafu dhidi yake.

Tusiime na shule zote za private walitudai sisi wazazi ada zao za mwaka mzima kama kawaida..
 
Tusiime tatizo miada mikubwa wanatoza hapo ndio maana wameathirika kwa kiwango kikubwa.
 
Pole Sana Mwalimu wa Tusiime, haya madai yafikisheni kwa maandishi kwa waziri wa elimu.
 
Tusiime Waje Wenyewe Wajibu Hoja
Kweli inabidi ifanyike hivyo maana haki ni muhimu kutendeka. Kama ile shule ya Arusha St Jude ilimulikwa iweje hawa waachwe wakivuruga taratibu na sheria
 
Kabisa kuna shule kibao wamekula pesa za watu wanawatishia kuwafukuza
Inasemekana jamaa ana ushawishi wizara ya elimu. Labda PCCB, ama wizara ya Nazi na TRA hao ndio wanaweza kusimama nae sio Ndelichako
 
Hii thread ilishaletwa humu kitambo sana. Nadhani hata mmiliki wa shule alikanusha hii kitu na akadaibkuwa ni propaganda chafu dhidi yake

Tusiime na shule zote za private walitudai sisi wazazi ada zao za mwaka mzima kama kawaida..
Ada za mwaka wakapokea , mishahara ya miezi mitatu wakachikichia , ngoma inakuja Kodi za TRA, NSSF, nao wanadai na hakuna sababu ya kushindwa kulipa kwani wizara iliekeza ada ilipwe yote.

Ni ajabu shule ifungwe March ushindwe kulipa hata robo mishahara kwa April ni ajabu lakini ndio kweli
 
Inasemekana jamaa ana ushawishi wizara ya elimu. Labda PCCB, ama wizara ya Nazi na TRA hao ndio wanaweza kusimama nae sio Ndelichako
Tumtafute naibu waziri katambi kwanza tuwasaidie watu
 
Ada za mwaka wakapokea , mishahara ya miezi mitatu wakachikichia , ngoma inakuja Kodi za TRA, NSSF, nao wanadai na hakuna sababu ya kushindwa kulipa kwani wizara iliekeza ada ilipwe yote.

Ni ajabu shule ifungwe March ushindwe kulipa hata robo mishahara kwa April ni ajabu lakini ndio kweli
Amelipwa pesa yote ya mwaka mzima anasema hakupata faida upuuzi mtupu .serkali ainagalie hili
 
Amelipwa pesa yote ya mwaka mzima anasema hakupata faida upuuzi mtupu .serkali ainagalie hili
Huyu mbabe Katagira au anajiita chairman anakuambia usijisumbue kumshitaki mahakama ya kazi au popote hutamweza .Ukitaka mishahara yako acha kazi. Cha kushangaza waliokuwa mbele kudai haki kawaachisha na hiyo mishahara hajawapa. Yaani huyu alitakiwa kufanyiwa kitu ya St Jude account zifungwe kabisa. Huyu mbabaishaji anapeta St Jude inadhibitiwa
 
Huyu mbabe Katagira au anajiita chairman anakuambia usijisumbue kumshitaki mahakama ya kazi au popote hutamweza .Ukitaka mishahara yako acha kazi. Cha kushangaza waliokuwa mbele kudai haki kawaachisha na hiyo mishahara hajawapa. Yaani huyu alitakiwa kufanyiwa kitu ya St Jude account zifungwe kabisa. Huyu mbabaishaji anapeta St Jude inadhibitiwa
Ataingia kwenye 18 tu tumemuona manji atakuwa hivi
 
Back
Top Bottom