Shule za binafsi zifutwe

Unashangaa zero na 4 kwa shule za watoto wenye vipaji maalum? hiyo ni kutokana na uchakachuaji ngazi walizotoka, siku hizi kuchakachua na kufaulisha sana ni sifa ya kumuongezea mtu idadi ya wanafunzi na hivyo mapato. Utashangaa mengi na huu utitiri wa shule binafsi za wafanyabiashara ambao hela ni kwanza mengine yote baadaye.

Tujiulize, elimu bora gharama yake kiasi gani?
Elimu bora, mwanafunzi anatakiwa kuandaliwa vipi kuimudu ngazi hii ya elimu...
Elimu bora, nani mdhamini wake, mzazi/mlezi, shule (education provider) na Serikali/Mzazi (financial provider), mwanafunzi (Anayeandaliwa kielimu), mwajiri/Ujasiriamali (Mtumiaji)

Je soko linahusishwa kujua ni product ipi inatoka mashuleni (wana-ICT, ma-engineers, Doctors, Nurses etc etc)
Mzazi anafuatilia uelewa wa mwanafunzi?
Mzazi/Serikali inaweka mazingira ya elimu sawa?
Mwanafunzi anachukua fursa zilizopo kujiendeleza mwenyewe?
Mzazi ana'invest hali na mali kumuwezesha mwanae apate elimu bora au ya mkato?
Haya ndiyo kati ya maswali tunahitaji kujiuliza na sio tu kuona uozo uliongia kwenye sekta ya elimu. Wamiliki wa haya mashule watazidi tu kukusanya hayo mapesa kama wahusika hawatajishughulisha kujua nini kunachotolewa pale kielimu.


Mfano, tukubaliane kuwa elimu bora gharama yake ni 500,000 TSH kwa mwaka, shule ina wanafunzi 500, je shule inaweza kuendeshwa kwa mil 20.8 kwa mwezi? Shule za serikali, gharama yao kwa mwanafunzi mmoja kwa mwaka ni kiasi gani?
Je wazazi wenyewe wanaweza kuanzisha shule ambayo uendeshaji wake hautakuwa wa kukimbilia profit bali education profit?

Maswali ni mengi sana jamani...
 
Zifutwe na serikali ipi? ya CCM?
Kaulize hizo shule zinazoitwa Saint ..... (yaani shule za watakatifu) zinamilikiwa na akina nani! Wabunge wa CC_, wakurugenzi wa serikali ya CC_, mawaziri wa serikali ya CC_, wenyeviti wa taasisi za CC_, wastaafu wa serikali ya CC_, n.k.

Haziko kwenye orodha ya kampuni za biashara na hawalipi kodi kwa vile ni shule za watakatifu ..... ingawa ada zake ni kuanzia 1m kwa mwaka na kuendelea hata kama ni za chekechea.

tukisema zifutwe kweli hatuta fika wanafunzi wengi siku iz itoshe shule za serekari zenyewe chach watafuta credeti watasoma wapi kama haito bado idadi ya watu inapanda kwa kasi tukizi funga tutasoma kweli. Ila nakubali ana na wewe kusema ni ghalama sana bac tuombe serekeri iweze kuzuia na kusimamia pia kubalansi ada zitozwazo na shule za watu binafsi kama ilivo kwa smatrd kwenye usafili!
 
tukisema zifutwe kweli hatuta fika wanafunzi wengi siku iz itoshe shule za serekari zenyewe chach watafuta credeti watasoma wapi kama haito bado idadi ya watu inapanda kwa kasi tukizi funga tutasoma kweli. Ila nakubali ana na wewe kusema ni ghalama sana bac tuombe serekeri iweze kuzuia na kusimamia pia kubalansi ada zitozwazo na shule za watu binafsi kama ilivo kwa smatrd kwenye usafili!

Ukifanya hivyo utapunguza tatizo ambalo baada ya muda litaendelea kukua, yaani unachosema ni tumeridhika kuwa serikali yetu haiwezi kujenga shule na kutoa elimu bora kwa kila mtoto wa tz??? tunakosea sana. Kodi yetu trilions wanapeleka wapi mishahara yao tu??? nauliza mishahara yao tu??? maana wale wa chini mishahara ni midogo kwa hiyo wakubwa mishahara na posho zao ndo zimalize kodi zetu???


Athari ya kuwa na taifa mbumbumbu ni kubwa mno, serikali ichukue jukumu la kutoa elimi pamoja na mashirka ya umma dini 100% sio private business people huwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.

Shule hizi zifutwe kwa maana ya wamiliki wa sasa wapewe fidia, shule zichukuliwe na serikali; serikali ichukue majukumu yake sio kuwatelekeza watz. Kwa sasa private school bei kubwa elimu duni, wizi wa mitihani umepata mbolea. Kwa hiyo tunapata hasara mara nyingi sana, kupoteza fedha wazazi, watoto kuwa na kiwango cha chini, taifa kuingia kwenye zama za wizi wa mitihani, siku hizi haiwezekani mtihani kutokuibiwa amini nakwambia, it is the order of the year.
 
Mzazi: Nimesomesha, nimemlipia ada kubwa, hakupata elimu, nani alaumie???
Mfanyabiashara: Nimewekeza nimepata faida, elimu sikutoa pesa nilichukua. nani alaumiwe???
Serikali: Tumethubutu, tumeweza, tunasonga mbele. Kauli na yanayotokea TZ ni utata mtupu? nani alaumiwe??
 
The good thing kila mtu yuko huru kutoa maoni, bad thing mtu anasema chochote kile, mie nilifikiri serikali ipunguziwe mzigo wa kuendesha shule na secta nyingine wakati sekta binafsi imeonyesha inaweza kuleta mabadiliko makubwa mazuri na kwa kipindi kifupi kuliko serikali iliyokuwa hewani 5o+ years na bado wanapiga jaramba katika mipango mikakati, sera na ilani zao.

Sekta binafsi ipewe uwezo na kuamniwa zaidi sasa, performance ya shule binafsi ni nzuri na inataia moyo na hakuna mhitimu asiyejua kusoma wala kuandika. Changamoto zipo na lazima ziwepo ili vichwa vifanye kazi na hili pia linagusa na sekta binafsi
 
The good thing kila mtu yuko huru kutoa maoni, bad thing mtu anasema chochote kile, mie nilifikiri serikali ipunguziwe mzigo wa kuendesha shule na secta nyingine wakati sekta binafsi imeonyesha inaweza kuleta mabadiliko makubwa mazuri na kwa kipindi kifupi kuliko serikali iliyokuwa hewani 5o+ years na bado wanapiga jaramba katika mipango mikakati, sera na ilani zao.

Sekta binafsi ipewe uwezo na kuamniwa zaidi sasa, performance ya shule binafsi ni nzuri na inataia moyo na hakuna mhitimu asiyejua kusoma wala kuandika. Changamoto zipo na lazima ziwepo ili vichwa vifanye kazi na hili pia linagusa na sekta binafsi

Mkubwa hiyo unayoita performance ya shule binafsi ni kwenye makaratasi watoto wako nying'i nyang'a. Mi naswali kama tumefika sehemu serikali leo tunasema ina mzigo mzito, naona tumepotea sana. kwani imeajiri watu wangapi? kwani tunalipa kodi ngapi? unakatwa kodi kwenye mshahara, pia ukienda kununua redio hela hiyo hiyo unalipa VAT, kodi juu ya kodi harafu tunasema serikali inashindwa hivyo mtu binafsi ataweza!!! unaangalia kwa kina madhara yake?? unafurahia A+ wakati watoto hawajui kitu?? hapo hawa jamaa ndo wametukamata kweli kweli.

Kweli hapa siongelei kuandika na kusoma tu, naongea kwa upana wake elimu ilivyo, TZ saa kila mtu anacheti kizuri fanya naye kazi utaona anachoweza kufikiri ni tofauti kabisa na cheti. Hii ndo maana tunalalamika kuwa wakenya na waganda watachukua ajira zetu, fikiria tena hili linakuwaje??? vyeti vizuri mbele uelewa mdogo kibao, lazima wenye uelewa mkubwa wachukue kazi haina mjadala.

Naomba serikali isije na ajiza, infanye lililokuwasudiwa kwa kuwepo kwake sio kulalamika na kutoa excuse kibao. Sekta binafsi, mtu binafsi kwa taarifa yako haaminiwi hata kwa maswala ya ndoa tu. Huwezi weka suala la kitaifa kwa watu binafsi, tumepotea. Kama unafahamau mambo hata digrii za marekani watu binafsi au india tunajua madhara yake; tunakwenda huko huko, mfanyabiashara hawezi kuchuja fedha mwalimu mmoja alisikika akisema baada ya kumwambia meneja wa shule watoto wako hoi wafanyiwe utaratibu kurudia darasa; hofu ya meneja wakirudia wazazi watawahamisha na hayuko tayari, ikabidi mwalimu aamuliwe kutafuta njia mbadala ili wazazi wafurahie maendeleo ya watoto, unajua mwalimu anafanya nini baada ya hapo??? kila mtoto aliwekewa nafasi 1-10 tu kati ya watoto 120.
 
Haki Elimu nao wameliona hilo; Umesikia tangazo lao hvi karibuni? Shule binafsi wanajadili namna ya kufanya mambo kila mtoto apite japo wamo ambao hali zao kimasomo ni duni.

Tuishauri serikali iachane na shule binafsi. Hawa wafanya biashara waende maeneo mengine ya biashara sio elimu.
 
ni bora ziwe na ubia fulani na serikali na sio kuzifuta kwa serikali yetu haina uwezo kwa kila kitu kama huduma kwa jamii,wafanye kama hizi hospitali za taasisi binafsi na za dini ambazo ziko katika mpango wa DDH sijui,ili shule ziendelee na zikaguliwe ubora wa elimusio bora kufaulisha.utasikia matokeo kata ya kwanza,tarafa ya kwanza,kiwilya ya kwanza ya kimkoa ya pili ya kitaifa ya kwanza,mlete mwanao ada m3.pia wanapita kuchagua wanafunzi wenye uwezo kwenye shule za msingi na kuwachukua kesho yake eti wao wanatoa taaluma safi.tuwe macho.
 
ni bora ziwe na ubia fulani na serikali na sio kuzifuta kwa serikali yetu haina uwezo kwa kila kitu kama huduma kwa jamii,wafanye kama hizi hospitali za taasisi binafsi na za dini ambazo ziko katika mpango wa DDH sijui,ili shule ziendelee na zikaguliwe ubora wa elimusio bora kufaulisha.utasikia matokeo kata ya kwanza,tarafa ya kwanza,kiwilya ya kwanza ya kimkoa ya pili ya kitaifa ya kwanza,mlete mwanao ada m3.pia wanapita kuchagua wanafunzi wenye uwezo kwenye shule za msingi na kuwachukua kesho yake eti wao wanatoa taaluma safi.tuwe macho.

Lazima kila mara tujue kipi kinaanza, kama serikali yako haina uwezo hiyo sio serikali, baada ya kutuletea vitu vya ajabu kusaplimenti serikali isiyo na uwezo ni bora ukawa shujaa ukasema kuhusu kuifuta serikali iliyopo tuleta nyingine yenye uwezo ili mambo muhimu ya kitaifa yabaki kuwa muhimu na ya kitaifa.
 
Hivi kwa nini imekuwa tabia yetu watz kupenda vyeti vikubwa vikubwa wakati uelewa wetu mdogo? huoni ni mfumo wa shule binafsi unachangia??? mtoto mwenye uwezo wa three anapata one kali, yeye anajua alifanyiwa makeke tena akiwa form 2 au 4; mtoto amefanyiwa mtihani akiwa darasa la 4 tena na la 7, sasa kweli taifa litakuwaje?? kama kila msomi anafikiria kuiba mitihani kwa vile amezoeshwa tangu primary??? suala hili hasa kwa shule binafsi.
 
sicbaliani na wewe hizo shule zinaleta changamoto ila zile zalizo anzishwa bila cutimiza masharti zifutwe na zenye maresults mbaya culico ada wanazolipa wanafunzi hizo ziletwe gvt, shule bora zipewe masharti zisishuce ciwango fulani cha ufahulu mfano c, ataeiba mtihan afungwe yeye 1 yr iwe fundisho.
 
Mbataa unaongelea wizi wa mitihani wewe. hayo masharti ya ufaulu ndo yanaitesa nchi hii, wamiliki wanatafuta shortcuts matokeo yake wanawafundisha watoto wa taifa hili kucheat kwenye mitihani; bado unazishabikia tu shule binafsi???? LAZIMA TUKUBALI KUNA MAJUKUMU YA SERIKALI NA SERIKALI LAZIMA IFANYE MAJUKUMU YAKE YOTE, yale muhimu kama elimu.

Kama watu hawaamini wizara ingefanya suprise visit kwenye shule hizi na maswali; kijimtihani kisimamiwe na watu ambao wamevisit just for 30minutes, madarasa tofauti tofauti kwa kila shule na siku tofauti au hata moja. UTASHANGAA!!

Ina maana unaamini Kiingereza ndo elimu??? basi wazungu wote ni wasomi wakubwa sana bila kujali umri!!! Watoto wetu wanafundishw akiingereza tena cha kuongea tu, kuandika spelling mistakes ni kibao.
 
Kwa kuzingatia hali ya mporomoko wa elimu, shule za watu binafsi zifutwe. Shule hizi zimechangia kuua elimu tena bila hata huruma, hawa jamaa wamegeuza elimu ya taifa hili kuwa ni biashara wakti serikali wakiangalia. Waziri wa elimu taifisha shule hizi kwa kuwapa fidia wamiliki.

Shule zibaki kuwa za mashirika ya dini, taasisi za umma na serikali tu.

Hebu fikiria wizi wa mithani ni hizi english medium, ada kubwa yaani wizi wa kuaminiwa, elimu duni yaani watoto hawafundishwi kama ambavyo inatengazwa na kuonekana kwa TV, Je mtoto atapata elimu kwa lugha asiyoijua?? as lower as class 1 or 2 at 7&8yrs of age????

Elimu biashara inamchango mkubwa kwenye kufa kwa elimu TZ, eti mtu anafaulu hajui kusoma wala kuandika haya ni mambo ya elimu biashara. WAZIRI FUTEENI SHULE ZA BINAFSI.

Nawasilisha

kazi kweli kweli. hivi huwa hampitii madaftari ya watoto wenu. Unaambiwa mtoto ni Bright, umewahi kummuliza swali na kupata ukweli. au unasubiri matokeo yaliyopikwa ya mwisho wa muhula, then ya taifa baada ya kuwafanyia mitihani?
Pole wee, utakuja kuumbuka asubuhi kumekucha, na baridi limeshakupiga usiku kucha.
Hapa kila mtu achukue hatua kivyake, hakuna aliyekushika mkono ukaibiwe na kudanganywa kwenye hizo shule.
chukua hatua.
 
kazi kweli kweli. hivi huwa hampitii madaftari ya watoto wenu. Unaambiwa mtoto ni Bright, umewahi kummuliza swali na kupata ukweli. au unasubiri matokeo yaliyopikwa ya mwisho wa muhula, then ya taifa baada ya kuwafanyia mitihani?
Pole wee, utakuja kuumbuka asubuhi kumekucha, na baridi limeshakupiga usiku kucha.
Hapa kila mtu achukue hatua kivyake, hakuna aliyekushika mkono ukaibiwe na kudanganywa kwenye hizo shule.
chukua hatua.


Kiliochangu pole sana, unawaza kama mtu mmoja mmoja, hoja yangu ni ya kitaifa, tunapaswa kuwaza kitaifa. Kama kuna watu wengi wanaibiwa ni kwa vile serikali inaruhusu aina hii ya wizi, ni kama fedha za NSSF, PPF, NPF, NIC, bahati nasibu za mitandao ya simu etc ni wezi ambao wamepewa kibali na serikali. Watanzania wanaumia sana kama nchi, lakini serikali kwa nini iruhusu wizi wa kiana kama huu?? mbaya zaidi kwenye sekta ya elimu tofauti na bahati nasibu za simu, taifa linaangamia kwa kupata wasomi wapumbavu!!!! utashangaa leo mikataba mibovu, huduma mbaya serikali, kodi kubwa kwa wafanyakazi etc kumbe ni uwezo mdogo wa watendaji kubuni na kupambanua mambo ambao wamepatikana kwa mfumo mbaya wa elimu. Taifa linaangamia.

Utashangaa hata mazoezi darasani mtoto anaandikiwa ili anakili tu, swali linajibu kabisa, anavema yote. hata ukimfuatilia home unaweza usigundue hali halisi (wazazi wanataka elimu bora wanafight huku na huko kuitafuta, kumbe wezi wamesajiliwa na serikali sasa mzazi afanyeje??? atoe pistol hadharani mdomoni mwa mmliki au meneja wa shule???) au unaweza ugundue kama sisi tulivyogundua. ON TOP of everything serikali isisajili wezi harafu iwambie wananchi wake tumia akili usiibiwe!!!! shame on the government.
 
Zifutwe? Wewe mwenyeo umefikiri Kwanza kama jina lako? Hizi shule za serikali zilizopo zimewashinda kushughulikia, wataweza kuongoza shule kubwa? Wewe unafikiri wataweza kuwalipa mishahara walimu wa shule zenye kutajika kana Feza? Hebu fikirikwanza kabla ya kuweka uzi. Kwani wizi wa mitihani uko katika private schools only? Kwani mitihani inatoka wapi? Kama inatoka NECTA na inavuja nani wa kumlaumu? Wewe leo ukiliona bunda la Laki 1 utaliwacha njiani na ulipite tu?
FIKIRIKWANZA
 
Kupitia madaftari ni hoja yenye mashiko lakini kweli na ukweli kwamba kwa nini serikali isajili wezi hawa unabaki palepale, mbaya zaidi ni shule zote za binafsi kwa lengo la kufaulisha sana ili kushawizi wazazi wenye uchu wa elimu ya watoto wao watoe fedha yoyote kupata nafasi, lengo la mzazi ni zuri apate elimu nzuri mtoto, lakni mdomo wa mamba ni hatari zaidi. Mzazi huyu amapoteza hata kile kidogo alichonacho. TUFANYE MAAMUZI MAGUMU KWA MANUFAA YA TAIFA.
 
Shule za private ndio bora hasa ziwepo, zinafundisha vizuri na zina walimu wazuri. Dunia nzima shule binafsi zipo nyingi tu. tena mi naona ni bora kabisa kwa mfumo uliopo kwamba kuna shule binafsi zinafanya mitihani ya cambridge kuliko ya NECTA, na kuweko colleges zenye kutoa vyeti vya nje kuliko vya hapahapa, usijekuomba ukasomeshwa na mwalimu aliekuwa mkulima vijijini, utakoma, ndo elimu yetu uswahilini, walioko juu hawataki kuwawezeaha wenzao wakafikia uwezo walionao lakini wenzetu walioko juu wanataka kuwawezesha wenzao wawe juu ili maendeleo yawepo!
 
Chilubi kwanza asante kwa mchango wako; lakini lazima kufikiri tena kufikiri mbali zaidi, wananchi waisimamie serikali ifanye kazi zake, period mkuu. sio serikali iwe legelege harafu tukubali kila kitu kiende mzoba mzoba eti vile serikali haiwezi kufanya majukumu yake, serikali ikishindwa kufanya yale ya kiserikali na kitaifa imekoma kuwa serikali jamani, ni kundi la wahuni tu.

Matrioni ya pesa wanalipana posho harafu unasema watawezaje kulipa mishahara minono??? ona aibu, ndo maana Ndugai alisema wabunge nao wafaidi, anajua kuwa serikalini watu wanafaidi zaidi ya kawaida, mbaya kwa ndugai ni badala apige vita akaona ni heri naye ale hata kama shule zitakosa walimu na mishahara bora.

Lazima pia ufikirie kwa nini wizi wa mitihani umekolea, ni shule binafsi na biashara ktk elimu. na kuonesha kuwa akili ni duni sana kwa wafanyakazi wa serikali matokeo ya wizi wa mtihani anafutiwa matokeo mtoto wa std 7, mwalimu, mmliki na baraza linabaki.
 
Je Watanzania, are we ready for mabadiliko katika sekta ya Elimu??? au bado tunataka tupotee zaidi kabla ya kuanza kuitafuta njia kwa gharama kubwa kuliko ilivyo sasa???
 
Back
Top Bottom