Shule ya Sekondari Scolastica katika kashifa nyingine

Anonymous

Senior Member
Feb 3, 2006
125
321
Wakati mmiliki wa Shule ya Sekondari ya Scolastica iliyopo katika Mji mdogo wa Himo mkoani Kilimanjaro,Edward Shayo akiwa mahabusu ya Gereza Kuu la Mkoa la Karanga akishitakiwa kwa mauaji ya aliyekuwa mwanafunzi wa shule yake,Humphrey Makundi,kashfa nyingine imeikumba shule hiyo.

Safari hii shule hiyo imeingia katika kashfa ya kuajiri walimu sita kutoka nchi za Kenya na Uganda ambao hawana vibali vya kufanyakazi nchini lakini ikapigwa 'deal' kati ya Wakili wa Serikali Bw,Chavula na Afisa wa Uhasmiaji ili wasifikishwe mahakamani na badala yake watozwe tu faini ya dola 600 kila mmoja.

Katika makubaliano hayo yanayodaiwa kumshirikisha Wakili mwingine wa Serikali aitwaye Kibwana ambaye imebainika naye si raia wa Tanzania,ilishauriwa Idara ya Uhamiaji isimshitaki mmiliki wa shule hiyo Edward Shayo kwa kuajiri wageni bali alimwe tu barua ya onyo.

"Sisi maofisa wa chini wa Idara ya Uhamiaji tunasikitishwa sana na double standard hii na hapa ofisini kwetu kuna jalada la uchunguzi juu ya uraia wa bwana Kibwana",wamelalamika baadhi ya maoiisa wa uhamiaji ofisi kuu mjini moshi.

Haya yanatokea wakati vijana zaidi ya 800,000 wanahitimu vyuo mbali mbali na kuingia kwenye soko la ajira wakiwamo walimu,lakini hawapati ajira kutokana na kazi zinazopaswa kufanywa na watanzania kuchukuliwa na raia wa kigeni kama kazi ya kufundisha.
 
Kuna Mtanzania anafundisha huku Kenya au Uganda bila kuwa na kibali cha kuishi na kufanya kazi?

Au Tanzania kama alivyosema Mzee Mwinyi kwamba ni shamba la bibi?
 
hii ni fitna na husda, ebu fanyeni kazi na heshimuni maamuzi ya wakubwa wenu!!
 
Mleta mada, niambie ilikuwaje huyo mwanafunzi akauawa na mmiliki wa shule? Taarifa nimeipenda.
 
Weka clip kama wema Sepetu au Amber Ruty kuondoa ukakasi na mzizi wa fitina. otherwise funga mdomo mabosi wale nchi.
kumbe dola 600 ni m ngapi vile ?
 
Wakati mmiliki wa Shule ya Sekondari ya Scolastica iliyopo katika Mji mdogo wa Himo mkoani Kilimanjaro,Edward Shayo akiwa mahabusu ya Gereza Kuu la Mkoa la Karanga akishitakiwa kwa mauaji ya aliyekuwa mwanafunzi wa shule yake,Humphrey Makundi,kashfa nyingine imeikumba shule hiyo.

Safari hii shule hiyo imeingia katika kashfa ya kuajiri walimu sita kutoka nchi za Kenya na Uganda ambao hawana vibali vya kufanyakazi nchini lakini ikapigwa 'deal' kati ya Wakili wa Serikali Bw,Chavula na Afisa wa Uhasmiaji ili wasifikishwe mahakamani na badala yake watozwe tu faini ya dola 600 kila mmoja.

Katika makubaliano hayo yanayodaiwa kumshirikisha Wakili mwingine wa Serikali aitwaye Kibwana ambaye imebainika naye si raia wa Tanzania,ilishauriwa Idara ya Uhamiaji isimshitaki mmiliki wa shule hiyo Edward Shayo kwa kuajiri wageni bali alimwe tu barua ya onyo.

"Sisi maofisa wa chini wa Idara ya Uhamiaji tunasikitishwa sana na double standard hii na hapa ofisini kwetu kuna jalada la uchunguzi juu ya uraia wa bwana Kibwana",wamelalamika baadhi ya maoiisa wa uhamiaji ofisi kuu mjini moshi.

Haya yanatokea wakati vijana zaidi ya 800,000 wanahitimu vyuo mbali mbali na kuingia kwenye soko la ajira wakiwamo walimu,lakini hawapati ajira kutokana na kazi zinazopaswa kufanywa na watanzania kuchukuliwa na raia wa kigeni kama kazi ya kufundisha.
Hiyo kashfa iko wapi? Mkinyimana mbege mnakuja JF ya GT kushitakiana!
 
Back
Top Bottom