Mdomomrefu
Member
- Jan 26, 2022
- 19
- 17
Habari watanzania wenzangu, poleni na mahangaiko ya dunia hii.
Mnamo trh 12.8.2021 Afisa wa elimu Wilaya ya Njombe Vijijini ndugu Mbwana Ndumbalu alifika shuleni Mtwango sekondari huku akiongozana na chombo cha dola, alifika na kudai kuwa shule imeshindwa kujiendesha bila ya watumishi hao kukubali kuwa wameshindwa kuiendesha hivyo alidai kuwa inachukuliwa na Serikali.
Kisha watumishi wakakubali lakini walihoji kuhusu haki zao. Afisa huyo alidai kuwa deni lote litalipwa na pia akaenda NSSF pia akasema wasiendelee kudai shule kwa kuwa deni lote litalipwa na Serikali. Kisha wakakubaliana kuwa mwisho ilikuwa ni Desemba.
Afisa huyo wa elimu alikwenda kwa commissioner na kusajili upya Shule kama ni ya Serikali na inadaiwa commissioner huyo ni baba yake mdogo. Na ilipofika Desemba walifunga shule bila ya uwepo wa Afisa huyo.
Januari watumishi hao wameendelea na hali ya sitofahamu huku Afisa huyo akimtumia academic master aliyesaliti wenzie akidai kuwa wanapaswa kuendelea hadi mwezi wa sita. Huku Afisa huyo akijua kuwa atastaafu mwezi wa tatu so kikombe atakikwepa.
Mimi binafsi nimeaona nilifikishe hapa JamiiForums kuutarifu umma kuwa shule inataka kuchukuliwa kiudhurumati bila ya hata Serikali kuu kujua.
Asanteni Sana kwa mda wenu
Mnamo trh 12.8.2021 Afisa wa elimu Wilaya ya Njombe Vijijini ndugu Mbwana Ndumbalu alifika shuleni Mtwango sekondari huku akiongozana na chombo cha dola, alifika na kudai kuwa shule imeshindwa kujiendesha bila ya watumishi hao kukubali kuwa wameshindwa kuiendesha hivyo alidai kuwa inachukuliwa na Serikali.
Kisha watumishi wakakubali lakini walihoji kuhusu haki zao. Afisa huyo alidai kuwa deni lote litalipwa na pia akaenda NSSF pia akasema wasiendelee kudai shule kwa kuwa deni lote litalipwa na Serikali. Kisha wakakubaliana kuwa mwisho ilikuwa ni Desemba.
Afisa huyo wa elimu alikwenda kwa commissioner na kusajili upya Shule kama ni ya Serikali na inadaiwa commissioner huyo ni baba yake mdogo. Na ilipofika Desemba walifunga shule bila ya uwepo wa Afisa huyo.
Januari watumishi hao wameendelea na hali ya sitofahamu huku Afisa huyo akimtumia academic master aliyesaliti wenzie akidai kuwa wanapaswa kuendelea hadi mwezi wa sita. Huku Afisa huyo akijua kuwa atastaafu mwezi wa tatu so kikombe atakikwepa.
Mimi binafsi nimeaona nilifikishe hapa JamiiForums kuutarifu umma kuwa shule inataka kuchukuliwa kiudhurumati bila ya hata Serikali kuu kujua.
Asanteni Sana kwa mda wenu