Shule ya msingi Shoga Chunya Tanzania

Shule ya msingi Shoga Chunya Tanzania

huenda kwa lugha ya asili ya huko chunya linamaa
na nzuri tu;watu chunya mtujuze
 
Nimepigwa butwaa kukuta shule inaitwa hilo jina la SHOGA hasa ukizingatia mkanganyiko wa kimaadili unao ikumba nchi yetu kwasasa kutoka na kushamiri kwa vitendo vya Ushoga. Nashauri wizara ya Elimu ione umuhimu wa kubadilisha jina la shule hiyo.

attachment.php

Chunya wengi ni wasafwa , usenge kwa kisafwa inatokana au ina maana ya KUFYEKA . Kwa kisafwa ukimwambia mtu kufyeka utamwambia USENGA , .. Sasa yawezekana walishindwa kutafsiri vyema wakasema usenge.
 
Hahaaa! umenikumbusha mbali sana. Nilipita wilaya fulani ya Mkoa wa Simiyu huko nyuma sana miaka ya 2000's nikakutana na shule ya msingi inaitwa jina lake kwenye ubao wa barabarani limeandikwa Shule ya msingi KUMALIJA, nikacheka sana. Miaka mitano baadaye nilipita shuleni hapo ( kwa bahati tu) nikakuta imebadilishwa jina.Nilipouliza kwa mwenyeji wangu ni kwa nini shule ile imebadilishwa jina? Akaniambia kuwa wanafunzi walikuwa wanafuta neno LIJA hivyo kuleta tafsiri mbaya. Kila walimu wakirekebisha jina wanafunzi wanalifuta tena kwa hiyo ukawa mchezo wa kuviziana kati ya walimu na wanafunzi. Baada ya walimu kuchoka wakaamua kubadilisha kabisa jina la shule ili kuondoa usumbufu. Hata hivyo jina hilohilo la KUMALIJA nimeliona limeandikwa ktk hoteli moja 'KUMALIJA HOTE'L pale stendi ya mabasi Nyegezi Mwanza. Sijui lina maana gani.
 
Back
Top Bottom