Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Hawa ni watoto wa shule ya Marys ingawa sijajua ni ya Mkoa gani lakini kwa aslimia 100 ni Tanzania
> Ndugu Watanzania hasa wenye watoto wanaosoma zile shule za kuchukuliwa na School Bus hivi mmewahi kufuatilia usalama wa Watoto wenu au mko busy na mambo yenu?
> Mmmewahi kufuatilia matumizi ya ada zenu, je mnatendewa haki?
Ebu shuhudie hao Malaika walivyorundikwa kwenye hicho kipanya. Wamiliki wa Shule wabadilike
MREJESHO: SCHOOL BUS ILIYOBEBA WANAFUNZI(WATOTO) 48 YAPIGWA FAINI NA KUACHIWA
-
Kwa mujibu wa vyanzo rasmi kutoka Jijini Mbeya, JamiiForums imethibitisha kuwa mmiliki wa gari hiyo alitozwa faini ya elfu 30
-
Aidha, faini hiyo ni kama onyo na endapo kosa hilo litajirudia basi wamiliki watafikishwa Mahakamani