Shughuli gani ataweza fanya aliyesom 'Bachelor of Science in Physics (BSC-PHYS)'?

akida jr

Senior Member
Jan 1, 2014
111
58
Habari zenu wanajukwaa,

Ndugu yangu amehitimu kidato cha sita 2018 mchepuo wa 'PCB' akafaulu kwa C kila somo. Ndoto yake ni kusoma Doctor of Medicine (MD) na hivyo aliomba kozi hiyo kwenye vyuo vitatu Muhimbili, KCMC na Dodoma (UDOM) chaguo lake la kwanza likiwa MD kila chuo. Matokeo yake amechaguliwa Udom kwa kozi ya 'Bachelor of Science in Physics (BSC-PHYS) ambayo ilikuwa chaguo la pili. Hata baada ya kufanya maombi awamu ya pili kwenye vyuo vya MUHAS na KCMC, hakukuwa na jawabu lolote.


Hata hivyo, kijana amekata shauri kwenda tu kusoma kozi hiyo hiyo aliyochaguliwa nayo, shida iliyopo ni kwamba hatujui hasa ni nini atafanya baada ya kuhitimu hiyo programu (yaani ni shughuli gani huwa wanafanya waliosoma hiyo kozi)?

Tafadhali nisaidieni mawazo kwa niaba yake.

Nawatakieni siku njema.
 
Huyo Anaweza Akawa Ni Mwalimu Japokuwa Hatakuwa Kama Aliesoma Ualimu Kabisa
 
Mwambie aache mara moja Hiyo bora asome coz nyingine hata pharmacy, lab, dentist, heri avumilia had mwakan kuliko kwenda kusoma hiyo coz ataishia kuwa ticha naifaham vzr Sana
 
Ila nchi hii ya ajabu sana yani. Mtu unalazimishwa kusoma kitu usichokitaka.

Mimi mwenyewe ni mhanga wa mambo haya. In the end unamaliza chuo hata hujielewi ufanye nini.

Asilimia 95+ ya wanafunzi wa vyuo Tanzania wanasoma mambo ambayo wao wenyewe hawakuyataka.

Imebidi tu kwa kuwa wamelazimishwa na breaucracy za vyuo na TCU.

Shame.
 
Ukiangalia kwa kina sio kila product ya chuo inasehemu ya kwenda....mitaala ya chuo kulingana na teknolojia na hali ya sasa maranyingi unakuta kuwa haviendani....na mitaala mingi inapaswa kuongezewa cozi mbali mbali ambazo zitafanya ziwe na mashiko mtaani. La serikali inapaswa kujua wale wataalamu wanaenda wapi na wakitoka pale na anapasea wakafanye nin....maana Tukiendelea hivi ni sawa na kusomesha watu wa kuwaacha wahangaike alaf unakuwa umepoteza mkopo uliyompa maana hujui ataurudishaje
 
Serikali inahimiza watoto wasome masomo ya sayansi wakati nafasi zenyew kwa vyuo vikuu ni chache...
Ila Madogo wengi wanakosa muongozo angejaribu nyingine za Afya tofauti na MD nadhani asingekosaa
 
Kuna broo anasoma hiyo koz udom anajutaa sanaa, anasoma ili apate boom tuu, anesema akimaliza anaenda kusoma clinical ofcers
 
Serikali inahimiza watoto wasome masomo ya sayansi wakati nafasi zenyew kwa vyuo vikuu ni chache...
Ila Madogo wengi wanakosa muongozo angejaribu nyingine za Afya tofauti na MD nadhani asingekosaa
Ni kweli ndugu bali dogo naye wakati ule aliweka ngumu. Alijaza hii aliyochaguliwa ili kuziba nafasi wazi, chuo nayo hawakufanya ajizi wamempeleka huko huko.
 
Ukiangalia kwa kina sio kila product ya chuo inasehemu ya kwenda....mitaala ya chuo kulingana na teknolojia na hali ya sasa maranyingi unakuta kuwa haviendani....na mitaala mingi inapaswa kuongezewa cozi mbali mbali ambazo zitafanya ziwe na mashiko mtaani. La serikali inapaswa kujua wale wataalamu wanaenda wapi na wakitoka pale na anapasea wakafanye nin....maana Tukiendelea hivi ni sawa na kusomesha watu wa kuwaacha wahangaike alaf unakuwa umepoteza mkopo uliyompa maana hujui ataurudishaje
Nakuunga mkono ndugu
 
Ila nchi hii ya ajabu sana yani. Mtu unalazimishwa kusoma kitu usichokitaka.

Mimi mwenyewe ni mhanga wa mambo haya. In the end unamaliza chuo hata hujielewi ufanye nini.

Asilimia 95+ ya wanafunzi wa vyuo Tanzania wanasoma mambo ambayo wao wenyewe hawakuyataka.

Imebidi tu kwa kuwa wamelazimishwa na breaucracy za vyuo na TCU.

Shame.
Pole, hapa itabidi dogo asubiri tu mwakani.
 
Hiyo ni mojawapo ya kozi za kibwege nchi hii.

- Kwa kuwa huwezi hata kuwa mwalimu labda kama utakuwa na 5M ili usome Post-graduate diploma in education. Vinginevyo utakuwa mwalimu wa part-time au private ukibahatika.

USHAURI.

- Soma kozi nyingine ya Afya kama;

- Pharmacy
- Dentistry
- Orthopedic Tech
- Medical Lab

- Kama una SALIO nenda nje ya nchi, kapige MBBS.
Kuna vyuo vizuri tu cheap China, Russia, Philippines ada zao hazizidi 5M per year.

Ukishindwa kabisa soma DIPLOMA,

- CO
- Pharmacy
- Dental Therapy
- Orthopedic
- Medical Lab
- EHO

Hutajuta,

Note.
Kumbuka hii nchi ni ya kizwazwa, hivyo ISHI KWA AKILI.
 
Mwambie aache mara moja Hiyo bora asome coz nyingine hata pharmacy, lab, dentist, heri avumilia had mwakan kuliko kwenda kusoma hiyo coz ataishia kuwa ticha naifaham vzr Sana
Sawa ASANTE
 
Pole, hapa itabidi dogo asubiri tu mwakani.
Hapana mkuu, nadhani kuna namna naweza kufanya baada ya kufika chuoni akabadilisha faculty/course.

Enzi nasoma chuo mimi miaka mitano iliyopita hili liliwezekana sijui kwa sasa.

Wataalamu mje mtoe msaada wa mawazo.
 
Back
Top Bottom