Shocking Truth Kutoka Loliondo

At least Mungu amekupanua kufikiri zaidi kuliko ushabiki wa kishirikina katika jina la Kanisa la..?
 
Mzazi wangu ana tatizo la moyo na mapafu, baada ya kupata dawa ya Babu alijisikia vizuri sana kiasi kwamba akaacha kwa muda madawa yake anayotumia kila siku ya hospitali. Ghfla hali imekuwa mbaya na miguu imevimba imebidi azirudie zile dawa kabla mambo hayajaharibika zaidi, anaendelea vizuri kwa sasa.

Pengine kikombe kimoja tu cha dawa ya Babu hakitoshi? inategemea na ukubwa wa tatizo au? au hii dawa vipi tena?
 
Nani aliwaita? wao na shda zao walitaka tiba...wakaenda kwa babu, na kama imani yao ilikua zero ndo kabisa..
 
Haya naona sasa majibu yanaanza kutoka,
we need more proof.
 
NYENYERE usiropoke tu kama vile unavyoenda chooni na kuachia makalio yako yatoe uchafu free.
Hayo unayoyasema khs Babu una uhakika ameongea yeye au unaskia habari kutoka kwa watu tu.
Hapa JF ni kwa great thinkers b4 u write u must do a research.

Kama hapa ni kwa great thinkers, then wewe pia you have to think great.
 

usitufanye watoto wadogo wewe. hapo kwenye bold unataka kutuambia

1. walikuruhusu ukaingia hadi chumbani kwao kushuhudia hiyo heshima ilivyorudi, au

2. ulipiga chabo?

3. walikuja kukupa taarifa ya performance ya chumbani kwao baada ya kikombe? na walikuambia wewe kama nani?

4. vipi, ulikuwa unajua performance yao kabla ya kikombe? na ulijuaje?

sasa, kawaambie hao waliopata heshima kwenye kikombe kuwa tunataka vyeti vya hospitali kabla na baada ya kikombe na sio shuhuda zinazotokana na illusion.

zaidi sana acha kudanganya watu,

muogope Mungu

ubarikiwe
 
Nani kasema babu anatibu KIFO? Wagonjwa walikufa, wanakufa na watendelea kufa hata kama watatumia kikombe au dawa za kisasa. Kama tarehe tayari mtu ana ondoka.
 
Nani aliwaambia waache kutumia dawa?

Mbona Babu anasisitiza watu waendelee kufanya matibabu ya kawaida hadi WAKAPIME afya zao Hospital?

Hao basi WALIDHANI vibaya na imewa-cost. RIP wao na hiyo Radio WAPO.

Sasa jamani, Mungu yupi anakuponya halafu anasema endelea kutumia dawa zako, ukiacha unakufa???????
 

Wasiopona ndio mnawaambia hawana imani, yaani mna excuse kwenye kila kitu...
 

Thats the thing, Nyenyere, they are not critically thinking. Wanashabikia kitu ambacho hata hawakielewi. Sasa hivi wanasema wasiopona hawana imani, na hapo watoto wadogo ambao hawajapona ni vipi sasa? Alianza kwa kusema kuwa unapona baada ya siku saba, sasa hivi kaongeza kuwa ni miezi mitatu. This is so crazy.....
 

Hivi Radio Wapo inamilikiwa na nani? Imekuwa propaganda "machine" against "Babu wa Loliondo"!

Tumeambiwa "time and again" kuwa Babu anaponya kwa "IMANI" and so the Holy Bible Says

Mark 10:52 "Go, for your faith has healed you.."

Kwa hiyo kama "HUNA IMANI" huwezi kupona!! Strange!
 
swala la loliondo ni ''confusion'' kubwa sana....

lawama za teamo na familia yake zinawaangukia watu wa MEDIA moja kwa moja.....!

hizi media hizi zitawajibishwa kwenye hivi vifo pia
 
Nina ushahidi wa mgonjwa mmoja wa kisukari. Alipotoka kwa babu alikuwa anatamba kuwa KAPIGA KIKOMBE cha babu na aligonga soda mbalimbali njiani. Baada ya siku saba kapima kakuta sugar as usual.

Sasa tuamini nini kwa shuhuda hizi?

Umetoa mfano mmoja kwa madhara,huenda hukuwa unajua ila ninajua watu zaidi ya 20 waliopona kabisa sukari akiwemo Lyatonga. Endelea kupinga.
 
Ukweli utajulikana hivi punde!!
 
Nani aliwaambia waache kutumia dawa?

Mbona Babu anasisitiza watu waendelee kufanya matibabu ya kawaida hadi WAKAPIME afya zao Hospital?

Hao basi WALIDHANI vibaya na imewa-cost. RIP wao na hiyo Radio WAPO.

Mkuu hapa sijakuelewa vizuri, unasema watu waende hospitali au kwa babu? Au unamaanisha babu hatibu na anataka watu wamtemblee au anafanya majaribio!
 
Unajua maneno ya KUSIKIA mitaani huwa yanachanganya sana watu. Tatizo ni kuwa hakuna waandishi wa habari MAKINI waliokwenda kwa Babu na kumuuliza maswali na majibu wayatowe kwenye magazeti na redioni ili watu wajuwe haswaa nini watapata huko kwa Babu na nini wafanye baada ya kutoka kwa Babu.

Babu kwa mfano hapa chini anasema kabisa kuwa "ukiumwa kichwa, nenda upate panadol............"

Tafadhali jitahidi uangalie video kadhaa YOUTUBE ambazo BABU mwenyewe anaongea na si hizi STORY unasikia mitaani.

Mkuu hapa sijakuelewa vizuri, unasema watu waende hospitali au kwa babu? Au unamaanisha babu hatibu na anataka watu wamtemblee au anafanya majaribio!
 
Last edited by a moderator:
Kwa hiyo unakubaliana na wale Wasabato SIJUI ambao walikaa Msituni na kuamini kuwa MUNGU atawaletea chombo ili WASAFIRI majuu?? Unataka kusema kuwa Mungu akikutibu basi USILE kwa sababu UNA IMANI?

Unataka kusema kuwa kama una IMANI basi unaweza usifanye KAZI na Mungu atakupa chakula?

Hii IMANI naona mnaichezea sasa. Kumbuka sisi ni KIZAZI cha Adamu na Mungu kasema kuwa TUTAISHI KWA JASHO LETU.

Kama Mwili wa Binadamu umedhoofika, inabidi URUTUBISHWE. Unaweza kuwa una HIV ila kumbuka kuwa HATA MAFUA yanaweza kukuuwa. Babu anaweza kukutibu na VIRUS wakafa wote ila kumbuka mwili wako bado uko dhaifu na inabidi ULE na kutumia madawa ya kurutubisha mwili.

Nashindwa kuelewa kitu kigumu hapa. Kama huamini, ACHA KWENDA na waache waende wanaoamini. Labda kama BABU kaharibu SOKO LAKO na sasa hivi wewe na jamaa zako MATAPELI, kipato chenu kimekuwa HOI.

Bahati nzuri, Tanzania ina eneo kubwa sana. Nendeni Mkalime na mtuondolee hivyo vihuruma vyenu kwa Watanzania. Tangu lini mmekuwa na huruma kwa Watanzania? Mbona CCM inauwa watu kila siku na hatujawahi kuwasikia MKILALAMIKA? Akina Kakobe/Kulola/Mwingira type utawajua tu na vidinidini vyao na kujifanya wanawajali sana Watanzania.

Heri yangu mie SINA DINI. Lakini kama sina njia ya KUPONA, ntaenda kwa BABU. At the end of the day, I HAVE NOTHING TO LOOSE.
Sasa jamani, Mungu yupi anakuponya halafu anasema endelea kutumia dawa zako, ukiacha unakufa???????
 
Wakati ni muamuzi mzuri sana wa mambo. Mi naamini ipo siku tu ukweli utajulikana.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…