DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mgombea ubunge wa Jimbo la Ukonga kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Bakari Shingo amesema uteuzi wake si wa bahati mbaya bali ni dhamira ya chama chake kuhakikisha changamoto zinazowakabili wananchi jimboni humo zinapatiwa ufumbuzi.
Akizungumza jana Septemba 15, 2025 katika uzinduzi wa kampeni uliofanyika viwanja vya Mombasa, Kata ya Ukonga, Shingo amesema wananchi wa jimbo hilo wamesumbuliwa kwa muda mrefu na ukosefu wa maendeleo licha ya kuwa na viongozi waliopata nafasi kubwa serikalini.
“Hatugombei kwa bahati mbaya, tumegombea kwa sababu tumevurugwa. Kijana tuliyemuamini ameshindwa kutulipa hisani. Hatujapata mwakilishi anayeishi na kushirikiana na wananchi wake. Ndiyo maana tumeamua kusimama kudai haki ya watu wa Ukonga,” amesema Shingo.
Amezitaja changamoto zinazolikabili jimbo hilo kuwa ni pamoja na ukosefu wa stendi ya mabasi, soko, miundombinu duni, msongamano wa wanafunzi mashuleni, michango isiyo halali katika shule na mfumo mpya wa ulipaji vibali vya marekebisho ya nyumba bila elimu kwa wananchi.
Akizungumza jana Septemba 15, 2025 katika uzinduzi wa kampeni uliofanyika viwanja vya Mombasa, Kata ya Ukonga, Shingo amesema wananchi wa jimbo hilo wamesumbuliwa kwa muda mrefu na ukosefu wa maendeleo licha ya kuwa na viongozi waliopata nafasi kubwa serikalini.
“Hatugombei kwa bahati mbaya, tumegombea kwa sababu tumevurugwa. Kijana tuliyemuamini ameshindwa kutulipa hisani. Hatujapata mwakilishi anayeishi na kushirikiana na wananchi wake. Ndiyo maana tumeamua kusimama kudai haki ya watu wa Ukonga,” amesema Shingo.
Amezitaja changamoto zinazolikabili jimbo hilo kuwa ni pamoja na ukosefu wa stendi ya mabasi, soko, miundombinu duni, msongamano wa wanafunzi mashuleni, michango isiyo halali katika shule na mfumo mpya wa ulipaji vibali vya marekebisho ya nyumba bila elimu kwa wananchi.