Napenda kuwapa tano wachoma nyama ya mishikaki na ndizi pale mikumi ukitokea Morogoro, kwa kweli nyama zenu ni tamu hatari na kubwa si mchezo mpaka raha, nikipitaga mikumi lazima ninunue mishikaki kama rambo 2 hivi, ni kutafuna kwa kwenda mbele mpaka Iringa, ila isije kuwa mnatulisha nyama za mbwa na paka, eti mnalipaga TRA kwa kuuza hizo nyama? Shauri zenu Magufuli anakuja