Shikamoo ni salamu ya ovyo

Ishiiiiiy watembee na kadi za clinic.

Swali la kizushi: juzi tulikuwa na mashoga zangu umbea wa hapa na pale likazuka swali!

Let say mdada ana 30yrs ana date mbaba wa 55 yrs. Kabla ya kudate heshima kibao kama anapokea ekaristi.

sasa ndo ku date haswa hivi kikatiba isiyo rasmi huyu mwanaume shikamoo yafaa kuendelea kumzeesha tena?

Wanaume mkuje mjibu haraka mnatuchanganya. Sasa mtu umelala nae the same bed at asubuhi "shikamo" hii imekaaje?

Mko wapi wanaume nawasubiri hapa!!!
 
Kusalimia inaonekana kama inawapa watu shida sana.

Mimi awe mdogo ama mkubwa akitaka shikamoo nampa kwa sababu hainipunguzii wala kuniondolea chochote.

Kwenye jamii ama kabila letu, mkubwa anaweza kuanza kumsalimia mdogo ama baba akamsalimia mtoto ama mama akamsalimia mtoto na ila anaanza na salamu ya kuitikia, mfano, shikamoo inatolewa na mdogo, mkubwa anaitikia marahabaa, sasa kikwetu mkubwa anaweza kuanza na marahabaa wewe ukamalizia shikamoo.

So sisi hatuna ulazima nani aanze, ila salamu lazima ipo.

Mtu kumpa shikamoo inakuuma nini? Polepole alisema, mpe shikamoo hata 9 kwa siku anaezitaka.
 
Nikimwangalia mtu zaidi ya sekunde tatu nisijue nampa salamu gani basi nakusha tu
Eeeh kama hataki anapita hv me nikikutana na mtu nikimsalimia asiitikie anaefuata huwa simsalimii ya kwanza ina-replace wa pili
 

Salamu ya Kishenzi sana hii, upuuzi mtupu.
 

Washakua wapenzi hao, washaunganisha vikojoleo so hakuna tena shikamoo.
 
Kuna kimama nilikutana nacho kwenye bajaji nikakiambia "za saa hizi" kikaniletea jau eti "unalingana na mwanangu wa kwanza, nipe shikamoo yangu" yaani tabu tupu
Umetumia lugha chafu sn na kweli umeonesha jinsi usivyo na adabu. Yani mama wa watu tena mtu mzima unamuita "kimama". Kizazi hiki laana tupu. Vipi angekuwa mama yako ndo anaitwa"kimama" utajiskiaje.
 
Shikamoo imenasa kwemye damu, kuiondoa ni kazi! Mtu akikuzidi umri shikamoo ni halali yake.
 
Kumbe tupo wengi daaaah
 
Kuna kimama nilikutana nacho kwenye bajaji nikakiambia "za saa hizi" kikaniletea jau eti "unalingana na mwanangu wa kwanza, nipe shikamoo yangu" yaani tabu tupu
Ahaahahah[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…